Iran kujenga Hospitali ya kisasa Zanzibar

mdau wetu

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
548
58
JUHUDI za serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuinua huduma za afya kwa wananchi, ikiwemo kuwapunguzia gharama za kwenda kutibiwa nje ya nchi zimeanza kuonesha dalili za mafanikio baada ya serikali kutiliana saini makubaliano ya ujenzi wa hospitali mbili za kisasa zitakazojengwa katika mji wa Wete Pemba na mkoa wa Mjini Mgharibi Unguja.
Hospitali hizo zitajengwa na Jumuiya ya Mwezi Mwekundu ya Iran (Iran Red Crescent Society) mara baada jumuiya hiyo kukamilisha utafiti wa mahitaji ya afya ya wananchi wa Zanzibar unaotarajiwa kukamilika mwezi Disemba mwaka huu.
Hatua hiyo inafikiwa baada ya serikali ya Zanzibar kutiliana saini makubaliano ya mradi huo huko Dubai, Falme za Kiarabu wiki iliyopita, ambapo Waziri Afya na Ustawi wa Jamii, Juma Duni Haji alitia saini hiyo kwa niaba ya Zanzibar, huku Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad akishuhudia tukio la utiaji saini makubaliano hayo.
Waziri wa Afya, Juma Duni amesema chini ya makubaliano hayo, jumuiya hiyo itajenga hospitali za kisasa zitakazotoa mahitaji yote, ambapo Zanzibar jukumu lake itakuwa ni kuipatia sehemu zitakazojengwa hospitali hizo katika mkoa wa Mjini Magharibi na huko Wete kwa upande wa Pemba.
“Serikali ya Zanzibar haitatoa fedha yoyote katika ujenzi huo, isipokuwa maeneo yatakayojengwa hospitali hizo, baada ya hatua ile ya utiaji saini watafanya utafiti wa mahitaji halisi ya kiafya ya Wazanzibari ambao utakuwa umekamilika ifikapo mwezi Disemba mwaka huu na ujenzi utaanza”, alisema Waziri Duni.
Alieleza kuwa utafiti huo pia utajumuisha mahitaji ya uajiri kwa madakatari watakaohitajika katika hospitali hizo, pamoja na taratibu za kuwapatia vibali vya kufanyia kazi kwa madaktari wageni watakaohitajika kuja kuhudumia wagonjwa.
Duni alisema jumuiya hiyo ya Mwezi Mwekundu ya Iran ni ya hisani (Charitable Society) ambayo tayari imejenga miradi mikubwa ya hospitali katika miji mbali mbali, ikiwemo Dubai na huduma inazozitoa zimesifiwa juu ya ubora wake na hata unafuu katika upatikanaji wake kwa wananchi wenye vipato vya chini.
Alieleza kuwa walipokuwa Dubai walitembelea moja ya hospitali zinazoendeshwa na jumuiya hiyo, ambayo inatoa huduma zote muhimu katika kiwango cha hali ya juu na wagonjwa wengi wamekuwa wakienda kupata huduma kwa unafuu.
Waziri Duni alisema hospitali hizo zitakapoanza kutoa huduma Zanzibar itakuwa ni hatua kubwa na ya mafaniko kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba kupata matibabu, kwa sababu hadi sasa huduma zinazopatikana nchini hazijatosheleza na kuna wananchi wengi wanaopewa rufaa kwenda kutubiwa nje ya nchi, jambo ambalo sio wananchi wote wanaoweza kumudu gharama zake.
Alisema faraja kubwa zaidi itakuwa kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, ambao hata kesi ndogo za matibabu mara kadhaa hutakiwa kuja Unguja katika hospitali ya Mnazimmoja, jambo ambalo pia alisema ni mzigo kwao kutokana na hali za kimaisha za wananchi wengi bado ni duni.
“Hospitli itakayojengwa Wete kule Pemba ina umuhimu mkubwa zaidi ikizingatiwa kwamba, hata kesi za kawaida wao hutakiwa kuja Unguja na kutumia gharama nyingi za usafiri na matibabu yenyewe”, alisema.
Ijumaa iliyopita, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema serikali inachakua juhudi kubwa kuhakikisha huduma za kisasa na za kiwango cha juu za matibabu zinapatikana Zanzibar kwa nia ya kuwaondolea usumbufu na gharama kubwa wanazopata wananchi pamoja na serikali, pale wanapotakiwa kwenda kufanyiwa matibabu zaidi nchi za nje.
Akizungumza na madaktari kutoka hospitali ya MIOT ya India walipomtembelea ofisini kwake, alisema bado Zanzibar inahitaji wataalamu waliobobea zaidi katika sekta mbali mbali, ikiwemo ya afya kufanikisha azma ya kuwapatia wananchi wa Unguja na Pemba huduma za matibabu za uhakika na kwa urahisi.
Maalim Seif alisema hadi sasa kesi za wagonjwa wanaotakiwa kupatiwa matibabu ni nyingi, ikiwemo watoto wadogo wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo, ambao hutakiwa kwenda kufanyiwa upasuaji nchini India wakifuatana na jamaa pamoja na mhuduma wa afya, ambapo serikali na wananchi watapata nafuu kubwa iwapo huduma kama hizo zitakapokuwa zinapatikana hapa hapa Zanzibar.
Mbali na nchi za nje baadhi ya wagonjwa hapa Zanzibar hutakiwa kwenda kupata matibabu zaidi katika hospitali za Tanzania Bara, pale huduma husika zinapokosekana katika hospitali za Zanzibar.
 
nijambo zuri ndio maana ya umoja wa kitaifa watu wanashirikiana kwa mambo yote yenye tija kwa taifa.
 
JUHUDI za serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuinua huduma za afya kwa wananchi, ikiwemo kuwapunguzia gharama za kwenda kutibiwa nje ya nchi zimeanza kuonesha dalili za mafanikio baada ya serikali kutiliana saini makubaliano ya ujenzi wa hospitali mbili za kisasa zitakazojengwa katika mji wa Wete Pemba na mkoa wa Mjini Mgharibi Unguja.
Hospitali hizo zitajengwa na Jumuiya ya Mwezi Mwekundu ya Iran (Iran Red Crescent Society) mara baada jumuiya hiyo kukamilisha utafiti wa mahitaji ya afya ya wananchi wa Zanzibar unaotarajiwa kukamilika mwezi Disemba mwaka huu.
Hatua hiyo inafikiwa baada ya serikali ya Zanzibar kutiliana saini makubaliano ya mradi huo huko Dubai, Falme za Kiarabu wiki iliyopita, ambapo Waziri Afya na Ustawi wa Jamii, Juma Duni Haji alitia saini hiyo kwa niaba ya Zanzibar, huku Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad akishuhudia tukio la utiaji saini makubaliano hayo.
Waziri wa Afya, Juma Duni amesema chini ya makubaliano hayo, jumuiya hiyo itajenga hospitali za kisasa zitakazotoa mahitaji yote, ambapo Zanzibar jukumu lake itakuwa ni kuipatia sehemu zitakazojengwa hospitali hizo katika mkoa wa Mjini Magharibi na huko Wete kwa upande wa Pemba.
"Serikali ya Zanzibar haitatoa fedha yoyote katika ujenzi huo, isipokuwa maeneo yatakayojengwa hospitali hizo, baada ya hatua ile ya utiaji saini watafanya utafiti wa mahitaji halisi ya kiafya ya Wazanzibari ambao utakuwa umekamilika ifikapo mwezi Disemba mwaka huu na ujenzi utaanza", alisema Waziri Duni.
Alieleza kuwa utafiti huo pia utajumuisha mahitaji ya uajiri kwa madakatari watakaohitajika katika hospitali hizo, pamoja na taratibu za kuwapatia vibali vya kufanyia kazi kwa madaktari wageni watakaohitajika kuja kuhudumia wagonjwa.
Duni alisema jumuiya hiyo ya Mwezi Mwekundu ya Iran ni ya hisani (Charitable Society) ambayo tayari imejenga miradi mikubwa ya hospitali katika miji mbali mbali, ikiwemo Dubai na huduma inazozitoa zimesifiwa juu ya ubora wake na hata unafuu katika upatikanaji wake kwa wananchi wenye vipato vya chini.
Alieleza kuwa walipokuwa Dubai walitembelea moja ya hospitali zinazoendeshwa na jumuiya hiyo, ambayo inatoa huduma zote muhimu katika kiwango cha hali ya juu na wagonjwa wengi wamekuwa wakienda kupata huduma kwa unafuu.
Waziri Duni alisema hospitali hizo zitakapoanza kutoa huduma Zanzibar itakuwa ni hatua kubwa na ya mafaniko kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba kupata matibabu, kwa sababu hadi sasa huduma zinazopatikana nchini hazijatosheleza na kuna wananchi wengi wanaopewa rufaa kwenda kutubiwa nje ya nchi, jambo ambalo sio wananchi wote wanaoweza kumudu gharama zake.
Alisema faraja kubwa zaidi itakuwa kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, ambao hata kesi ndogo za matibabu mara kadhaa hutakiwa kuja Unguja katika hospitali ya Mnazimmoja, jambo ambalo pia alisema ni mzigo kwao kutokana na hali za kimaisha za wananchi wengi bado ni duni.
"Hospitli itakayojengwa Wete kule Pemba ina umuhimu mkubwa zaidi ikizingatiwa kwamba, hata kesi za kawaida wao hutakiwa kuja Unguja na kutumia gharama nyingi za usafiri na matibabu yenyewe", alisema.
Ijumaa iliyopita, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema serikali inachakua juhudi kubwa kuhakikisha huduma za kisasa na za kiwango cha juu za matibabu zinapatikana Zanzibar kwa nia ya kuwaondolea usumbufu na gharama kubwa wanazopata wananchi pamoja na serikali, pale wanapotakiwa kwenda kufanyiwa matibabu zaidi nchi za nje.
Akizungumza na madaktari kutoka hospitali ya MIOT ya India walipomtembelea ofisini kwake, alisema bado Zanzibar inahitaji wataalamu waliobobea zaidi katika sekta mbali mbali, ikiwemo ya afya kufanikisha azma ya kuwapatia wananchi wa Unguja na Pemba huduma za matibabu za uhakika na kwa urahisi.
Maalim Seif alisema hadi sasa kesi za wagonjwa wanaotakiwa kupatiwa matibabu ni nyingi, ikiwemo watoto wadogo wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo, ambao hutakiwa kwenda kufanyiwa upasuaji nchini India wakifuatana na jamaa pamoja na mhuduma wa afya, ambapo serikali na wananchi watapata nafuu kubwa iwapo huduma kama hizo zitakapokuwa zinapatikana hapa hapa Zanzibar.
Mbali na nchi za nje baadhi ya wagonjwa hapa Zanzibar hutakiwa kwenda kupata matibabu zaidi katika hospitali za Tanzania Bara, pale huduma husika zinapokosekana katika hospitali za Zanzibar.

Kwa nini viongozi wetu wamekuwa addicted na misaada namna hiyo? Yaani kwao serikali kutokuchangia chochote ndiyo wanaona sifa! Kweli tua viongozi wapumbavu
 
Kwa nini viongozi wetu wamekuwa addicted na misaada namna hiyo? Yaani kwao serikali kutokuchangia chochote ndiyo wanaona sifa! Kweli tua viongozi wapumbavu
Ukiona hivyo kuna some kind of strings attached we subiri tuu. Nothing is free in this world
 
Back
Top Bottom