kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,987
- 17,861
Jenerali Qassem Soleimani: Iran iko tayari kuvisaidia vikosi vya Muqawama vya Palestina kwa kila hali
Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kutoa msukumo na kuvisaidia kwa kila hali vikosi vya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina.
Meja Jenerali Qassem Soleimani ameyasema hayo katika mazungumzo aliyofanya kwa njia ya simu na makamanda wa brigedi za Izzuddin al- Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS na wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina pia.
Katika mazungumzo hayo Jenerali Qassem Soleimani amesisitiza pia kwamba makundi mengine ya Muqawama katika eneo la Mashariki ya Kati yako tayari kuuhami msikiti mtukufu wa Al Aqsa.
Jumatano ya tarehe 6 ya mwezi huu wa Desemba, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza uamuzi ambao kwa mujibu wa jumuiya za kimataifa na nchi mbalimbali duniani unagongana na kukinzana na maazimio ya kimataifa. Trump aliitangaza Baitul Muqaddas kuwa mji mkuu wa Israel na kutoa amri ya kufanywa maandalizi ya kuuhamishia katika mji huo ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilikuwa miongoni mwa nchi za mwanzo ambazo zililaani hatua hiyo ya Trump. Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilitoa taarifa siku hiyo hiyo ya Jumatano usiku na kusisitiza kwamba hatua ya Rais wa Marekani ya kuitambua Quds kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni ni ukiukaji wa wazi wa maazimio ya kimataifa.
Nchi nyingi duniani pamoja na jumuiya za kimataifa, nazo pia zimelaani hatua hiyo ya Trump...
Chanzo; Radio tehran
Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kutoa msukumo na kuvisaidia kwa kila hali vikosi vya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina.
Meja Jenerali Qassem Soleimani ameyasema hayo katika mazungumzo aliyofanya kwa njia ya simu na makamanda wa brigedi za Izzuddin al- Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS na wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina pia.
Katika mazungumzo hayo Jenerali Qassem Soleimani amesisitiza pia kwamba makundi mengine ya Muqawama katika eneo la Mashariki ya Kati yako tayari kuuhami msikiti mtukufu wa Al Aqsa.
Jumatano ya tarehe 6 ya mwezi huu wa Desemba, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza uamuzi ambao kwa mujibu wa jumuiya za kimataifa na nchi mbalimbali duniani unagongana na kukinzana na maazimio ya kimataifa. Trump aliitangaza Baitul Muqaddas kuwa mji mkuu wa Israel na kutoa amri ya kufanywa maandalizi ya kuuhamishia katika mji huo ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilikuwa miongoni mwa nchi za mwanzo ambazo zililaani hatua hiyo ya Trump. Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilitoa taarifa siku hiyo hiyo ya Jumatano usiku na kusisitiza kwamba hatua ya Rais wa Marekani ya kuitambua Quds kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni ni ukiukaji wa wazi wa maazimio ya kimataifa.
Nchi nyingi duniani pamoja na jumuiya za kimataifa, nazo pia zimelaani hatua hiyo ya Trump...
Chanzo; Radio tehran