intel imeshikwa kubaya na AMD

Nafaka

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
12,156
31,043
Naona review za processor mpya za Ryzen ni kuwa zimeipiga mtama mkali intel mbali kabisa likija suala la gaming. Wataalam wa mambo wanasema kwamba technology ya AMD ni hatari sana na intel bado anahangaika na 7nm kiasi kwamba hata processor alizotoa zilikuwa chache kiasi kwamba wateja wake waliamua kutazama kwingine, na AMD akachukua nafasi kujazia huo uhaba. Wataalam wa mambo wanadai japo intel bado ni Giant kwenye ulimwengu huo akiwa na market share kubwa kabisa, ila wanasema mambo yakiendelea hivi atakula za uso. AMD kwasasa amejiamini kiasikwamba processor zake zinauzwa bei kuliko za intel wakati siku za nyuma alikuwa yeye anauza cheap.
ry.jpg

Chief-Mkwawa njoo uongeze nyama
ry.jpg
 
Naona review za processor mpya za Ryzen ni kuwa zimeipiga mtama mkali intel mbali kabisa likija suala la gaming. Wataalam wa mambo wanasema kwamba technology ya AMD ni hatari sana na intel bado anahangaika na 7nm kiasi kwamba hata processor alizotoa zilikuwa chache kiasi kwamba wateja wake waliamua kutazama kwingine, na AMD akachukua nafasi kujazia huo uhaba. Wataalam wa mambo wanadai japo intel bado ni Giant kwenye ulimwengu huo akiwa na market share kubwa kabisa, ila wanasema mambo yakiendelea hivi atakula za uso. AMD kwasasa amejiamini kiasikwamba processor zake zinauzwa bei kuliko za intel wakati siku za nyuma alikuwa yeye anauza cheap.
View attachment 1621476
Chief-Mkwawa njoo uongeze nyama
View attachment 1621476
Nimeona reviews Mkuu ya Anandtech, Intel amekuwa destroyed vibaya mno,

Ujue siku nyingi Ryzen ilishaipita core ya intel kwenye Ipc, sema Intel alikuwa na advantage ya frequency, hii ryzen 5000 series nayo inafika 5ghz hivyo intel hana advantage.

Kwenye laptop sema Tiger lake inafanya vizuri ina ipc na graphics kali kuliko Ryzen 4000 series za laptop.

Ngoja tuone intel atajibu nini kwenye Desktop na Rocket lake.
 
Nimeona reviews Mkuu ya Anandtech, Intel amekuwa destroyed vibaya mno,

Ujue siku nyingi Ryzen ilishaipita core ya intel kwenye Ipc, sema Intel alikuwa na advantage ya frequency, hii ryzen 5000 series nayo inafika 5ghz hivyo intel hana advantage.

Kwenye laptop sema Tiger lake inafanya vizuri ina ipc na graphics kali kuliko Ryzen 4000 series za laptop.

Ngoja tuone intel atajibu nini kwenye Desktop na Rocket lake.
Bado naogopa kujaribu maana niliwahi kumili HP flani ilikuwa na AMD zamani 2010, ilikuwa inapata moto wakati nilinunua mpya mcty, na ilikuwa ina visanga sana.
 
Bado naogopa kujaribu maana niliwahi kumili HP flani ilikuwa na AMD zamani 2010, ilikuwa inapata moto wakati nilinunua mpya mcty, na ilikuwa ina visanga sana.
Sababu ni manufacturing process ya kizamani, 28nm ama zaidi. Hizi za 7nm ama 5nm zipo vizuri.

Sema bado Amd hawajakuwa serious kwenye cpu za watts kidogo kama Intel walivyo na core m ya watts 4.
 
Sababu ni manufacturing process ya kizamani, 28nm ama zaidi. Hizi za 7nm ama 5nm zipo vizuri.

Sema bado Amd hawajakuwa serious kwenye cpu za watts kidogo kama Intel walivyo na core m ya watts 4.
Siku hizi nilijua umuhimu wa kununua PC kutokana na matumizi yako. Zamani nilikuwa nataka PC iwe na specifcs kubwa haijaishi nataka kuifanyia kazi gani. Ila toka ninunue Dell inspiron 11 Series 3000 2-1nimeridhika maana hata kama umem umekata nafanya kazi pasipo kuwa online inakaa na charge masaa saba ili mradi nisiwe online na ziwe kazi za office, na kama naplay kitu kiwe audio pia iwe kwenye energy saver. Sema ina processor ndogo sana ila kwa kusurf na kazi zangu iko safi sana
 
Siku hizi nilijua umuhimu wa kununua PC kutokana na matumizi yako. Zamani nilikuwa nataka PC iwe na specifcs kubwa haijaishi nataka kuifanyia kazi gani. Ila toka ninunue Dell inspiron 11 Series 3000 2-1nimeridhika maana hata kama umem umekata nafanya kazi pasipo kuwa online inakaa na charge masaa saba ili mradi nisiwe online na ziwe kazi za office, na kama naplay kitu kiwe audio pia iwe kwenye energy saver. Sema ina processor ndogo sana ila kwa kusurf na kazi zangu iko safi sana
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 bd sana
 
Mkuu hivi hp elitebook 725 g2 yenye processor ya amd A8 pro-7150B r5, 10 compute core 4c+6g (4cpu) 1.9 GHz

Inafaa kununuliwa kwa 500k?
Haifai mkuu, kwa Amd nunua Ryzen tu ndio nzuri cpu zake, Amd za zamani hazina issue.
 
Mkuu ni wapi naweza pata hp slim laptop nzuri kwa bei 500k?

Nilikua natamani sana nipate hp folio 9480
Andika Google folio 9480 tsh zitakuja results za kutosha tu, capricorn, discount kubwa, etc.

Bei 550k mpaka 600k Sema hizo ni bei za online tu unaweza kuwashusha kidogo.
 
Mkuu
Andika Google folio 9480 tsh zitakuja results za kutosha tu, capricorn, discount kubwa, etc.

Bei 550k mpaka 600k Sema hizo ni bei za online tu unaweza kuwashusha kidogo.
Mkuu kuna hii hp probook 440 g4

Core i5 7200U cpu 2.5ghz 2.71ghz ram 8gb

Hii inafaa kwa laki 6?


Mkuu naona jamaa anasema hii ni ssd je ni kweli?
 
Mkuu
Mkuu kuna hii hp probook 440 g4

Core i5 7200U cpu 2.5ghz 2.71ghz ram 8gb

Hii inafaa kwa laki 6?


Mkuu naona jamaa anasema hii ni ssd je ni kweli?
Sio mbaya kwa hio bei, hasa ikiwa na ssd. Na laptop yoyote inaweza kuwa na ssd
 
AMD imetengenezwa specific kwenye sehemu za baridi lakin bongo hapa itachemka mno mpaka mashine itazima pamoja wanajaribu kuweka fen nyingi lakin hapa bongo Intel bado wanawashika
 
AMD imetengenezwa specific kwenye sehemu za baridi lakin bongo hapa itachemka mno mpaka mashine itazima pamoja wanajaribu kuweka fen nyingi lakin hapa bongo Intel bado wanawashika
Hizo ni Amd za zamani kabla Ya Ryzen.

Hizi ryzen ni efficient zaidi ina maana hata kwenye kupata joto hazipati sana.
 
Back
Top Bottom