Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,220
- 9,647
Ndugu zangu Watanzania,
Siku yaja na miaka yaja ambapo wapinzani watakubali kuwa CCM ndio chama pekee kinachopaswa kuungwa mkono na kupewa ushirikiano katika kuliongoza taifa letu, watakubali kuwa Sera ajenda Dira na muelekeo wa CCm ndio sahihi na unatosha kutuvusha Watanzania kuelekea nchi ya Kanaan.
Watakubali kuwa CCM ndio moyo wa watanzania linapokuja suala la Imani juu ya chama, watakubali kuwa, vyama vyao ni SHIKIZI tu kwa ajili ya kujipatia ruzuku, watakubali tu wapo upinzani kutolea mawazo yao lakini linapokuja suala la kuikabidhi nchi mikononi mwa chama basi CCM ndio chama pekee kinachopaswa kupewa jukumu Hilo.
Hii ni kutokana na historia yake CCM ambayo huwezi ukaitenganisha CCM na historia ya taifa hili. Huwezi ukaizungumzia Tanzania bila kuiambatanisha na CCM, Tanzania ni CCM, ni sawa na mtu na ngozi, huwezi ukamchuna au kumtenganisha mtu na ngozi akabaki hai, CCM ndio Tanzania na Tanzania ndio CCM.
CCM imejizatiti kisawasawa linapokuja jambo lenye maslahi kwa taifa, hakuna kuyumba katika maslahi ya taifa, CCM inaweza ikabadilisha mbinu, mikakati, sera, ajenda, uongozi wa juu na ilani kuendana na wakati lakini maslahi ya taifa ni ya kudumu na yanayolindwa kwa jasho na damu kuhakikisha kuwa taifa letu linabaki lenye amani na tulivu.
Kazi hii nyeti huwezi hata kwa bahati mbaya kuwapa upinzani huu usio na muelekeo wala ajenda wala uchungu na nchi hii, ndio maana ni kawaida kusikia kiongozi wa upinzani akisimama jukwaani na kusema nchi hii haitatawalika au nchi itawaka moto.
Hii ni kwa kuwa hawana uchungu na nchi hii zaidi ya kujali matumbo yao, hawaoni hasara kuvuruga amani yetu, ndio maana hata watoto wao wana uraia wa nchi za kigeni, ndio maana hata uzalendo wao ni hafifu sana juu ya taifa letu. Ndio maana huwa wanazungumza chochote kinachokuja katika midomo yao, ndio maana Watanzania kuamua kuwapuuza na kuwadharau wao na vyama vyao vilivyokosa dira na muelekeo.
Kauli za aina hiyo huwezi ukazisikia hata kwa bahati mbaya zikitoka kwa kiongozi yeyote na wa ngazi yoyote wa CCm, kwa kuwa wanajuwa na Wana uchungu na taifa letu na wanajuwa dhamana waliyo nayo katika kulipigania taifa letu ikibidi hata kuhatarisha maisha kwa ajili ya kulilinda Taifa.
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627
Siku yaja na miaka yaja ambapo wapinzani watakubali kuwa CCM ndio chama pekee kinachopaswa kuungwa mkono na kupewa ushirikiano katika kuliongoza taifa letu, watakubali kuwa Sera ajenda Dira na muelekeo wa CCm ndio sahihi na unatosha kutuvusha Watanzania kuelekea nchi ya Kanaan.
Watakubali kuwa CCM ndio moyo wa watanzania linapokuja suala la Imani juu ya chama, watakubali kuwa, vyama vyao ni SHIKIZI tu kwa ajili ya kujipatia ruzuku, watakubali tu wapo upinzani kutolea mawazo yao lakini linapokuja suala la kuikabidhi nchi mikononi mwa chama basi CCM ndio chama pekee kinachopaswa kupewa jukumu Hilo.
Hii ni kutokana na historia yake CCM ambayo huwezi ukaitenganisha CCM na historia ya taifa hili. Huwezi ukaizungumzia Tanzania bila kuiambatanisha na CCM, Tanzania ni CCM, ni sawa na mtu na ngozi, huwezi ukamchuna au kumtenganisha mtu na ngozi akabaki hai, CCM ndio Tanzania na Tanzania ndio CCM.
CCM imejizatiti kisawasawa linapokuja jambo lenye maslahi kwa taifa, hakuna kuyumba katika maslahi ya taifa, CCM inaweza ikabadilisha mbinu, mikakati, sera, ajenda, uongozi wa juu na ilani kuendana na wakati lakini maslahi ya taifa ni ya kudumu na yanayolindwa kwa jasho na damu kuhakikisha kuwa taifa letu linabaki lenye amani na tulivu.
Kazi hii nyeti huwezi hata kwa bahati mbaya kuwapa upinzani huu usio na muelekeo wala ajenda wala uchungu na nchi hii, ndio maana ni kawaida kusikia kiongozi wa upinzani akisimama jukwaani na kusema nchi hii haitatawalika au nchi itawaka moto.
Hii ni kwa kuwa hawana uchungu na nchi hii zaidi ya kujali matumbo yao, hawaoni hasara kuvuruga amani yetu, ndio maana hata watoto wao wana uraia wa nchi za kigeni, ndio maana hata uzalendo wao ni hafifu sana juu ya taifa letu. Ndio maana huwa wanazungumza chochote kinachokuja katika midomo yao, ndio maana Watanzania kuamua kuwapuuza na kuwadharau wao na vyama vyao vilivyokosa dira na muelekeo.
Kauli za aina hiyo huwezi ukazisikia hata kwa bahati mbaya zikitoka kwa kiongozi yeyote na wa ngazi yoyote wa CCm, kwa kuwa wanajuwa na Wana uchungu na taifa letu na wanajuwa dhamana waliyo nayo katika kulipigania taifa letu ikibidi hata kuhatarisha maisha kwa ajili ya kulilinda Taifa.
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627