Interview ya Nikki Mbishi, Wakazi na P-Mawenge ni ishara kuwa XXL imepoteza dira

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Mar 16, 2015
1,393
3,234
Baada ya Dozen kuhama Clouds FM, Leo XXL wamemfanyia mahojiano Nikki mbishi kuhusu bifu yake na Wakazi pamoja na kuhusu diss track ya P Mawenge, baada ya mahojiano wakawaunganisha live kupitia simu wakazi na p mawenge.

Kiukweli nikiri tu wazi kwamba interview nzima ilikuwa kituko, pengo la B Dozen limeonekana wazi wazi,ukiacha Mchomvu na Mina ally kuuliza maswali pasipo mpangilio, wazo la kuwakuwaunganisha live wasanii hao mahasimu sijalielewa. Je walitaka kuwapatanisha au Kuwagombanisha na kuchochea ugomvi zaidi? Maana mwisho wa siku hawajapatana wameishia kuzozana tu on air, ndiyo maana media zinalalamikiwa kusapoti bifu.

XXL mmefeli kabisa, mnaonesha wazi mmekosa dira baada ya kuondoka kwa Dozen.
 
Nikki kamuuliza wakazi: mlifikia wapi kujua nani ananipenyezea taarifa zenu za kwenye group ma intelligensia wako?

Wakazi: nini?

Nikki: ma intellijensia wako walifikia wapi kujua kwamba nani alikua ananipenyezea taarifa? Au we kile ulichokua unakizungumza pia ulikua unakiona kipo sahihi?

Nikki wa pili alikuambia kuweni na mipaka, mwana fa naye aliwaambieni kua kuweni na mipaka, je mlikua mnaongea nini mle?

Wakazi anakakohoa alafu kacheka anaonekana anajing'atang'ata kutafuta cha kusema.

Nikki mbishi anamjia na swali lingine juu kwa juu kabla swali lake la mwanzo halijajibiwa.

Nikki: unataka ku prove nini kwa watu wakati zile meseji zako zinajieleza??

Nikki mbishi anaamua ku-shut down convo kwa kauli hii

Nikki: Acha unafki oya kata hiyo simu tuendelee na mambo yetu adamu. Saizi sijibu tena swali lingine. Bwana eeh nitaanza kupost tena zile upya watu waone.
 
Kipindi kiligeuka kuwa Cha kupiga kelele mchomvu anauliza swali Niki hajamaliza kujibu nae meena Ally anauliza Tena alafu pia maswali mengi waliokuwa wanauliza si ya msingi kipindi kilikosa leader kabisa pengo la bdozen limeonekana na wasipoangalia kipindi kitazidi kudorora.
 
Kumbe bado hujaelewa industry ya intertainment mkuu...bifu ndo mbinu bora katika industry hyo..bila bifu bila drama bila chokochoko hakuna burudan..nao clouds wanalifaham hilo na ndo umekua msing wa mafanikio yao toka mwanza

Ma ndomana wanautofaut na ITV.TBC na the like
 
Mbona kawaida hilo la kuwaunganisha watu wenye kutoelewana siyo mara ya kwanza liliwahi kutokea hata huyo B12 akiwepo
 
Back
Top Bottom