IPP media imedanganya kuhusu JWTZ?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,023
18,563
Wana JF, leo nimeona picha kwenye IPPMedia iliyoambatana na kichwa cha habari kuwa mainjinia wa JWTZ watasaidia katika ujenzi wa SGR.

Lakini jambo lililonishangaza ni hiyo picha iliyowekwa ikionyesha askari wakiwa na silaha wakisemwa kuwa ni askari wa JWTZ (au TPDF). Hapo nimetilia shaka sana, kwa kuwa JWTZ huwa hawavai nusu kombati (camouflage) na pia silaha walizoshika ni assault rifles M16 za Marekani ambazo nadhani Polisi wa Kenya walipewa na USA katika kupambana na magaidi badala ya kutumia G-3 na SMG au AK 47, ambazo kidogo ni hafifu.

Je, inawezekana kwamba IPPMedia wametupiga changa la macho kwa kuweka picha ya askari Polisi wa Kenya na kuwaita JWTZ? Nadhani hii ni picha ya riot squad ya Polisi wa Kenya ambayp IPPMedia wameamua kuwaita TPDF. Nani amewahi kuona JWTZ wakiwa wamevalia kama picha inavyoonyesha? Huu utakuwa uzembe wa hali ya juu kwa mhariri wao.

1539156158404.png

TPDF all out to offer engineers for SGR construction project
 
Ndo madhara ya kuajiri waandishi kanjanja.

Tatizo elimu mtu hana competency mnampa kazi.

Hao ni polisi wa Kenya tena before.
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?
 
Ndo madhara ya kuajiri waandishi kanjanja.

Tatizo elimu mtu hana competency mnampa kazi.

Hao ni polisi wa Kenya tena before.
ITV hakuna ukanjanja mkuu kasome journalism alafu nenda katafute kazi pale kama utapata ni lazima upitie radio ndogo au wakupike wao kama RICHARD STEVEN
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?

Angalia kwa chini ya picha upande wa kushoto wameandika kwamba picha ni ya TPDF wakati siyo, je una hakika gani kama taarifa siyo ya Kenya pia?
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?
Kwa kuzingatia mfano wako,ni kuwa alichokifanya huyo habari ya Magufuli kawekwa mtu mwingine. Habari ya Tanzania unawekaje jeshi la Kenya,wapi na wapi.
 
Kwa kuzingatia mfano wako,ni kuwa alichokifanya huyo habari ya Magufuli kawekwa mtu mwingine. Habari ya Tanzania unawekaje jeshi la Kenya,wapi na wapi.
Ni E.A na wao wanaujenzi kama wetu unaendelea 😂😂😂
 
ITV hakuna ukanjanja mkuu kasome journalism alafu nenda katafute kazi pale kama utapata ni lazima upitie radio ndogo au wakupike wao kama RICHARD STEVEN
Kama hamna ukanjanja hiyo picha apo vp sio ukanjanja huo?

Huyo richard steven asiyejua hata matumizi ya R na L?? Hata jina lake lenyewe anaita LICHADI STIVIN

Putz!
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?
Naelewa sana suala la kutumia kitu kinaitwa file photo. Lakini hapa huwezi kusema ni suala la file photo. Zaidi ya hilo, caption kwenye hiyo picha inasema wazi "Tanzania Peoples's Defence Force". Au hujui maana yake?
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?
ITV hakuna ukanjanja mkuu kasome journalism alafu nenda katafute kazi pale kama utapata ni lazima upitie radio ndogo au wakupike wao kama RICHARD STEVEN

Buda Ina maana hujaona tatizo kwenye hiyo habari?

Mimi sio mwandishi ila kuweka picha ambayo haiendani na habari huo ni ukanjanja.

Walitakiwa waweke pic ya Askali wetu.
 
Kumbe tatizo ni picha tu sicho kilichoandikwa? Hujawahi kuona heading za magazeti magufuli atua kwa kishindo mwanza alafu picha inayowekwa ni ya akiwa chato au ikulu?

Kwa kuzingatia mfano wako,ni kuwa alichokifanya huyo habari ya Magufuli kawekwa mtu mwingine. Habari ya Tanzania unawekaje jeshi la Kenya,wapi na wapi.
Hahaha! Kweli Mkuu, ni sawa na uandike kichwa cha habari "Magufuli asema amechoka kutuma rambirambi" halafu kwenye hiyo habari uweke picha ya Raisi Uhuru Kenyatta, halafu uandike chini yake Raisi wa Tanzania John Magufuli. Yaani huyu bwashee anaona eti sio ukanjanja ni sawa.
 
Shida ni pale habari wanayo ila picha za habar hawana wanadownload.
Hahaha! Kweli Mkuu, ni sawa na uandike kichwa cha habari "Magufuli asema amechoka kutuma rambirambi" halafu kwenye hiyo habari uweke picha ya Raisi Uhuru Kenyatta, halafu uandike chini yake Raisi wa Tanzania John Magufuli. Yaani huyu bwashee anaona eti sio ukanjanja ni sawa.
 
Buda Ina maana hujaona tatizo kwenye hiyo habari?

Mimi sio mwandishi ila kuweka picha ambayo haiendani na habari huo ni ukanjanja.

Walitakiwa waweke pic ya Askali wetu.
Sawa tutaweka ya mgambo au sungusungu 😂😂😂✏
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom