Iran yataka Trump ashtakiwe kwa mauaji ya Jenerali Soleimani

Sudan na China pia sio wanachama. Baraza la usalama la kimataifa hapo ndilo litakalopendekeza kesi kwa mwendesha mashtaka au mwendesha mashtaka mwenyewe aamue kuchunguza. Kuhusu kutokuwa na nchi ya kumkamata sio swala la kushangilia sababu matokeo yake ndio haya tunayaona Congo, Ethiopia, Iran n.k. Dunia inahitaji usawa kwenye hivi vyombo vya kimataifa. Hatua ya kwanza kufikia usawa hapa ni kuona hati ya kumkamata inatoka baadae sasa tuangalie nani atamfunga paka kengele
Kwenye Baraza la Usalama USA ni mwanachama wa kudumu na anaweza kublock maamuzi kwa kura yake ya veto. Kuna usawa flan unapaswa kuwepo kati ya mataifa, ila siamini kama mataifa yote yana hadhi sawa.Ni kama ilivyo kwa watu, ukiwa na fedha ni mtu ndio lakini unakuwa na hadhi tofauti, ndivyo ilivyo baina ya mataifa.
Wa kumfunga kengele US hayupo, wala haitatokea kwenye kizazi hiki. Badala ya kuanzia kwa taifa kubwa kama US wangekomaa hata na kataifa kama Israeli, ili wakifanikiwa wapate pa kuanzia. Kwa sasa US is an "indomitable " force.
 
Kwani siwalisha lipiza kisasi ama hakikutosha.

Huyo rais wa irani mwenyewe anajua anachoongea hakiwezekani sasa sijui anamdanganya nani.
 
Kwenye Baraza la Usalama USA ni mwanachama wa kudumu na anaweza kublock maamuzi kwa kura yake ya veto. Kuna usawa flan unapaswa kuwepo kati ya mataifa, ila siamini kama mataifa yote yana hadhi sawa.Ni kama ilivyo kwa watu, ukiwa na fedha ni mtu ndio lakini unakuwa na hadhi tofauti, ndivyo ilivyo baina ya mataifa.
Wa kumfunga kengele US hayupo, wala haitatokea kwenye kizazi hiki. Badala ya kuanzia kwa taifa kubwa kama US wangekomaa hata na kataifa kama Israeli, ili wakifanikiwa wapate pa kuanzia. Kwa sasa US is an "indomitable " force.
Kuandaliwa resolution tu ni hatua kubwa, inaonesha utayari wa UN kushughulikia wahalifu wote lakini pia italeta aibu kwa Marekani kuendelea kutumia utawala bora, demokrasia na haki za binadamu kama kigezo cha kuvamia au kuwekea vikwazo nchi nyingine. Pili, Iran ina nia ya kuishtaki Marekani kwahiyo bila shaka watakuwa wamewaza kuwa mwanachama wa ICC au kutambua mamlaka ya mahakama hiyo sababu kutegemea UNSC wanaweza kukwama kama ulivyosema hapo juu. Kuna hatua fulani iliyopigwa na hii mahakama, kwa sasa Mwendesha mashtaka ameruhusiwa kuchunguza wamarekani kuhusu vita vya Afagnistan.

Kuhusu Israel, ni ngumu kufanikiwa sababu sio Marekani wala Israel iliyokili kuua wanasayansi wa Iran. Umenipoteza hapo uliposema waishtaki Israel wapate pa kuanzia.

Muhimu ni kuona mashtaka yamefunguliwa baadae sasa ndio tuanze kujadili nani atamkamata Trump,
Al Bashir pamoja na kushtakiwa kwenye hii mahakama bado alikuwa anazurula nchi mbalimbali hadi alipotoka madarakani kwa maandamano ndio mipango ya kumfikisha ICC imeanza, kwahiyo hata kwa Marekani pamoja na kwamba inaonekana ni ngumu kukamatwa ila yanaweza kupatikana mazingira yatakayoruhusu kukamatwa kwake mf, shinikizo kutoka ndani ya Marekani.
 
Kuandaliwa resolution tu ni hatua kubwa, inaonesha utayari wa UN kushughulikia wahalifu wote lakini pia italeta aibu kwa Marekani kuendelea kutumia utawala bora, demokrasia na haki za binadamu kama kigezo cha kuvamia au kuwekea vikwazo nchi nyingine. Pili, Iran ina nia ya kuishtaki Marekani kwahiyo bila shaka watakuwa wamewaza kuwa mwanachama wa ICC au kutambua mamlaka ya mahakama hiyo sababu kutegemea UNSC wanaweza kukwama kama ulivyosema hapo juu. Kuna hatua fulani iliyopigwa na hii mahakama, kwa sasa Mwendesha mashtaka ameruhusiwa kuchunguza wamarekani kuhusu vita vya Afagnistan.

Kuhusu Israel, ni ngumu kufanikiwa sababu sio Marekani wala Israel iliyokili kuua wanasayansi wa Iran. Umenipoteza hapo uliposema waishtaki Israel wapate pa kuanzia.

Muhimu ni kuona mashtaka yamefunguliwa baadae sasa ndio tuanze kujadili nani atamkamata Trump,
Al Bashir pamoja na kushtakiwa kwenye hii mahakama bado alikuwa anazurula nchi mbalimbali hadi alipotoka madarakani kwa maandamano ndio mipango ya kumfikisha ICC imeanza, kwahiyo hata kwa Marekani pamoja na kwamba inaonekana ni ngumu kukamatwa ila yanaweza kupatikana mazingira yatakayoruhusu kukamatwa kwake mf, shinikizo kutoka ndani ya Marekani.
Sioni dalili ya Wamarekani kutaka Raisi wao yeyote kupelekwa mbele ya hii mahakama. Kuhusu UN sioni dalili ya Resolution kupitishwa kutokana na nguvu na influence ya US. Zaidi ni kuwa, nchi kama Iran ikifungua mashtaka haoribu sifa za US kwani Iran yenyewe ipo kundi la nchi korofi na zinazotuhumiwa kuunga mkono ugaidi, hivyo kufungua inaweza onekana kama wanatafuta sympathy ya ku cover tuhuma zao. Kwa Israeli hoja ilikuwa, kabla hujaweza ishtaki nchi kubwa kama US unaweza jaribu uthabiti wa hiyo strategy kwa nchi ndogo kama Israeli.
 
Sioni dalili ya Wamarekani kutaka Raisi wao yeyote kupelekwa mbele ya hii mahakama. Kuhusu UN sioni dalili ya Resolution kupitishwa kutokana na nguvu na influence ya US. Zaidi ni kuwa, nchi kama Iran ikifungua mashtaka haoribu sifa za US kwani Iran yenyewe ipo kundi la nchi korofi na zinazotuhumiwa kuunga mkono ugaidi, hivyo kufungua inaweza onekana kama wanatafuta sympathy ya ku cover tuhuma zao. Kwa Israeli hoja ilikuwa, kabla hujaweza ishtaki nchi kubwa kama US unaweza jaribu uthabiti wa hiyo strategy kwa nchi ndogo kama Israeli.
Sawa.
 
Tangu siku ile ya tukio la kurevenge wao wakaishia kutungua ndugu zao waliokuwa ktk ndege ya abiria Iran simuelewi analia au anacheka
Kuna mtu mmoja wa zamani za kale aliyewahi kusema: "Kabla haujalipa kisasi, hakikisha kwanza unachimba makaburi mawili". Before you embark on a journey of revenge, dig two graves!

Huo msemo unaakisi kwa kiasi kikubwa sana na hilo tukio la kutungua ndege.
 
Back
Top Bottom