Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 11,634
- 26,370
Wakuu,
Baada ya kuwepo kwa ugonjwa wa covid-19 maarufu kama Corona nchini Tanzania,serikali kupitia Waziri mkuu ilipiga marufuku mikusanyiko mbalimbali ikiwemo,semina,mikutano,vikao,warsha nk,na ikaenda mbali zaidi kwa kufunga shule kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu.
Lakini katika hali ya Kushangaza serikali imeendelea kuacha Minada ifanyike kama kawaida.
Kuna mnada umefanyika leo tarehe 20/3/2020 katika kijiji cha Malendi tarafa ya Shelui wilayani Iramba na chanzo cha taarifa ni wakazi wa eneo husika.
Ni Minada hii hii ambayo hukusanya watu wengi kutoka maeneo tofauti tofauti ambapo watu hubanana,bidhaa hushikwa na watu wengi kwa wakati mmoja,ulaji na unywaji wa vinywaji baridi na vileo.
Je kuachwa Minada iendelee kuna nia njema na afya za watanzania? Au mapato ni muhimu kuliko afya za watu?
Sent using Jamii Forums mobile app
Baada ya kuwepo kwa ugonjwa wa covid-19 maarufu kama Corona nchini Tanzania,serikali kupitia Waziri mkuu ilipiga marufuku mikusanyiko mbalimbali ikiwemo,semina,mikutano,vikao,warsha nk,na ikaenda mbali zaidi kwa kufunga shule kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu.
Lakini katika hali ya Kushangaza serikali imeendelea kuacha Minada ifanyike kama kawaida.
Kuna mnada umefanyika leo tarehe 20/3/2020 katika kijiji cha Malendi tarafa ya Shelui wilayani Iramba na chanzo cha taarifa ni wakazi wa eneo husika.
Ni Minada hii hii ambayo hukusanya watu wengi kutoka maeneo tofauti tofauti ambapo watu hubanana,bidhaa hushikwa na watu wengi kwa wakati mmoja,ulaji na unywaji wa vinywaji baridi na vileo.
Je kuachwa Minada iendelee kuna nia njema na afya za watanzania? Au mapato ni muhimu kuliko afya za watu?
Sent using Jamii Forums mobile app