Iringa: Ahukumiwa kunyongwa baada ya kumtupa mtoto wake Mto Ruaha

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,365
8,097
Mahakama ya Hakimu Mkazi iliyopewa mamlaka ya ziada mkoani Iringa imemuhukumu kunyongwa hadi kufa Abuutwalib Seif (34) Mkazi wa Igumbilo, baada ya kukutwa na hatia ya kumuua kwa kumtupa mtoto wake Khadija Seif (5) mto wa Ruaha. Mtoto alikuwa ni mlemavu wa viungo.

Akisoma kesi hiyo jana Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Said Ally Mkasiwa amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akijishughulisha na kazi ya upigaji debe katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Igumbilo.

Aidha kwa mujibu wa taarifa za mahakamani hapo, mtuhumiwa alikuwa akiishi na mtoto huyo ghafla akawa haonekani na alipoulizwa na majirani alisema amemrudisha kwa bibi yake.

"Mwili wa mtoto huo ulipopatikana akiwa amekufa Mto Ruaha majirani walimfata na kumwambia mtuhumiwa lakini hakuonesha Jitihada zozote za kwenda kuuchukua ndipo akakamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi," amesema hakimu huyo.

Kesi hiyo ilikuwa na mashahidi 6 wakiwemo majirani waliothibitisha kumtambua mtoto huyo ambaye alikuwa mlemavu wa viungo ndipo mahakama ikamtia hatiani mtuhumiwa huyo kwa kutenda kosa.

Akitoa malezo yake ya awali mtuhumiwa amekiri kumtupa mtoto huyo Mto Ruaha saa 8 usiku kutokana na hali ngumu ya maisha iliyokuwa ikimkabili.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Magreth Mahundi aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa ambaye ametenda kosa hilo kwa mtoto wake wa kumzaa.

Kwa upande wake wakili aliyemsimamia Mtuhumiwa Cosmas Kishamawe aliiomba Mahakama kumuachilia huru mtuhumiwa kwa sababu ni kosa la kwanza na ana mtoto na wazazi wake ambao wanamtegemea na umri wake bado ni mdogo hivyo ana ndoto nyingi ambazo angependa kuzitimiza.

Hata hivyo mahakama ikamuhukumu kifungo cha kunyongwa mpaka kufa kwa kosa la kumtupa mtoto wake akiwa hai katika Mto Ruaha.

MWANANCHI
 
Dunia ina mambo mengi , MUNGU azidi kutusaidia tu, mwanao wakumzaa hata awe mlemavu sidhani kama unaweza kumtupa, huyu aliingiliwa na pepo labda.

Sheria nayo ni msumeno, sasa imemnyoosha mshitakiwa.
 
Kwa upande wake wakili aliyemsimamia Mtuhumiwa Cosmas Kishamawe aliiomba Mahakama kumuachilia huru mtuhumiwa kwa sababu ni kosa la kwanza na ana mtoto na wazazi wake ambao wanamtegemea na umri wake bado ni mdogo hivyo ana ndoto nyingi ambazo angependa kuzitimiza.
... utetezi wa kipimbi kweli kweli! Ila jamaa katili kinoma; unamuua mwanao kisa mlemavu? Dah!
 
Hivi kabla ya kunyongwa hakunaga adhabu nyingine mtu anaweza Pewa Kisha ndo anyongwe?
Umeuliza swali fikirishi sana. Maana Kunyongwa sio adhabu bali ni kuuawa.

Wakati Adhabu ni tendo/hali anayolazimishwa mtu kuifanya ambayo inamsulubu ki-hali/kifkra ili ajutie alilolifanya.
 
Maskini mtoto, tena wa miaka mitano mbaya zaidi anatupwa na baba yake mzazi ambae angepaswa kumlinda,
Hakika siku ya kiyama tutakimbiana
Imagine mtoto anakutanishwa na baba yake alie muua? Bado nawaza
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi iliyopewa mamlaka ya ziada mkoani Iringa imemuhukumu kunyongwa hadi kufa Abuutwalib Seif (34) Mkazi wa Igumbilo, baada ya kukutwa na hatia ya kumuua kwa kumtupa mtoto wake Khadija Seif (5) mto wa Ruaha. Mtoto alikuwa ni mlemavu wa viungo.

Akisoma kesi hiyo jana Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Said Ally Mkasiwa amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akijishughulisha na kazi ya upigaji debe katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Igumbilo.

Aidha kwa mujibu wa taarifa za mahakamani hapo, mtuhumiwa alikuwa akiishi na mtoto huyo ghafla akawa haonekani na alipoulizwa na majirani alisema amemrudisha kwa bibi yake.

"Mwili wa mtoto huo ulipopatikana akiwa amekufa Mto Ruaha majirani walimfata na kumwambia mtuhumiwa lakini hakuonesha Jitihada zozote za kwenda kuuchukua ndipo akakamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi," amesema hakimu huyo.

Kesi hiyo ilikuwa na mashahidi 6 wakiwemo majirani waliothibitisha kumtambua mtoto huyo ambaye alikuwa mlemavu wa viungo ndipo mahakama ikamtia hatiani mtuhumiwa huyo kwa kutenda kosa.

Akitoa malezo yake ya awali mtuhumiwa amekiri kumtupa mtoto huyo Mto Ruaha saa 8 usiku kutokana na hali ngumu ya maisha iliyokuwa ikimkabili.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Magreth Mahundi aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa ambaye ametenda kosa hilo kwa mtoto wake wa kumzaa.

Kwa upande wake wakili aliyemsimamia Mtuhumiwa Cosmas Kishamawe aliiomba Mahakama kumuachilia huru mtuhumiwa kwa sababu ni kosa la kwanza na ana mtoto na wazazi wake ambao wanamtegemea na umri wake bado ni mdogo hivyo ana ndoto nyingi ambazo angependa kuzitimiza.

Hata hivyo mahakama ikamuhukumu kifungo cha kunyongwa mpaka kufa kwa kosa la kumtupa mtoto wake akiwa hai katika Mto Ruaha.

MWANANCHI
Ni laana ktk taifa. Kwa Rasimali tulizonazo, nadhani tulipaswa kuwalea walemavu wote nchi nzima. Walipaswa wawe na makazi bora, chakula etc. Hii hukumu ni mapungufu
 
Hivi kabla ya kunyongwa hakunaga adhabu nyingine mtu anaweza Pewa Kisha ndo anyongwe?
Kukaa mahabusu ukisubiria siku tarehe na mwaka ambapo mnyongaji atakuja ujui ni lini,hii ni adhabu tosha kabla ya kitanzi chenyewe,faida ni kwamba unapata mda mwingi Sana wa kuomba toba kwa Mola wako so unakufa kifo cha amani
 
Kukaa mahabusu ukisubiria siku tarehe na mwaka ambapo mnyongaji atakuja ujui ni lini,hii ni adhabu tosha kabla ya kitanzi chenyewe,faida ni kwamba unapata mda mwingi Sana wa kuomba toba kwa Mola wako so unakufa kifo cha amani
Unahisi mkuu ni Sawa kumpa yeye kifo cha Amani na kumpa nafasi ya kutubu wakati yeye hakutoa vyote hivyo kwa mtoto aliyemuua?

Kwanini mtu kama huyu tunampa nafasi ya kula chakula kizuri Bure, kukaa kwa Amani Bure akisubiria huko kunyongwa na zaidi anapewa nafasi kujiandaa kwa kutubu na mengineneyo wakati yeye kadhulumu uhai wa mtoto asiye na hatia, kamtupa mtoto aliwe na mamba na unajua kisaikolojia inauma kiasi gani kwa mtoto ambae Anamuona baba yake kama mlinzi mkuu lakini ndio ansukumiza mtoni aliwe na mamba?
 
Huyo mtoto aliumia kiasi gani kuona baba yake kama ndie Mungu wake duniani akimtupa bila huruma majini.
Hata kama maisha ni magumu kiasi hicho, yaani unapiga debe uhakika wa mia 2 upo vipi wasio na hata matumaini wanakoroga uji na siku inasonga
 
Back
Top Bottom