Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,261
Katika kuendelea kujiweka sawa na patashika ya Vodacom Premier League VPL, Mabingwa wa Nchi Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, leo Jumamosi Oktoba 12, 2019 watakuwa na mechi ya kirafiki dhidi ya Bandari FC kutoka nchini Kenya.
Mchezo huo unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini, utapigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuanzia saa 10:00 jioni, huku Kocha wa Simba SC, Patrick Aussems akisema kikosi chake kimejiandaa vilivyo kucheza na timu nzuri.
"Tumejiandaa na mchezo tukijua tunaenda kucheza na timu nzuri. Utakuwa mchezo nzuri kwa wachezaji kuendelea kuwa fiti na kwetu kama timu kujipima", amesema Kocha Aussems.
•••Wanasimba na wadau wa kandanda karibuni kushuhudia burudani ya pekee yenye viwango vya CAF pamoja na ushindi Uwanja wa Taifa..NguvuMoja
Mchezo huo unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini, utapigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuanzia saa 10:00 jioni, huku Kocha wa Simba SC, Patrick Aussems akisema kikosi chake kimejiandaa vilivyo kucheza na timu nzuri.
"Tumejiandaa na mchezo tukijua tunaenda kucheza na timu nzuri. Utakuwa mchezo nzuri kwa wachezaji kuendelea kuwa fiti na kwetu kama timu kujipima", amesema Kocha Aussems.
•••Wanasimba na wadau wa kandanda karibuni kushuhudia burudani ya pekee yenye viwango vya CAF pamoja na ushindi Uwanja wa Taifa..NguvuMoja