Ipi insurance Company bomba?

dropingcoco

Senior Member
Jun 21, 2008
124
11
Wadau nina kamkoko kangu nataka nikakatie comprehensive insurance, sasa ningeomba kwa anayejua ni insurance company gani si wasumbufu wa kulipa wakati wa misukosuko anielekeze, hizi ajali za kila siku zinatia simanzi pale ambapo umekatia ki-third party.....nashukuru kwa msaada wenu

NB.....na pia wenye bei nzuri
 
hivi kweli eeh....halafu pia kwa sisi wakinadada nasikia tuna punguzo la asilimia kadhaa kwenye mambo hayo.......wadau msaada plz
 
hivi kweli eeh....halafu pia kwa sisi wakinadada nasikia tuna punguzo la asilimia kadhaa kwenye mambo hayo.......wadau msaada plz

Mwee we mtoto !
 
Phoenix ni wazuri. Usikate ya gari tu fikiria na life insurance
 
nini tena jamani jamani?
Unajua nilivyoiona hiyo rangi nikajua ni post ya Preta, maana nimezoea kuona unapost kwa rangi hiyo kwahiyo sikuhangaika hata kusoma jina. Sasa hapo kwenye nini tena, nikajua unajiuliza swali! Haya tukiacha hayo ni kweli wanawake wanapata punguzo kwenye insurance premium.
 
Unajua nilivyoiona hiyo rangi nikajua ni post ya Preta, maana nimezoea kuona unapost kwa rangi hiyo kwahiyo sikuhangaika hata kusoma jina. Sasa hapo kwenye nini tena, nikajua unajiuliza swali! Haya tukiacha hayo ni kweli wanawake wanapata punguzo kwenye insurance premium.

nieleweshe zaidi mpendwa kwa faida yangu na wenzangu.....hiyo premium ni ipi?
 
hata hao phoenix.......nimewahi pata ajali biliv me...bila kuwakatia ma-asesa wao utaambulia hasara......pamoja na kukata compresive you have to give them something in order to get what you deserve....hauna palipobaki ni rushwa kw akwenda mbele
(REJEA SIGNATURE YANGU HAPO CHINI....NI KATI YA YALIYONIKUTA)
 
nieleweshe zaidi mpendwa kwa faida yangu na wenzangu.....hiyo premium ni ipi?
Oh ni amount unayochajiwa na zile kampuni za insurance ndiyo inaitwa hivyo. Kwahiyo kama unakata comprehensive au otherwise charge yake ni ndogo kwa kina dada/mama, kwa sababu wao risks yao ya kuhusika kwenye ajali ni ndogo. Nadhani hata life cover charges kwa wanawake ni ndogo kutokana na life span yao kuwa kubwa though kwa Tz inaweza kuwa tofauti kutokana na ukweli kwamba maambukizi mengi ya ukimwi ambao kwa kiasi fulani unapunguza life span ni makubwa kwa wanawake. But this is only true km charges zinafanywa scientifically.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom