Ipi Njia Sahihi ya KuKanda Maumivu ya Viungo?

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
Wakati tunakuwa enzi zetu huku Mwalimu (Marehemu) akiwa amezuia uwepo wa Runinga katika Tanganyika na Majokofu yakiwa nadra majumbani mwetu, tulikuwa tukitumia maji ya moto kuchua viungo ambavyo vimekuwa vikiumia kutokana na shughuli zetu mbaslimbali za kiuchumi, kijamii, burudani, michezo na starehe.

Sikuhizi mtu akiumia maumivu ambayo zamani yalikuwa yanatibiwa kwa kukandwa huwa anawekewa bonge la barafu.

Hebu wenye weledi ya Utabibu mnijuze ni ipi njia sahihi kwa mtu aliyeteguka kumpatia huduma ya kwanza kumkanda kwa maji ya moto au kumbandikia bonge la barafu?
 
Sahihi ni barafu siku ya kwanza ikifatiwa na maji ya moto kuanzia siku ya pili,hii tuliambiwa na mtaalamu wetu wa mazoezi.
 
Back
Top Bottom