Ipi ni bora zaidi kuifanya?

dimaa

JF-Expert Member
Jul 30, 2016
4,019
5,435
Habari zenu viongozi,


Katika suala la kuanzisha maisha wengi wetu hupenda kujipanga kwanza ndo waoe.

Wengine/ wachache hupenda kuoa ndo waje waanze maisha na wenza wao.


Sasa hao wachache wanadai mwanamke akikukuta unakila kitu, yaani nyumba , gari na vyanzo vinginevyo vya mapato wanakuwaga na shida sana.


Afadhali umuoe mje muanze maisha , mchume wote kwa pamoja , hata mkiachana na mkaamua kugawana mlichochuma inakuwa haina athari kwa wote, kwa sababu mmechuma wote kwa pamoja.



Je wewe members wa jf ungependelea chaguo gani kati ya hizo?
 
Mi naona ni vema mwanamke akukute na kila kitu.Vinginevyo utasikia NIMEKUKUTA UNALALA CHINI tukaanza wote leo unaleta nyodo
 
Mi naona ni vema mwanamke akukute na kila kitu.Vinginevyo utasikia NIMEKUKUTA UNALALA CHINI tukaanza wote leo unaleta nyodo
Kumbuka lakini mkiacha mnagawana pasu kwa pasu
 
Jipange kwanza ndio uoe mkuu,kuna utofauti mkubwa wa mabinti wa miaka ya 80s kurudi nyuma na hawa wetu wa 80s kuja 2017
 
Pasupasu ya nini sasa yaani unaingia ndoani ukiwa na mawazo ya talaka jamani mbona mko hivyo?
Hapana, nikitu ambacho unatakiwa uwe nacho akilini huenda kikatokea, nasisi nibinadamu, so lolote laweza tokea.
 
Back
Top Bottom