Elections 2015 IPI AZMA YA ACT-Wazalendo: ZZK Anang'ata na kupuliza

munirah

JF-Expert Member
Mar 13, 2015
551
218
Wanajamvi habarini!

Nimelazimika kuuleta uzi huu hasa baada ya kuona blah blah za kisiasa zinavyozidi kuendelea hapa nchini ikiwemo upinzani kuusema vibaya utawala na jingine upinzani kuusema upinzani!

Katika mkutano wa ACT pale Mwembetogwa mjini Iringa ZZK ananukuliwa akisema kati ya wagombea wa urais kwa tiketi ya UKAWA na CCM hakuna anayetufaa kwa kuwa hawakuwa mstari wa mbele kupambana na rushwa na ufisadi kama Escrow Buzwagi Richmond nk!

Siasa inahadaa umma! Leo ZZK akiyasema haya huku akisahau kuwa chama chake kupitia kauli zake kimesema hakitasimamisha mgombea wa URAIS! ZZK anasahau alikuwa akimkaribisha ENL ajiunge na ACT ikiwa atakuwa tayari kuuanika utajiri wake! Haikuishia hapo ZZK alisikika akifanya imfluence katika audio kuwa vijana wa ACT waliopo ARUSHA waji organise na kumfata ENL na kumkaribisha chamani baada ya mh enl kukatwa Dodoma!

Bado sijaijua sera ya uzalendo wa wana ACT ambayo wao wenyewe hawajaisimamia kwa kuonyesha mfano halisi! Nionavyo mimi.....kitendo cha ENL kuwapa ACT mgongo na kitendo cha ACT kugomewa kujiunga na UKAWA imekuwa mwiba kwao sasa wanasahau kutoa sera zao na kuushambulia upinzani ambao hata hivyo hawatoa majibu!

ZZK nafahamu upo katika wakati wa mpito katika hatua za kuijenga ACT bora ambayo unataka kuwaaminisha watanzania kuwa viongozi wake watakuwa wazalendo hapo baadae! Kwakuwa bado ACT haijawa mpinzani au kwa kuwa bado ni chama kibichi kabisa......nadhani sasa mjipange katika kutoa elimu ya uzalendo kwa raia na pia mtambue kuwa wote mko katika boti moja na wanaUKAWA no matter what!


Unapotuambia wagombea hao hawafai leo hii wakati hauna alternative kutoka chama chako ni sawa na unatuhadaa wananchi! Nina imani kwamba ENL angejiunga na ACT kusingekuwepo kauli hizi za msimu!

Kupitia audio rec ZZK aliskika akisema yupo na mzee Mallah ambae ni mmoja wa madiwani aliyefukuzwa CDM kwa kashfa ya rushwa kule Arusha tena wakati zzk akiwa bado mwanachama hai wa cdm na inawezekana alichangia utimuliwaji huo wa madiwani hao! ACT imempokea Mallah na ZZK anatanabaisha kuwa wapo nae DAR wakiandaa mipango mikakati ya ACT.

Sasa nashindwa kuiona azma ya wana ACT katika kueneza uzalendo kwa kuwa watangazaji wa siasa za kung'ata na kupuliza! Hapo hapo zzk atamsema mgombea wa ccm na hapo hapo wa ukawa akisahau kuwa alikuwa tayari kumkaribisha!

Wazalendo pia wanataka mabadiliko lakini hawaeleweki wapo upande gani! Kauli za Prof KITILA ambaye ni ACT damu katika kipindi cha mwanzo wa ENL kuhama ccm zilipongezwa sana hasa baada ya kusema UKAWA wamesajili mshambuliaji hodari alipohojiwa BBC swahili lakini baadaye akaja kugeuka kuwa upinzani umefanya makosa makubwa kumchukua ENL katika video amesimama mbele ya vendor!


Nitumie rai hii kuwashauri wanasiasa wachunge sana kauli zao na wawe na maono ya mbele kuona kwamba kauli atakayoitoa leo inaweza ikachukuliwa kawaida lakin watu wa leo hawasahau tena! Wanaelewa sana na wanafatilia siasa kwa hamasa kubwa! ACT msiwe mpini wa kuua upinzani bali mjijenge kwa misingi ya uzalendo ambao mnataka kuuaminisha umma kwamba mnautetea! ZZK jitahidi kuzichanga karata zako upya ili mkiwa chama cha upinzani chenye ushawishi hapo baadae muweze kusimamia mlichokiamini!

AMANI IWE NANYI WANAJF WANA-ACT WANA-CCM NA WANA-UKAWA MASLAHI YA TAIFA MBELE ITIKADI BAADAE
 
Mwenyewe ZZK alikuambia usimuamini mwanasiasa yeyote! Leo hii unapinga ufisadi, kesho yake unautakasa. Wapi na wapi?
 
ACT sio chama cha siasa mkuu. Lile ni genge la wahuni, matapeli, wasaliti, majizi na walaghai. Hilo genge liko kwa ajili ya kazi maalumu ya kuisaidia CCM. Sasa hivi Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah anaweweseka. Lakini kwa bahati mbaya sana hiki kimbunga cha Lowassa hakiaacha mtu. Kila kitakayemkuta amekaa vibaya kwenye nafasi za Ubunge na Udiwani huko mikoani kitamswaga akiwemo Ayatollaaah
 
Zitto asubiri miaka 20 hiko chama chake kama kitakuwa hata na wagombea 20.
 
ZZK anaangamia taratibu kujenga chama sio mchezo wote wanamuangalia ZZK mifuko yake na masikini sasa hivi hana access na ATM baada ya kuondoka/kufutwa uanachma CDM ameanza kupauka na nguvu aliyoanza nayo inapungua siku hadi siku na anawaona UKWA ndio wabaya wake.
 
Dah kweli nimeamini kuwa mitz tumerogwa na alieturoga kafwaaa!Leo hii lowasa kawa msafi!!Lowasa aliokipaisha chadema na kujijengea sifa kwakuonekana ni chama kinachotetea wanyonge na kupinga ufisadi et leo kama msafi!Masikin nchi yangu!
ACT sio chama cha siasa mkuu. Lile ni genge la wahuni, matapeli, wasaliti, majizi na walaghai. Hilo genge liko kwa ajili ya kazi maalumu ya kuisaidia CCM. Sasa hivi Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah anaweweseka. Lakini kwa bahati mbaya sana hiki kimbunga cha Lowassa hakiaacha mtu. Kila kitakayemkuta amekaa vibaya kwenye nafasi za Ubunge na Udiwani huko mikoani kitamswaga akiwemo Ayatollaaah
 
Dah kweli nimeamini kuwa mitz tumerogwa na alieturoga kafwaaa!Leo hii lowasa kawa msafi!!Lowasa aliokipaisha chadema na kujijengea sifa kwakuonekana ni chama kinachotetea wanyonge na kupinga ufisadi et leo kama msafi!Masikin nchi yangu!


Kwani kuna binadamu msafi duniani hapa mkuu. Wewe mwenyewe hapo ulipo sio msafi. Wewe ni nani mpaka umwambie kuwa sio msafi. Nitajia mgombea mmojawapo aliye msafi kati ya waliojitokeza mpk sasa ndio tuendelee. Kama hutamtaja shut up your mouth. Huu sio wkt wa kujadili siasa za maji taka, tujadili hoja. Leteni hoja wananchi watawasikiliza lakini sio kuchafua wagombea wengine kwa kisingizio cha usafi. Hatuchagui malaika, tunachagua binadamu awe Rais. Sasa km unahitaji mtu msafi ni vizuri akaenda kutafuta Malaika kule mbinguni sio hapa duniani
 
ZZK anaangamia taratibu kujenga chama sio mchezo wote wanamuangalia ZZK mifuko yake na masikini sasa hivi hana access na ATM baada ya kuondoka/kufutwa uanachma CDM ameanza kupauka na nguvu aliyoanza nayo inapungua siku hadi siku na anawaona UKWA ndio wabaya wake.

Kaka unakosea kukifananisha chama chenye mwaka mmoja unakilinganisha na chama chenye miaka 23.

zitto sio mwanasiasa wa kubabaisha kama unavyodhani. ACT-Wazalendo utaiona vizuri bungeni misingi na sera za chama utaziona kwa vitendo kupitia wabunge wake.

unajua kinachokutatiza unamchukulia zitto uwezo wake unamlinganisha sijui na nani chadema kwa sasa. kidogo labda Dr Slaa wakati huo akiwa ni katibu lakini kwa sasa naye kakaa pembeni.

UKAWA haiwezi kushinda na mtakimbiana baada ya uchaguzi, mtapeana kila aina ya matusi
 
Kaka unakosea kukifananisha chama chenye mwaka mmoja unakilinganisha na chama chenye miaka 23.

zitto sio mwanasiasa wa kubabaisha kama unavyodhani. ACT-Wazalendo utaiona vizuri bungeni misingi na sera za chama utaziona kwa vitendo kupitia wabunge wake.

unajua kinachokutatiza unamchukulia zitto uwezo wake unamlinganisha sijui na nani chadema kwa sasa. kidogo labda Dr Slaa wakati huo akiwa ni katibu lakini kwa sasa naye kakaa pembeni.

UKAWA haiwezi kushinda na mtakimbiana baada ya uchaguzi, mtapeana kila aina ya matusi

Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah ni tapeli, muongo, mlaghai na mnafiki. Zitto hana tofauti na Prof.Lipumba jinsi alivyokuwa anafanya unafiki. Mwisho wake amekuja kuumbuka. Tunazo nondo zote kuhusu Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah na genge lake, tunasubiri muda tu ufike tuanze kuzimwaga. Wewe humfahamu Ayatollaaah vizuri ndio maana mnamuona ni km mungu wenu
 
Kwani kuna binadamu msafi duniani hapa mkuu. Wewe mwenyewe hapo ulipo sio msafi. Wewe ni nani mpaka umwambie kuwa sio msafi. Nitajia mgombea mmojawapo aliye msafi kati ya waliojitokeza mpk sasa ndio tuendelee. Kama hutamtaja shut up your mouth. Huu sio wkt wa kujadili siasa za maji taka, tujadili hoja. Leteni hoja wananchi watawasikiliza lakini sio kuchafua wagombea wengine kwa kisingizio cha usafi. Hatuchagui malaika, tunachagua binadamu awe Rais. Sasa km unahitaji mtu msafi ni vizuri akaenda kutafuta Malaika kule mbinguni sio hapa duniani

Mnapenda kumuiga mbowe vimaneno vyake,nyie kenueni tu ashapiga pesa yule
 
Mnapenda kumuiga mbowe vimaneno vyake,nyie kenueni tu ashapiga pesa yule

Hakuna anayemuiga Mbowe. Tatizo lenu mkiambiwa ukweli mnakimbilia kwenye propaganda za kipuuzi. Mimi simfahamu Mbowe, na wala sijayasema haya kwa niaba ya Mbowe. Nimeyasema mwenyewe kwa niaba yangu binafsi. Wewe subiri muda ushahidi wa yote ninayosema nitautoa mimi. Niko jikoni. Ndio maana nikasema wewe humfahamu Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah vizuri. Unapompigania mtu ni vizuri kujipanga na kufahamu na upande wake wa pili wa shilingi. Otherwise, utakija kuumbuka

ACT sio chama cha siasa, ni genge la wahuni, matapeli na walaghai ambao waliwekwa na CCM kwa ajili ya kudhoofisha nguvu ya vyama vya upinzani vyenye nguvu kwa upande wa bara na Zanzibar. Kwa upande wa huku bara kuna ACT, na kwa upande wa huku Tanganyika kuna ACT. Ushahidi upo na muda ukifika tutautoa. Tunasubiri kampeni zianze ndio tumwage nondo zetu.

Hata ukifuatilia kauli na matendo ya viongozi na mashabiki wa vyama hivi utaona kweli wanafanya kazi waliyotumwa na CCM. Kazi yao kubwa ni kushindana na CHADEMA au CUF kuliko kushindana na CCM ambacho ndicho chama tawala. Mahali kokote duniani sijawahi kuona chama cha siasa kinashindana na chama kingine cha upinzani, ili eti chenyewe ndicho kiwe chama cha upinzani badala ya kingine. Sijawahi kusikia wala kuona kitu km hicho. Ninachojua lengo la chama chochote cha siasa ni kushika dola, si vinginevyo
 
ACT ni waviziaji wa ruzuku..utaona watakavyokaa kimya baada ya Uchaguzi wakishaanza kupokea mgao.Hili ni genge la watafuta ulaji.Kwani unawasikilizaga??
Uti wao mgongo upo CCM na ndo maana wamekuwa funded all over na mifuko ilee iliyowatoa tano bora Dodoma.
 
ACT ni waviziaji wa ruzuku..utaona watakavyokaa kimya baada ya Uchaguzi wakishaanza kupokea mgao.Hili ni genge la watafuta ulaji.Kwani unawasikilizaga??
Uti wao mgongo upo CCM na ndo maana wamekuwa funded all over na mifuko ilee iliyowatoa tano bora Dodoma.

Ulichokisema ni kweli mkuu. Tunazo data zote kuwahusu tunasubiri muda tu. Wao wanadhani mambo wanayoyafanya ni siri kumbe kila kitu kinajulikana. Tutawaumbua wanafiki na matapeli hawa
 
ACT sio chama cha siasa mkuu. Lile ni genge la wahuni, matapeli, wasaliti, majizi na walaghai. Hilo genge liko kwa ajili ya kazi maalumu ya kuisaidia CCM. Sasa hivi Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah anaweweseka. Lakini kwa bahati mbaya sana hiki kimbunga cha Lowassa hakiaacha mtu. Kila kitakayemkuta amekaa vibaya kwenye nafasi za Ubunge na Udiwani huko mikoani kitamswaga akiwemo Ayatollaaah

Bado tu unaamini hivyo mkuu
 
ZZK anaangamia taratibu kujenga chama sio mchezo wote wanamuangalia ZZK mifuko yake na masikini sasa hivi hana access na ATM baada ya kuondoka/kufutwa uanachma CDM ameanza kupauka na nguvu aliyoanza nayo inapungua siku hadi siku na anawaona UKWA ndio wabaya wake.

Bado amepauka , mbona mbowe yeye ameshaasoma alama za nyakati na kumheshimu zitto nyie mmebaki kama vibarka msiokuwa na msaada kwa chadema, 2020, mtapoteana sana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom