MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Kwa hakika yale maneno yasemwayo sana mitaani kua "Upinzani ndio bunge, na bunge ni upinzani" hii ina maana ya kwamba hakuna bunge bila upinzani. Mwenendo wa bunge la sasa kimahudhurio si mzuri!
Ni wazi kabisa baada ya wabunge wa upinzani kuamua kutoka na kutohudhuria vikao vyote vya bunge endapo anayeongiza ni Naibu spika Tulia Acksoni kwa sababu ya kutokutumia mizania sawa kutoka pande zote wakati wa mijadala, bunge zima limebaki na wabunge wa chama kimoja cha CCM! sasa nao wengi wanaonekana kutohudhuria vikao kwa sababu zao binafsi na wengine kwa majukumu ya kazi za kiserikali hasa mawaziri.
Japo kwenye suala la posho linawahusu wale wa upinzani lakini hawa wa CCM hata kama hawapo lakini posho wanalipwa tu. Maana "mkuki mtamu kwa nguruwe ila kwa binadamu mchungu"
Imethibitika kua sasa mahudhurio ya wabunge wa CCM ni hafifu sana, wengi hawapo bungeni na imeonesha wazi wazi kabisa pasina shaka kua wabunge wa upinzani pekee ndio waliokua wakihudhuria vikao vyote vya bunge pamoja na uchache wao ili kuhakikisha kua wanaisimamia serikali ipasavyo. Hali ya kutokuwepo bungeni kwa wabunge wa upinzani imeoekana ni pengo na pigo kubwa sana kwa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania ambapo kwa sasa taswira yake halisi kwa sasa inafifia. Sijui ni kwanini huyu Naibu Spika hashtuki na halionei taifa uchungu.
Kuna uwezekano kabisa siku moja Naibu Spika akaahirisha kikao kwa sababu ya uchache wa wabunge waliopo ndani ya ukumbi, kuna uwezekano akatoa sababu nyingine kabisa ya kuahirisha kikao kwa kuogopa kuwaumbua wabunge wa CCM lakini tatizo likawa wazi kabisa.
Bunge bila ya LISSU,Zitto, Mnyika,Mdee,Maiko,Bulaya,Heche, Kubenea,Pareso, Gekulu sio bunge kabisa hata dunia nzima inatambua.
Ni wazi kabisa baada ya wabunge wa upinzani kuamua kutoka na kutohudhuria vikao vyote vya bunge endapo anayeongiza ni Naibu spika Tulia Acksoni kwa sababu ya kutokutumia mizania sawa kutoka pande zote wakati wa mijadala, bunge zima limebaki na wabunge wa chama kimoja cha CCM! sasa nao wengi wanaonekana kutohudhuria vikao kwa sababu zao binafsi na wengine kwa majukumu ya kazi za kiserikali hasa mawaziri.
Japo kwenye suala la posho linawahusu wale wa upinzani lakini hawa wa CCM hata kama hawapo lakini posho wanalipwa tu. Maana "mkuki mtamu kwa nguruwe ila kwa binadamu mchungu"
Imethibitika kua sasa mahudhurio ya wabunge wa CCM ni hafifu sana, wengi hawapo bungeni na imeonesha wazi wazi kabisa pasina shaka kua wabunge wa upinzani pekee ndio waliokua wakihudhuria vikao vyote vya bunge pamoja na uchache wao ili kuhakikisha kua wanaisimamia serikali ipasavyo. Hali ya kutokuwepo bungeni kwa wabunge wa upinzani imeoekana ni pengo na pigo kubwa sana kwa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania ambapo kwa sasa taswira yake halisi kwa sasa inafifia. Sijui ni kwanini huyu Naibu Spika hashtuki na halionei taifa uchungu.
Kuna uwezekano kabisa siku moja Naibu Spika akaahirisha kikao kwa sababu ya uchache wa wabunge waliopo ndani ya ukumbi, kuna uwezekano akatoa sababu nyingine kabisa ya kuahirisha kikao kwa kuogopa kuwaumbua wabunge wa CCM lakini tatizo likawa wazi kabisa.
Bunge bila ya LISSU,Zitto, Mnyika,Mdee,Maiko,Bulaya,Heche, Kubenea,Pareso, Gekulu sio bunge kabisa hata dunia nzima inatambua.