Iraq: Polisi wawatishia Waandamanaji kwa kutumia Mbwa, Waandamanaji wajibu kwa kuleta Simba

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,442
3,353
Tangu Oktoba 01, 2019 Wananchi wa Iraq walianza maandamano ya dhidi ya Wanasiasa wanaoongoza nchi hiyo wakiwashutumu kwa mfumo uliokithiri rushwa na utawala usiokidhi katika kuongoza nchi

Taarifa zinadai kuwa siku za hivi karibuni, Polisi wanaopambana na Waandamanaji hao waliwatishia Waandamanaji kwa Mbwa waliofunzwa. Katika kujibu mapigo mmoja wa Waandamanaji aliandamana na Simba akishishia kumuachia Simba huyo kuwashambulia Mbwa wa Polisi na Polisi wenyewe

1.jpg

2.jpg

Takribani watu 319 wakiwemo Waandamanaji na Polisi wamefariki tangu kuzuka kwa maandamano hayo Kamati ya Bunge ya Haki za Binadamu imebainisha hayo

Waandamani wanaofunga mitaa, hususani Vijana wameigawanya nchi hiyo katika vipande viwili kipande cha mji mkuu Baghdad na Kipande chenye utajiri wa Mafuta Kusini mwa nchi hiyo

Makundi kadhaa ya Haki za Binadamu hivi karibuni wamelalamikia Polisi kwa kutumia nguvu zaidi katika kutuliza Waandamanaji hao

Amnesty International imezitaka Mamlaka za nchi hiyo kuvitaka vikosi vya kutuliza ghasi akutotumia nguvu, ikisema waandamanaji sita walifariki Jumamosi katikati ya Baghdad
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Huyo simba ni mtiifu kiasi gani hata asirarue waandamanaji kwanza akararue mbwa
 
Tangu Oktoba 01, 2019 wananchi wa Iraq walianza maandamano wakidai kukithiri kwa rushwa na utawala usiokidhi matakwa ya raia katika kuongoza nchi hiyo. Umasikini, elimu, maji safi, haki za binaadamu, uonevu, na dhiki iliokithiri kua chanzo kikuu cha raia kuandamana.


Inadaiwa Polisi wanaopambana na waandamanaji hao wanatumia "MBWA" waliofunzwa ili kuwatawanya waandamanaji hao, lakini katika kujibu "MAPIGO" mmoja wa waandamanaji aliandamana na "SIMBA" akitishia kuwashambulia "MBWA" wa Polisi na "POLISI WENYEWE".

Takriban watu 319 wakiwemo waandamanaji na Polisi wamefariki tangu kuzuka kwa maandamano hayo, huku Makundi kadhaa ya Haki za Binadamu wakilalamikia Polisi kwa kutumia nguvu zaidi katika kutuliza waandamanaji hao.

-IndependentUK
images.jpeg
iraq-protest.jpeg
dmix_4.png__655x0_q85_crop_subsampling-2_width-655.jpeg
 
Simba katika hifadhi zetu za taifa (Serengeti, Manyara, Ngorongoro, Mikumi, Ruaha) wasije kuadimika #2020.

Polisi wetu lazima waombe matumizi ya "VAR" kutumika.
 
hawa ndio wanaume wanaoweza kuwatisha polisi wa bongo.

sio mjinga mmoja anasema polisibnipigeni muone,nitawafunga mimi.bro utavunjwa mguu na uishie kufunga zipu ya suruali yako.
 
Back
Top Bottom