Iran yasafirisha chakula kuenda Taifa lililotengwa la Qatar

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,261
3549541f0d6a6125c78bcc68c5eb8a43.jpg
Iran imetuma ndege tano zilizosheheni chakula kuenda nchini Qatar, ambayo inakumbwa na uhaba wa chakula baada ya kutengwa na nchi zingine za kiarabu.

Mataifa kadha yakiwemo hasimu mkubwa wa Iran, Saudi Arabia, wiki iliyopita yalikata uhusiano na Qatar baada ya kuishtumu kwa kufadhili ugaidi.

Mpaka na Saudi Arabia ambapo asilimia 40 ya chakula cha Qatar hupitia umefungwa.

Raia wa Qatar wameamrishwa kuondoka kutoka mataifa hayo lakini Qatar imesema kuwa haitafanya hivyo.

Haijulikani ikiwa chakula hicho ni msaada au ni cha kuuzwa.

Shirika la Ndege la Iran liliandika katika mtandao wa Twitter, wakati chakula hicho kikijazwa kwenye ndege ya nchini Iran.

Wadadisi wanasema kuwa uhusiano mzuri kati ya Qatar na Iran ni moja ya sababu zilizochangia mzozo huo.

Qatar kwa upande wake inasema haijajibu baada ya Saudi Arabia, Bahrain na UAE wiki iliyopita, kuamrisha raia wote wa Qatar waondoke ndani ya siku 14.

Karibu watu 11,000 kutoka nchi tatu wanaaminika kuishi nchini Qatar.

Chanzo: BBC
 
Aliye kwambia iran hawapatani na Mmarekani nani
Uhusiano wa Kidiplomasia kati ya nchi hizo siyo mzuri toka mapinduzi yaliyofanywa na Ayattollah Khomeini kwa kumuondoa Shah aliyekuwa kibaraka wa USA. Hata uhusiano kati ya Saudia Arabia na Irani siyo mzuri kihivyo tangu 2016. Wewe fuatilia tu au uliza swali lakini usibishe bila kuwa na chochote cha kusindikizia ubishi wako.
 
huo ndio urafiki mzuri.
Na wewe unaamini ni urafiki? Iran hapo kapata kanafasi kuji show off. Yuko kistratejia zaidi; they are trying to send a message to somewhere in an attempt how influecial and powerful they are. Ni nyota ya jaha kwao japo akiachiwa zigo ndani ya miezi 6 analitema hana huo ubavu.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom