Ipo siku isiyo na jina Tundu Lissu ndio anaeweza kuwa anasaini kuidhinisha bwana fulani akatibiwe nje ya nchi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Hili wazo nimekuwa nalo kwa muda mrefu na limekuwa likinijia na kupotea na leo tena limenijia hivyo nimeona bora nililete hapa ku-share na wengine.

Ni hivi,hisia zangu zinanionyesha kwamba, ipo siku Tundu Lissu huyu wanaemnyima haki yake ya matibabu,atakuwa kwenye ofisi kubwa ambapo watesi wake watalazimika kusubiri idhini yake wakatibiwe nje ya nchi kama sehemu ya formalities.

Hata kama sahihi yake itakuwa sio takwa la kilazma kisheria,lakini kwa nafasi atakayokuwa nayo wakati huo,anaweza kutumia madaraka kufanya hiki anachofanyiwa leo ila naamini yeye hatalipiza bali itakuwa ni somo tosha kwa watesi wake kuwa maisha yanabadilika na madaraka ni ya kupita tu.

Tundu Lissu anaweza kufika hapo kwa wakati tusioujua na kupitia chama chake cha sasa,chama tofautI au hata kupitia muungano wa vyama vya siasa utakaoundwa wakati huo.

Vile vile sio lazima awe mkulu wakati haya yanatimia, bali anaweza pia kuwa ndio waziri mwenye dhamana na matibabu ya watu wakiwemo watesi wake wa leo.

Kupona kwa Lissu katika mazingira yale si kwa hivi hivi tu, balI nina amini Mungu ana makusudio yake juu ya mtu huyu na kupitia kwa Lissu, atatoa somo kubwa kwa wanadamu hawa waliopewa madaraka na wanayatumia vivyo sivyo

Hifadhi hii thread.
 
Siku zote ukiwa na roho ya kimasikini, utabaki na roho hiyo hiyo ya umasikini wa fikira! Jua DUA la KUKU halimpati mwenye, kaa kila siku ukimwombea Rais mabaya ng'o hutafanikiwa! ila haya mazuri anayoyafanya M/Mungu pia anayaona. Ndo maana anambariki.
 
Very true Mkuu, nani alidhani kuwa miaka kadhaa baada ya Martin Luther King Jr kutoa hotuba ya "I have a dream..." Mtu mweusi tena mwenye bibi, kaka na dada na ndugu walio hai wanaoishi Africa angekuja kuwa Rais wa Marekani.

Nakumbuka story ya Musa na jinsi ambavyo Mungu alimuhifadhi tangia utoto ktk mazingira magumu na baadae ktk nyumba ya Farao na mwisho wa yote akamtumia kuwaongoza watu wake kutoka utumwani kwenda nchi ya ahadi.

Yawezekana Mungu alimnusuru ili siku moja aje kutoa funzo muhimu sana kwa wote watakaojaliwa kuwa hai wakati huo.

Good morning.
 
Mtu akiwa anaongea akasema 'Kwa mfano' Au 'Kwa hisia zangu' huwa huwezi kumbishia Hata Kama analoongea Ni la kufikirika

'Kwa Mfano nikiwa Rais Au Kwa hisia zangu naamini Katavi ina Miundombinu bora ya barabara Kuliko Brussels'
 
IPO SIKU, Mh Tundu Lissu ndio atakua mwanasheria mkuu wa serikali, na ndio atasimamia case zote za "mafisadi, matumizi mabaya ya madaraka, kupotea/kuuliwa kwa raia, na dhuluma iliowahi kufanywa na viongozi wa serikali dhidi ya raia na wafanyabiashara".

IPO SIKU, Mh Tundu Lissu atagoma hizo case zote zisisimamiwe na wanasheria wa serikali (PP na DPP), azisimamie yeye mwenyewe kuanzia;

1) Ukusanyaji wa vielelezo na ushahidi mahakamani.

2) Kuandika mashtaka (Charge Sheet & Information).

3) Kuiwakilisha serikali mahakamani yeye mwenyewe, badala ya kuwaachia wanasheria wadogo wadogo.

4) Kuwahoji yeye mwenyewe washtakiwa mahakamani dhidi ya uvunjifu huo wa sheria mbele ya mahakimu na ma judge.

IPO SIKU, tutafurahi sana.

Nawasilisha,
 
Kwa njia ya mapinduzi ya kijeshi au kupitia kura za wananchi, ndoto za abunuasi!
Kwani Rais wa sasa kaingia kwa mapinduzi ? Ninavyoamini mimi hata yeye miaka kadhaa nyuma, hakufahamu kama atakuwa Rais, ni busara tu za watu ziliwaongoza kumteua kugombea baada ya kuona kuwa bila kuwa na mtu asiyekuwa na makundi, wangepoteza. Ipo siku inaweza kutokea watakaokuwepo, waone kuwa ili ufisadi uishe kabisa nchi hii, fualini ndo anafaa. Huyu aliyepo anaonekana kubagua mafisadi kadhaa kwa mfano katika ya wale waliopewa pesa ya mboga ni nani ameulizwa mahakamani kuwa alipewa pesa kwa kufanya kazi gani ?
 
Back
Top Bottom