Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,486
- 51,063
- Thread starter
- #161
Siku nyingine tutofautishe Benki kama Entity inayojitegemea, na Nchi ambayo benki hiyo imesajiliwa.Kujipeleka ama kutokujipeleka kukopa kunategemeana na sera za mkopaji na mkopeshaji. Mkopeshaji mwingine anaweza kukufuata yeye mwenyewe kukuomba umkope ama kukushawishi huku akiwa na nia ovu dhidi ya masilahi yako, ndicho kile nilichokisema awali, debt-trap diplomacy. Hakuna urafiki wowote hapo!
Hoja yangu ya msingi tangu awali ipo katika jinsi ambavyo hiyo mikopo inatolewa ukilinganisha na kiasi chote cha deni la nje la Tanzania. Kwa sababu, si kila serikali hutoa mikopo directly kwa serikali za nchi nyingine. Mara nyingi, benki za nchi husika na taasisi au mashirika ya kifedha hutumika badala yake!
Hivyo, takwimu za government-to-government loans haziakisi uhalisia wa deni lote ambalo Tanzania inadaiwa, wala si kipimo sahihi cha kuthibitisha kuwa China na Marekani haziongozi katika kuikopesha Tanzania.
Benki ni mitaji ya watu wengi kutoka katika mataifa mengi, Pesa kutoka katika mashirika na makampuni mengi ya duniani kote, kutoka firms nyingi.
Serikali huwa zina shares tu katika mabenki hayo lakini haimaanishi kuwa pesa za mabenki hayo zote ni za serikali fulani.
Kwa hiyo ukikopshwa hela na Standard Chattered bank ya Uingereza haimaanishi kuwa Uingwreza imekukopesha, bali shareholders wote wa benki hiyo including watu ambao siyo waingereza wanekukopesha, na Wanasubiri faida yaokutokana na riba waliyokutwanga!
Nchi fulani inaweza kukubali kuidhamini nchi nyibgine tu pale itakapochukua mkopo katika benki fulani lakini haimaanishi kuwa nchi hiyo imeikopesha nchi nyingine.
A BANK IS A SEPARATE, FREE BUSINESS ENTITY