Ipo haja ya katiba mpya kuweka sheria ya ndoa za mikataba

Miwatamu

JF-Expert Member
Oct 2, 2012
1,450
487
.

Awali nilikuwa nikijiuliza ni nini hasa chanzo cha kuwepo ndoa za mikataba kwa wenzetu! Baada ya kufuatilia nimeona kuwa hata hapa kwetu sasa ni jambo muafaka kwa jambo hili.


Mara nyingi ukifuatilia mambo yanayosababisha za ndoa nyingi kuvunjika yanafanana kwa ukaribu sana. Nasema kuwa umefika wakati kwa kuwa ndoa nyingi hutokana na mambo ambayo nayo huwepo kwa misimu; aidha iwe ya ki-uwezo (pesa), muhemko wa mapenzi, ulimbukeni tu unaotokana na mtu alikotoka (kuvamia mji), sura, mapenzi kukosa mvuto. Nk.


Hapa nimejaribu kutaja vichache tu ambavyo tulio wengi tunavitumia kama kigezo cha kumchagua mtu kuwa mwenza.
1. Mara nyingi wapenzi wengi (hasa wanawake) humpenda mume kwa kutumia kigezo cha yeye kuwa na pesa kuliko kuangalia vitu vingine. (Pesa zinaisha!)


2. Wapenzi wanaweza kupendana na kuamua kufunga ndoa kutokana na muhemko wa penzi la siku moja tu walilopeana wakati wanafanya uasherati na kulitumia kama kigezo cha ubora wa mahusiano yao (Navyo huchachuka)
3. Wanawake wengine hupenda mume wa kwanza kutokana na ulimbukeni wa kuingia mjini ambapo anakuwa hajaweza kujua maujanja na kuona tofauti ya mtu na mtu. Akishaujua mji huona kuwa chaguo lake la awali halikuwa sahihi! (Mapenzi yamechachuka)


4. Wapenzi wengine hupenda kwa kuangaliana sura na maumbile yao tu! Pindi mtu anapobadilika shepu mwenzie humuona kama kinyago. (Mvuto wa mapenzi huanza kupotea)


5. Wakati penzi linapokuwa change wanandoa huweza kupeaqna penzi hata mara tano kwa siku ili mradi tu kila mmoja anajisikia kuchezea maungo ya mwenzake. Lakini hufika wakati wapenzi hao wanaweza kulala kitanda kimoja kwa mwezi mzima bila kufanya tenbdo la ndoa nah ii ni kwa sababu wote wamepoteza mvuto. ( Penzi limechuja)


6. Kitendo cha mume kupiga bao moja na kulala fofofo bila kuonesha uhitaji tena wakati alikuwa na uwezo wa kup[iga bao hata tano! Huku mwanamke akilala kitandani kama Kondoo wa kafara bila hata kuonesha ushirikiano katika kugonoka, basi yote hayo yanaashiria kuwa penzi limechachuka.


7. Mke na mume, kila mmoja anapoanza kuwa na kibanda cha pembeni ambacho akiwa nacho anapata msisimko war aha ya mapenzi, basi ujue ndani ya nyumba utakuwa umebaki ushahidi tu lakini ndoa halisi haipo. Na hapo tunasema ndoa imekuwa EXPIRED.



Kutokana na haya machache ambayo nimeyaweka hapa, ndipo sisi wana jamvi tunapoweza kuanzia kudadavua zaidi ili kuona umuhimu wa kuwa na ndoa za mkataba ambao unaweza kuwa Renewable kama wahusika wenyewe wataridhiana.


Tulijadili kwa hekima.
 
Back
Top Bottom