Iringa: DC Kasesela aokoa roho za watu kwenye ajali ya Mlowa

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,483
54,853
Mkuu Wa Wilaya ya Iringa akitoka kwenye kusikiliza mgogoro wa wakulima na wafugaji Idodi, alikuta ajali ndio imetokea ikabidi asimame na kuanza kuokoa majeruhi ambapo dereva alikimbizwa hospital ya mkoa na amelazwa wodi 5 katika hospital hiyo hali yake inaendelea vizuri

Dereva aliyetambulika kwa jina moja tu Michael Mkoroma akiwa na abiria Deogras Luoga na Miraji Mohamed wote watumishi Wa chuo cha DUCE walikuwa kwenye gari

Gari ya chuo kikuu kishiriki DUCE ilikuwa ikitokea kwenye ziara ya utafiti Ruaha National Park ilipinduka kwenye kona ya Mlowa kutokana na barabara kuwa na tuta pamoja na viinuko vidogo vidogo maarufu kwa jina la rasta
c6dd613c84e0b43bfd3f2a5196225f3e.jpg
fe574d9be4eb9657cb8eef6245d5809f.jpg
c89d3126d86d1c17823ffcdf7175cee6.jpg
0f015b2133509d7eee5605fe3e4cf8c7.jpg
5dd7b12deac61d8731e0ae2dd43371f7.jpg
c44dd59d199cdf1e86a7c19b64672cb1.jpg
537551ef459a67f075b6884fbac68165.jpg
58f862cc6b6522887b92b1d5a62cbb2a.jpg
9fca0c74a9807f46401145e89bf8d5c8.jpg

Mkuu Wa wilaya mhe kasesela mwenye shati jeupe la maua akiongoza kunyanyua gari
 
Hio barabara kama sio mzoefu ni mbaya sana..utafikiri haiendi ruaha national park
 
Ila Kasesera kwa kiki yupo juu. Yeye kuokoa tu. Mara utasikia "... kaokoa watu kwenye mafuriko Idodi, kabeba waathirika kwenye janga. Na hii amenyanyua gari kwa mikono yake mwenyewe..."! Safi lakini.
 
aiseee sasa huyu driver anaitupaje mahali kama hapo ? angeingia ngorongoro crater ingekuwaje / rasta ya serengeti
Pole majeruhi wote.Daah umenikumbusha barabara ya Ngorongoro-Mar(l?)anja,Naabi,Seronera,Ikoma/Ndabaka.Hiyo ndiyo barabara hatari ya rough road kwa Tanzania kama sijakosea.Ina mbavu za mbwa,mawe(loose rocks) na kona kona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom