kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,839
- 17,437
Iran yazindua droni yake ya Ghaza na mafanikio yake mapya ya kijeshi.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imezindua mafanikio matatu makubwa ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ikiwemo droni (ndege isiyo na rubani) ya Ghaza.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRIB, wakati huu wa kukaribia Khordad 3 kwa kalenda ya Kiirani ya Hijria Shamsia ambayo ni "Siku ya Muqawama, Kujitolea na Ushindi" Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH limezindua mafanikio matatu muhimu na ya kiistratijia ya kiulinzi na kijeshi, katika sherehe zilizohudhuriwa na Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la SEPAH na Brigedia Jenerali Amir Ali Hajizadeh, Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran.
Miongoni mwa sifa maalumu za ndege isiyo na rubani ya Ghaza ni uwezo wake mkubwa wa kiulinzi na kijeshi, utafiti na ugunduzi na kuruka angani kwa muda wa masaa 35.
Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la SEPAH katika sherehe za uzinduzi wa mafanikio mapya ya kiulinzi ya Iran
Droni hiyo ya Ghaza ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ina uwezo pia wa kubeba mabomu 13 na kuruka umbali wa kilomita 2000. Ina uwezo wa kubeba kilo 500 za zana za kijeshi na pia kukusanya taarifa za kijasusi na za kiishara. Kuingia droni hiyo ya kisasa katika orodha ya ndege zisizo na rubani za SEPAH kumezidisha sana uwezo wa ulinzi wa anga wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mbali na matumizi ya kijeshi, droni ya Ghaza inaweza kutumika pia katika tafiti mbalimbali zikiwemo za kwenye misitu, operesheni za misaada, uokoaji na ufikishaji misaada nyakati za ajali na majanga ya kimaumbile kama vile mafuriko, mitetemeko ya ardhi n.k.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imezindua mafanikio matatu makubwa ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ikiwemo droni (ndege isiyo na rubani) ya Ghaza.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRIB, wakati huu wa kukaribia Khordad 3 kwa kalenda ya Kiirani ya Hijria Shamsia ambayo ni "Siku ya Muqawama, Kujitolea na Ushindi" Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH limezindua mafanikio matatu muhimu na ya kiistratijia ya kiulinzi na kijeshi, katika sherehe zilizohudhuriwa na Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la SEPAH na Brigedia Jenerali Amir Ali Hajizadeh, Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran.
Miongoni mwa sifa maalumu za ndege isiyo na rubani ya Ghaza ni uwezo wake mkubwa wa kiulinzi na kijeshi, utafiti na ugunduzi na kuruka angani kwa muda wa masaa 35.
Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la SEPAH katika sherehe za uzinduzi wa mafanikio mapya ya kiulinzi ya Iran
Droni hiyo ya Ghaza ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ina uwezo pia wa kubeba mabomu 13 na kuruka umbali wa kilomita 2000. Ina uwezo wa kubeba kilo 500 za zana za kijeshi na pia kukusanya taarifa za kijasusi na za kiishara. Kuingia droni hiyo ya kisasa katika orodha ya ndege zisizo na rubani za SEPAH kumezidisha sana uwezo wa ulinzi wa anga wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mbali na matumizi ya kijeshi, droni ya Ghaza inaweza kutumika pia katika tafiti mbalimbali zikiwemo za kwenye misitu, operesheni za misaada, uokoaji na ufikishaji misaada nyakati za ajali na majanga ya kimaumbile kama vile mafuriko, mitetemeko ya ardhi n.k.