Intensive discussion; ushauri wa kisera kutatua tatizo la ukosefu wa ajira nchini angalau kwa 90%. Visababishi, mkwamo na jinsi ya kutoka

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Kwenye mjadala huu 'serious' tutajadili kwa kina juu ya vipengele vifuatavyo kuhusu hali ya ajira kwa vijana nchini;-

1.Hali ikoje kwa sasa?
2.Matokeo ya tatizo hili la ukosefu wa ajira ni nini kwa wakati huu?
3.Tatizo hili linasababishwa na nini?
4. Hali hii ikiendelea hivyo hatari yake ni nini?
5. Nini kinachofanyika kwa sasa na kwa nini tatizo bado ni kubwa?
6. Ushauri sasa; ni nini tunaweza kufanya na ili iwe nini? na mwisho ni,
7. Faida zitakazopatikana ikiwa ushauri tunaotoa utaonekana unafaa na kupokelewa vizuri.

Hali ya ajira kwa sasa hapa nchini kwetu ikoje kwa picha ya jumla?

Idadi ya vijana ambao angalau wanafika level ya chuo imeongezeka sana kwa miaka ya hivi karibuni. Hata hivyo, pengine zaidi ya 90% hawapati ajira kwenye sekta rasmi. Kwa mfano kuna vijana wengi tu ambao wamemaliza vyuo toka mwaka 2010 na hadi leo wanatafuta ajira na hawajapata.

Hili linafahamika vyema ndio maana tumekuwa tunasikia kauli ya ‘ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiri kulipuka’. Kwa ujumla watu wanakubalina kuwa sio tu kwamba tatizo lipo ila ni serious na lazima kifanyike kitu.
Matokeo ya tatizo hili la ukosefu wa ajira kwa sasa ni nini?

Vijana hawa wanakuwa hawawezi kuzalisha, hawawezi kujitegemea, hawachangii kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi wanakuwa ni watu waliokata tamaaa, wanaoishi wa kuombaomba, kujipendekeza, na inasemekana pia wanapoteza nguvu za kiume (jocking!). Aidha, katika hatua fulani utu na ubinadamu wao unakuwa compromised jambo ambalo linasikitisha sana.
Tatizo hili linasababishwa na nini kwa muhtasari?

Elimu zinazotolewa kwenye mifumo yote rasmi nchini zinamuandaa kijana kuajiriwa huku zikiua uwezo wake wa ubunifu. Kwa bahati mbaya ajira rasmi nazo hazipo kwa sababu kasi ya ukuaji wa sekta binafsi kwa kuzalisha wawekezaji wa ndani na kuvutia wawekezaji wa nje ni ndogo sana kuliko rate ya vijana wanaohitimu kila mwaka.
Hali ikiendelea kama ilivyo hatari yake ni nini mbele ya safari?

Pamoja na athati tajwa hapo juu, kama hatua za haraka zisipochukuliwa, tunaandaa kizazi ambacho sio tu kwamba hakitaweza kutoa mchango kwenye uchumi wa nchi bali pia hakitaweza kujikimu. Kizazi ambacho kitakuwa kimejikatia tamaa ambapo nchi inapokuwa na watu wengi waliokata tamaa na wasio na cha kupoteza ,ni hatari kubwa sana kiusalama.
Nini kinachofanyika kwa sasa na kwa nini tatizo bado ni kubwa?
1. Kutoa mikopo ya elimu ya juu; Serikali imejitahidi kweli kutoa mikopo ya elimu ya juu ili vijana wasome kweli kweli. Kwa bahati mbaya, wakimaliza ajira rasmi hamna, wanakuwa washapoteza ubunifu binafsi na mtaji hawana. Kwa hiyo hawezi kulipa mikopo.

2. Aidha, mikopo hiyo inaongezeka kwa 6% kila mwaka, kwa hiyo aliyekopa 10 M kwa mfano, baada ya miaka 15 ya kushindwa kulipa, anaweza kudaiwa karibu 30M (ambazo hataweza kulipa vile vile maana hana kazi maalum).

3. Mkazo kwenye VETA Ambapo vijana husoma ufundi. Hata hivyo kwa kuwa elimu hii nayo ina mtaala, hatimaye vijana hujikuta wakisomea mitihani na hivyo kuua uwezo wao binafsi wa ubunifu kwa kiasi fulani, hivyo hujikuta wakisubiria kuajiriwa vile vile, ajira ambazo kimsingi hazipo. Aidha, hata wale wanaobaki na ubunifu, hujikuta hawana mtaji kwa hiyo hawawezi kujiajiri na hivyo kurejea kwenye mzunguko wa tatizo.

4. Kuhimiza uwekezaji wa nje na ndani ambapo pamoja na serikali kujitahidi sana kwenye eneo hili, uwekezaji wa ndani unakuwa mgumu kwa sababu watu wengi hawana mitaji (miongoni mwa mambo mengine) na wawekezaji wa nje hawaji kwa kasi kubwa inayowezesha kutoa ajira za kutosha.

5. Kuhimiza kufanya kazi kwa kujitolea; Kuna fikra kuwa watu hawapati ajira kwa sababu hawana uzoefu kitu ambacho sio sahihi. Kutokana na fikra hiyo, vijana huhimizwa kujitolea sehemu mbalimbali, hatimaye baada ya kujitolea hujikuta hakuna la ziada kwa kuwa nafasi za kazi ni chache kuliko waliojitolea.Hatimaye huwajibika tena kuingia mtaani wakiwa hawana hili wala lile.

Kwa mantiki hiyo tunaomba kushauri sasa, kwa lengo la kuchochea mjadala na kupata mawazo mapana.
Ushauri sasa; ni nini tunaweza kufanya na ili iwe nini?

1. Elimu ya msingi iwe mpaka kidato cha nne. Lengo hapo ni kijana aweze kujua mambo ya msingi ya jumla. Katika kipindi hicho, vijana wawekewe mazingira ya kuvitambua vipaji vyao.

2. Baada ya kumaliza kidato cha nne, kuwe na mirengo mitatu;-

(a) Vijana wanaoendelea na kidato cha tano hadi vyuo. Mrengo huu usipewe kipaumbele sana maana kwanza ajira zake ni chache na pili unaandaa mameneja ambao hawatakiwi kuwa wengi. Hapa wapewe kipaumbele wale walioko ki-academics sanaaaa. Mrengo huu uchukue kama (20%) tu ya vijana wote.

(b) Mrengo wa VETA; Huu uchukue angalau (30) ya vijana kwa ajili ya kuandaa technicians, ambao nao kwa kiasi kikubwa pia watategemea kuajiriwa. Na,

(c) Mrengo wa kujiajiri ambapo kila kijana atachagua kazi anayoitaka kulingana na kipaji chake. Mrengo huu utachukua (50%) ya vijana wote waliobaki. Eneo hili ndilo linapaswa kupewa kipaumbele cha juu sana maana ndio litakalozalisha wawekezaji wa ndani ambao ndio watakaoajiri kundi (a&b hapo juu) Kwa hiyo hapa ndio tutakuwa tunatengeneza matajiri wenyewe sasa.
Hapa jukumu la serikali itakuwa ni

(i) Kutengeneza mfumo wa coaching & mentorship ambapo kila kijana atasaidiwa na coach au mentor kujipangia malengo na kuyatekeleza kwa ubunifu binafsi na pale anapokwama kupata ujuzi flani anapewa connections ya kuipata ujuzi husika (ikumbukwe sasa hivi solutions nyingi zinapatikana kwenye internet tu)

(ii) Kuwapatia mikopo vijana hawa ambayo itatumika kama mitaji ya kuanzia. Mikopo hii itapatika kutoka kwenye fungu litakalookolewa kwa wale wa elimu ya juu ambao watakuwa wamepungua. Inaweza kuongezewa kidogo kutoka kwenye vyanzo vingine kama itakavyoonekaa inafaaa.
Faida zitakazopatikana ikiwa ushauri tunaotoa utaonekana unafaa na kupokelewa vizuri.

1. Hao vijana 50% ambao watakuwa ni wawekezaji wandani watakuwa sio tu kwamba wamepata ajira bali ni matajiri chipukizi.Kwa mara ya kwanza kama taifa tutakuwa tumeanza kuzalisha matajiri wetu wenyewe kwenye batches.

2. Hii 50% ya vijana ambayo ni wawekezaji wa ndani itaajiri 30% ya technicians kutoka VETA na 20% ya mameneja ambao wameenda hadi vyuo vikuu (kama ilivyoelezwa kwenye (a&b hapo awali). Matokeo yake tatizo la ukosefu wa ajira litakuwa limeshatatuliwa kwa karibu 100%.

3. Mfumo huu utawezesha makundi yote kuweza kulipa mkopo tofauti na sasa ambapo karibu wote hawawezi kulipa maana hawana ajira.

4. Karibu vijana wote watakuwa wanaweza kuzalisha kwa ajili ya kujikumu na kujenga familia na kuishi maisha yenye heshima.

5. Karibu vijana wote watakuwa wanachangia kwenye ukuaji wa pato la taifa na kuchangamsha uchumi wa nchi kwa kiwango cha juu sana.

6. Uhalifu utashuka hadi karibu 0%
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Hali ya ajira kwa sasa hapa nchini kwetu ikoje kwa picha ya jumla?

Idadi ya vijana ambao angalau wanafika level ya chuo imeongezeka sana kwa miaka ya hivi karibuni. Hata hivyo, pengine zaidi ya 90% hawapati ajira kwenye sekta rasmi. Kwa mfano kuna vijana wengi tu ambao wamemaliza vyuo toka mwaka 2010 na hadi leo wanatafuta ajira na hawajapata.

Hili linafahamika vyema ndio maana tumekuwa tunasikia kauli ya ‘ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiri kulipuka’. Kwa ujumla watu wanakubalina kuwa sio tu kwamba tatizo lipo ila ni serious na lazima kifanyike kitu.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Matokeo ya tatizo hili la ukosefu wa ajira kwa sasa ni nini?

Vijana hawa wanakuwa hawawezi kuzalisha, hawawezi kujitegemea, hawachangii kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi wanakuwa ni watu waliokata tamaaa, wanaoishi wa kuombaomba, kujipendekeza, na inasemekana pia wanapoteza nguvu za kiume (jocking!). Aidha, katika hatua fulani utu na ubinadamu wao unakuwa compromised jambo ambalo linasikitisha sana.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Tatizo hili linasababishwa na nini kwa muhtasari?

Elimu zinazotolewa kwenye mifumo yote rasmi nchini zinamuandaa kijana kuajiriwa huku zikiua uwezo wake wa ubunifu. Kwa bahati mbaya ajira rasmi nazo hazipo kwa sababu kasi ya ukuaji wa sekta binafsi kwa kuzalisha wawekezaji wa ndani na kuvutia wawekezaji wa nje ni ndogo sana kuliko rate ya vijana wanaohitimu kila mwaka.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Hali ikiendelea kama ilivyo hatari yake ni nini mbele ya safari?

Pamoja na athati tajwa hapo juu, kama hatua za haraka zisipochukuliwa, tunaandaa kizazi ambacho sio tu kwamba hakitaweza kutoa mchango kwenye uchumi wa nchi bali pia hakitaweza kujikimu.

Kizazi ambacho kitakuwa kimejikatia tamaa ambapo nchi inapokuwa na watu wengi waliokata tamaa na wasio na cha kupoteza ,ni hatari kubwa sana kiusalama.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Nini kinachofanyika kwa sasa na kwa nini tatizo bado ni kubwa?
1. Kutoa mikopo ya elimu ya juu; Serikali imejitahidi kweli kutoa mikopo ya elimu ya juu ili vijana wasome kweli kweli. Kwa bahati mbaya, wakimaliza ajira rasmi hamna, wanakuwa washapoteza ubunifu binafsi na mtaji hawana. Kwa hiyo hawezi kulipa mikopo.

2. Aidha, mikopo hiyo inaongezeka kwa 6% kila mwaka, kwa hiyo aliyekopa 10 M kwa mfano, baada ya miaka 15 ya kushindwa kulipa, anaweza kudaiwa karibu 30M (ambazo hataweza kulipa vile vile maana hana kazi maalum).

3. Mkazo kwenye VETA Ambapo vijana husoma ufundi. Hata hivyo kwa kuwa elimu hii nayo ina mtaala, hatimaye vijana hujikuta wakisomea mitihani na hivyo kuua uwezo wao binafsi wa ubunifu kwa kiasi fulani, hivyo hujikuta wakisubiria kuajiriwa vile vile, ajira ambazo kimsingi hazipo. Aidha, hata wale wanaobaki na ubunifu, hujikuta hawana mtaji kwa hiyo hawawezi kujiajiri na hivyo kurejea kwenye mzunguko wa tatizo.

4. Kuhimiza uwekezaji wa nje na ndani ambapo pamoja na serikali kujitahidi sana kwenye eneo hili, uwekezaji wa ndani unakuwa mgumu kwa sababu watu wengi hawana mitaji (miongoni mwa mambo mengine) na wawekezaji wa nje hawaji kwa kasi kubwa inayowezesha kutoa ajira za kutosha.

5. Kuhimiza kufanya kazi kwa kujitolea; Kuna fikra kuwa watu hawapati ajira kwa sababu hawana uzoefu kitu ambacho sio sahihi. Kutokana na fikra hiyo, vijana huhimizwa kujitolea sehemu mbalimbali, hatimaye baada ya kujitolea hujikuta hakuna la ziada kwa kuwa nafasi za kazi ni chache kuliko waliojitolea.Hatimaye huwajibika tena kuingia mtaani wakiwa hawana hili wala lile.

Kwa mantiki hiyo tunaomba kushauri sasa, kwa lengo la kuchochea mjadala na kupata mawazo mapana.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Ushauri sasa; ni nini tunaweza kufanya na ili iwe nini?

1. Elimu ya msingi iwe mpaka kidato cha nne. Lengo hapo ni kijana aweze kujua mambo ya msingi ya jumla. Katika kipindi hicho, vijana wawekewe mazingira ya kuvitambua vipaji vyao.

2. Baada ya kumaliza kidato cha nne, kuwe na mirengo mitatu;-

(a) Vijana wanaoendelea na kidato cha tano hadi vyuo. Mrengo huu usipewe kipaumbele sana maana kwanza ajira zake ni chache na pili unaandaa mameneja ambao hawatakiwi kuwa wengi. Hapa wapewe kipaumbele wale walioko ki-academics sanaaaa. Mrengo huu uchukue kama (20%) tu ya vijana wote.

(b) Mrengo wa VETA; Huu uchukue angalau (30) ya vijana kwa ajili ya kuandaa technicians, ambao nao kwa kiasi kikubwa pia watategemea kuajiriwa. Na,

(c) Mrengo wa kujiajiri ambapo kila kijana atachagua kazi anayoitaka kulingana na kipaji chake. Mrengo huu utachukua (50%) ya vijana wote waliobaki. Eneo hili ndilo linapaswa kupewa kipaumbele cha juu sana maana ndio litakalozalisha wawekezaji wa ndani ambao ndio watakaoajiri kundi (a&b hapo juu) Kwa hiyo hapa ndio tutakuwa tunatengeneza matajiri wenyewe sasa.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Hapa jukumu la serikali itakuwa ni

(i) Kutengeneza mfumo wa coaching & mentorship ambapo kila kijana atasaidiwa na coach au mentor kujipangia malengo na kuyatekeleza kwa ubunifu binafsi na pale anapokwama kupata ujuzi flani anapewa connections ya kuipata ujuzi husika (ikumbukwe sasa hivi solutions nyingi zinapatikana kwenye internet tu)

(ii) Kuwapatia mikopo vijana hawa ambayo itatumika kama mitaji ya kuanzia. Mikopo hii itapatika kutoka kwenye fungu litakalookolewa kwa wale wa elimu ya juu ambao watakuwa wamepungua. Inaweza kuongezewa kidogo kutoka kwenye vyanzo vingine kama itakavyoonekaa inafaaa.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Faida zitakazopatikana ikiwa ushauri tunaotoa utaonekana unafaa na kupokelewa vizuri.

1. Hao vijana 50% ambao watakuwa ni wawekezaji wandani watakuwa sio tu kwamba wamepata ajira bali ni matajiri chipukizi.Kwa mara ya kwanza kama taifa tutakuwa tumeanza kuzalisha matajiri wetu wenyewe kwenye batches.

2. Hii 50% ya vijana ambayo ni wawekezaji wa ndani itaajiri 30% ya technicians kutoka VETA na 20% ya mameneja ambao wameenda hadi vyuo vikuu (kama ilivyoelezwa kwenye (a&b hapo awali). Matokeo yake tatizo la ukosefu wa ajira litakuwa limeshatatuliwa kwa karibu 100%.

3. Mfumo huu utawezesha makundi yote kuweza kulipa mkopo tofauti na sasa ambapo karibu wote hawawezi kulipa maana hawana ajira.

4. Karibu vijana wote watakuwa wanaweza kuzalisha kwa ajili ya kujikumu na kujenga familia na kuishi maisha yenye heshima.

5. Karibu vijana wote watakuwa wanachangia kwenye ukuaji wa pato la taifa na kuchangamsha uchumi wa nchi kwa kiwango cha juu sana.

6. Uhalifu utashuka hadi karibu 0%
 

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,954
12,519
Nimekusoma mpaka mwisho...

You are very good. Ni mawazo mazuri na yaliyojaa ushauri murua kabisa..

Kikwazo kikubwa cha haya ni SIASA ZETU CHAFU na KUKOSEKANA KWA UONGOZI BORA...

Hapa penyewe baada ya makala yako hii, wapo watu ambao hata hawatakusoma na kukuelewa..

Watakachofanya ni kusoma title ya article yako tu. Na kama haisemi lolote lililofanywa na Mwendazake na kisha kumsifia, basi wewe si lolote wala chochote na utaitwa "wakala wa mabeberu" au "CHADEMA wewe"...

Thank you..
 

macho_mdiliko

JF-Expert Member
Mar 10, 2008
17,703
27,840
Hapa jukumu la serikali itakuwa ni

(i) Kutengeneza mfumo wa coaching & mentorship ambapo kila kijana atasaidiwa na coach au mentor kujipangia malengo na kuyatekeleza kwa ubunifu binafsi na pale anapokwama kupata ujuzi flani anapewa connections ya kuipata ujuzi husika (ikumbukwe sasa hivi solutions nyingi zinapatikana kwenye internet tu)

(ii) Kuwapatia mikopo vijana hawa ambayo itatumika kama mitaji ya kuanzia. Mikopo hii itapatika kutoka kwenye fungu litakalookolewa kwa wale wa elimu ya juu ambao watakuwa wamepungua. Inaweza kuongezewa kidogo kutoka kwenye vyanzo vingine kama itakavyoonekaa inafaaa.
Tanzania maneno ni mengi. Tuna ardhi kubwa, yenye rutuba na hali ya hewa nzuri. Laiti tungeendelea na ile motto ya mwa. Nyerere ya ''Kilimo ndiyo uti wa Mgongo wetu'' tungekuwa mbali sasa hivi. Tungefanya somo la kilimo liwe lazima na kila shule iwe na mashamba ya mfano. Tulime bila kutumia chemical na mazao yetu tuya-brand hayana chemical. Tutafute masoko duniani kote tuilishe dunia. Hili ni jambo lililo kwenye uwezo wetu na lingeajiri watu wengi. Vinginevyo hata tukiandika ma-paper na ma-paper bila vitendo hatutafika popote.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Tanzania maneno ni mengi. Tuna ardhi kubwa, yenye rutuba na hali ya hewa nzuri. Laiti tungeendelea na ile motto ya mwa. Nyerere ya ''Kilimo ndiyo uti wa Mgongo wetu'' tungekuwa mbali sasa hivi. Tungefanya somo la kilimo liwe lazima na kila shule iwe na mashamba ya mfano. Tulime bila kutumia chemical na mazao yetu tuya-brand hayana chemical. Tutafute masoko duniani kote tuilishe dunia. Hili ni jambo lililo kwenye uwezo wetu na lingeajiri watu wengi. Vinginevyo hata tukiandika ma-paper na ma-paper bila vitendo hatutafika popote.
Mkuu wazo lako ni zuri. Hata hivyo, hicho kilimo chenyewe kinahitaji mtaji. Bila mtaji kijana hawezi kutoboa. Ndio mantiki ya mkopo tunayoizungumzia hapo juu. Pili, Kilimo 'practice' hakihitaji sana kusoma 'kilimo academics'

kwa mfano darasa la saba anaweza kulima kwa mafanikio sana kama ana mtaji na kwa msaada wa tutorials za youtube na internet, kuliko mtu aliyesomea kilimo darasani miaka 10.

Tatu haipaswi kila mtu kuwa mkulima hata kama anaweza kulima. Inatakiwa watu watawanyike kwenye sector nyingi ndio hapo tunaposema toka awali kila mtu achague anachokipenda na anachokimudu kisha afanyiwe coaching and mentoring baada ya kupatiwa mkopo.

Tukifanya hivyo tutafanikiwa sana ndugu yangu.
 

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,954
12,519
Mkuu inawezekana unahoja nzuri sana ila hujafafanua. Unaweza kufafanua hoja yako kwa kina zaidi inaweza kuwa na faida kubwa.
Ni rahisi kama hivi...

Kama tunataka kutoboa, sharti tu- decentralize madaraka + resources...

Tutengeneze mifumo ambayo itaruhusu watu kulingana na locality zao, wataweza kujipangia namna njema ya ku - manage day to day welfare zao bila kusubiri mamlaka nyingine iamue kuhusu mambo yao...

Mfumo tulio nao sasa, ni kweli una kitu kinaitwa "serikali za mitaa" kwa maana kuwa wananchi wana mamlaka kamili...

Lakini huu siyo ukweli. Serikali za mitaa kwa sasa ziko theoretically zaidi. Yaani hakuna practicability...

Hizi zinazoitwa serikali za mitaa kwa sasa, zinazoweza kufanya ni kuchagua viongozi tu hakuna zaidi ya hapo..

Hazina uwezo wa kukusanya mapato yake yenyewe na kupanga kuyatumia kulingana na mahitaji..

Chochote kinachokusanywa, kinakabidhiwa kwa Central Government nayo inaamua ipeleke nini kwa nani...

Kinachohitajika sasa ni kuacha CG ishughulike na mambo makubwa ya kitaifa na mambo yanayohusu localities yashughulikiwe na serikali za maeneo husika huku serikali hizo zikiwajibika moja kwa moja CG...

Tuendelee kujadiliana
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
sawa mkuu The Palm Tree ngoja tuone mawazo ya wadau wengine kama yapo maana moja ya changamoto tuliyo nayo ni watu kulaumu juu ya uwepo wa tatizo ila nao unakuta hawana solution, wanataka wengine waamue na watakeleze wao waridhishwe tu.
 

macho_mdiliko

JF-Expert Member
Mar 10, 2008
17,703
27,840
Mkuu wazo lako ni zuri. Hata hivyo, hicho kilimo chenyewe kinahitaji mtaji. Bila mtaji kijana hawezi kutoboa. Ndio mantiki ya mkopo tunayoizungumzia hapo juu. Pili, Kilimo 'practice' hakihitaji sana kusoma 'kilimo academics'

kwa mfano darasa la saba anaweza kulima kwa mafanikio sana kama ana mtaji na kwa msaada wa tutorials za youtube na internet, kuliko mtu aliyesomea kilimo darasani miaka 10.

Tatu haipaswi kila mtu kuwa mkulima hata kama anaweza kulima. Inatakiwa watu watawanyike kwenye sector nyingi ndio hapo tunaposema toka awali kila mtu achague anachokipenda na anachokimudu kisha afanyiwe coaching and mentoring baada ya kupatiwa mkopo.

Tukifanya hivyo tutafanikiwa sana ndugu yangu.
Andiko lako la mwanzoni nilikubaliana nalo kabisa. Ila tu nilitaka tuchague kitu rahisi tunachoweza kukifanya. Nakubali kabisa kilimo kinahitaji mtaji lakini mtaji wake siyo mkubwa kama sekta nyingine. Kuhusu elimu ya kilimo: Ni lazima. Ni lazima watu wasome wapate nadharia kama mazao yetu tunataka yakubalike kwenye soko la dunia. Hili halikwepeki. Na wakati wanasoma wantakiwa wafanye mambo practically. Mimi nilibahatika kusoma shule ya kanisa na ilikuwa na bustani nyingi za mboga. Hivyo primary school yangu yote tulikuwa tunafanya kilimo cha bustani kwa vitendo. Kuanzia kusiha mbegu kwenye vitalu mpaka knamna ya kuvuna mboga. Na mpaka sasa hivi nakumbuka na mwaka juzi nilijaribu kulima bustani za mboga kila mtu akashangaa zilivyomea na kuzaa vizuri. Nataka tu kuonyesha kuwa kitu ukisoma na kufanya shuleni hutakaa usahau na utafanya kwa ufasaha sana. Of course siyo kila mtu atakuwa mkulima lakini ni lazima tupate pa kuanzia. Ukishafaulu kwenye jambo moja kufanya jambo jingine ni rahisi sana. Tatizo letu tunajifanya kuweka vipaumbele vingi na mwishowe vyote vinashindikana. Na zaidi kilimo kinaenda sambamba na jira nyingine nyingi kama usafirishaji, viwanda n.k. Ni lazima tutafute jambo moja tuliwekee mkazo wa hali ya juu, japo mengine hatuyapuuza.
 

denooJ

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
15,114
55,237
Hii issue naona iko complicated sana, elimu, ajira au uwekezaji plus masoko ni vitu ambavyo kwangu naona vinaenda kwa pamoja, hivyo vyote lazima vifanyiwe kazi kwa pamoja, kikibaki kimoja tatizo litaendelea kuwepo.

Iko hivi, huyu kijana alietoka VETA mfano akajihusisha na kilimo, ataenda shambani kulima akiwa ameshawezeshwa kwa mkopo na serikali kama ulivyosema, na mkopo atakaopewa hapa lazima uwe wa maana ili aweze kumudu mahitaji yote ya shamba effectivelly, na wakati mwingine mambo shambani yanaweza kuyumba akajikuta anatumia zaidi ya alichonacho mfukoni.

Sasa hapa tukuchulie amevuna vizuri, je, masoko ya kuuza kwa wakati mazao yake yatakuwepo ya nje na ndani? au bado tatizo la masoko litaendelea kuwepo na kusababisha mazao ya huyu kijana kuharibikia shambani?

Lakini pia naipata picha nyingine hapa, serikali itatakiwa kujipanga haswa ku-provide financial assistance kwa hawa vijana, kwasababu wanaomaliza vyuo kwa mwaka ni wengi sana, sidhani kama serikali itaweza kuubeba huu mzigo bila msaada, hapa ningeshauri na sekta binafsi ihusishwe kwenye kutoa hiyo mikopo kwa riba ndogo kwa makubaliano maalum na serikali ( serikali iangalie namna ya kuwawezesha private sector ku sustain kutoa mikopo).

Kwa hali tuliyonayo sasa, naona ili hii hali angalau ianze kupungua, serikali itoe tender kwa makampuni binafsi, badala ya hizi tender kutolewa kwa taasisi za serikali kama majeshi, hili litasaidia kuongeza mzunguko wa pesa mtaani hivyo hali za wengi zitaanza kubadilika taratibu, hata kama kijana akiamua kuuza karanga atleast atakuwa na uhakika wa kuingiza kiasi fulani kwa siku, tofauti na hali ilivyo sasa, watu hawana pesa mifukoni, wafanyakazi wanalia mishahara midogo na hawa wangesaidia kupunguza tatizo kama hali zao zingekuwa nafuu, wangekuwa madukani na masokoni wakinunua bidhaa mbalimbali hivyo kuwaunga mkono hawa vijana wasio na ajira.
 

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,150
7,328
Mkuu denooJ unetoa mchango mzuri. Ningependa kuchangia kwenye maeneo mawili.

Kwanza kuhusu masoko ya mazao ya kilimo, kuna mazao yenye soko kubwa duniani, tatizo tunashindwa kufikia masoko hayo kwa sababu hatuzalishi kwa wingi na kwa uendelevu. Kwa mfano, China wanaingiza soya kutoka marekani yenye thamani ya mabilioni ya dola kila mwaka na bado haiwatoshi. Mfano wakituambia Tanzania tuwe tunawauzia tani 100000 kila mwezi tunaweza?

Kingine kuhusu mikopo kutoka sekta binafsi, sector binafsi haitakubali kukopesha mtu bila colateral kama nyumba hivi, na aina ya watu tunaowazungumzia hawana nyumba watu kitu chochote cha maana.

Mwisho nakubaliana na wewe kwamba kutatua tatizo la ajira, reforms kwenye elimu, masoko na uwekezaji lazima viende pamoja
 

Baba Nla

JF-Expert Member
Nov 21, 2018
568
1,436
Mkuu nafuatilia huu mjadala kwa makini nikiwa mmoja wa vijana wengi waliohitimu na kukosa ajira rasmi..
Itoshe kusema pia sisi wahitimu wengi ni WAVIVU hasa kwenye kutafuta jinsi gani ya kuanza kupiga hatua za maendeleo, hivyo kuibebesha mzigo serikali kwa sasa nafikiri sio sawa labda kwa miaka ijayo, kwa sasa ni lazima nasi vijana tuzishughulishe akili zetu kuona ni jinsi gani tunaweza kuanza kujitegemea.
Kiukweli inauma kijana kuwa tegemezi, nakumbuka kuna uzi humu unasema "vijana 25-33 yrs wanawategemea wazazi au mashemeji" hii ishu ipo jaman na kiukweli bila kubadilisha mentality ya kundi hili la vijana lililopo bado serikali itazidi kubebeshwa mzigo mkubwa, ila ni wakati sasa wa serikali kubadilika ili kupunguza future errors..
NLA!
 
3 Reactions
Reply
Top Bottom