Miwatamu
JF-Expert Member
- Oct 2, 2012
- 1,450
- 487
Ndugu wana jamvi, kwa kila mtu anayependa amani, uhuru na mshikamano ambao umekuwepo kwa kipindi chote tangu tupate uhuru, hakika ataanza kujiuliza mara mbilimbili ni wapi tumeteleza nawapi tuendako kwa sasa!!
Watu wengi wamekuwa wakiinyoshea serikali kidole kwa lengo jema tu, la kutaka kuitawala nchi hii kwa mjibu wa sheria na kanuni zilizowekwa. Lakini kinyume na hapo mfumo wa utawala umebadilika na kuwa wa aina moja! Nasema hivyo kwa kuwa sasa hivi kuanzia nyumbani kwako, ofisini, kwenye vijiwe na kwingineko, ili mtu uonekane wa maana lazima uwe unaunga mkono mfumo uliopo hata kama ni mbovu.
Waona mbali wamekuwa wakikosoa kuwa mfumo wa kufanya taasisi ya ulinzi kuwa ni sehemu ya chama tawala, ipo siku italeta sintofahamu katika jamii au Taifa kwa ujumla. Sasa kitu hicho tumeanza kukiona! Kitendo cha Kamanda wa Mkoa wa Mwanza kuuawa ni kielelezo tosha kuwa sasa hali si shwari. Polisi wameshindwa kulinda nchi na wananchi wake, sasa njia mbadala itafikia hatua kila kundi linajitengenezea interijensia yake ya kujilinda! Na hapo ndipo taabu itakapokuwa imeanzia.
My take: ili kukomesha haya yasiendelee, tunaomba serikali isimamie haki pale panapostahili ili kila mtu aamini kuwa kitengo cha usalama kipo kwa ajili ya watu wote na nchi yao. Vinginevyo makubwa zaidi ya hili la Mwanza na Mbagala tutaendelea kuyaona sana.
Je, wewe unasemaje kwa hili?
Watu wengi wamekuwa wakiinyoshea serikali kidole kwa lengo jema tu, la kutaka kuitawala nchi hii kwa mjibu wa sheria na kanuni zilizowekwa. Lakini kinyume na hapo mfumo wa utawala umebadilika na kuwa wa aina moja! Nasema hivyo kwa kuwa sasa hivi kuanzia nyumbani kwako, ofisini, kwenye vijiwe na kwingineko, ili mtu uonekane wa maana lazima uwe unaunga mkono mfumo uliopo hata kama ni mbovu.
Waona mbali wamekuwa wakikosoa kuwa mfumo wa kufanya taasisi ya ulinzi kuwa ni sehemu ya chama tawala, ipo siku italeta sintofahamu katika jamii au Taifa kwa ujumla. Sasa kitu hicho tumeanza kukiona! Kitendo cha Kamanda wa Mkoa wa Mwanza kuuawa ni kielelezo tosha kuwa sasa hali si shwari. Polisi wameshindwa kulinda nchi na wananchi wake, sasa njia mbadala itafikia hatua kila kundi linajitengenezea interijensia yake ya kujilinda! Na hapo ndipo taabu itakapokuwa imeanzia.
My take: ili kukomesha haya yasiendelee, tunaomba serikali isimamie haki pale panapostahili ili kila mtu aamini kuwa kitengo cha usalama kipo kwa ajili ya watu wote na nchi yao. Vinginevyo makubwa zaidi ya hili la Mwanza na Mbagala tutaendelea kuyaona sana.
Je, wewe unasemaje kwa hili?