ecolizer baba
Member
- Sep 29, 2010
- 88
- 310
Wakuu wanaJF
Leo ndiyo ile siku ambayo madaktari waliweka wazi kuwa watagoma endapo serekali itashindwa kuwasimamisha kazi mawaziri wa afya. Napost uzi huu ili kujua hali ikoje kwa wale walio karibu na hospitali zetu hususan MUHIMBILI, KCMC, BUGANDO, DODOMA, MBEYA n.k,Je? Kuna madaktari kazini?
Na vipi wananchi wa kawaida wanasemaje kuhusu mvutano huu kati ya serikali na madaktari?
Lakini pia ikumbukwe kuwa waziri mkuu Pinda alipokuwa anaongea na madaktari tar 9/02/2012 pale CPL MNH aliwaahidi wananchi kuwa serikali ina nia ya dhati kutatua mgogoro kwenye sekta ya afya na kwa kuanza akawasimamisha Blandina Nyoni( aliyeteuliwa na kuapishwa na rais) na Deo Mtasiwa( sina uhakika aliteuliwa na nani labda mnisaidie).
Sasa kama pinda alimsimamisha kazi mteule wa rais ambaye ndiye mtendaji mkuu wa wizara na kusema kuwa atamshauri rais awafukuze mawaziri je?
1. kwa nini asiwe na mamlaka ya kuwasimamisha wateuele wengine wa rais ambao wako ofisi moja na katibu mkuu?
2. au hakushuri rais kama alivyo ahidi kufanya? Na kama ni hivyo ina maana aliudanganya umma hivyo anapaswa kujiuzulu mara moja kulinda heshima yake.
3. kama alimshauri rais halafu huyu bwana mkubwa akapuuzia pia anapaswa kuonesha nia yake ya dhati ya kuwatetea wanyonge kwa kujiuzulu maana amedharauliwa kupita kiasi.
4. kama madaktari wataendelea na msimamo wao wa kugoma hadi serikali iwafukuze mawaziri na serikali ikakataa kwa madai kuwa rais hafanyi kazi kwa shinikizo, je? serikali itaweza kuwafukuza madaktari wote na kuajiri wengine au itaendelea kuatimua wanajeshi kutibu raia?
5. Na vipi kwa upande wa madaktari, je? wapo tayari kushikilia msimamo wao hadi mwisho bila kusalitiana endapo wataambiwa warudi kazini mmoja mmoja kwa kusaini makubaliano maalumu?
KITU KINGINE KILICHONISHANGAZA NI KWAMBA YALE MATANGAZO YALIYOKUWA YAMEBANDIKWA KWENYE NGUZO NA KUTA ZA HOSPITALI YA MUHIMBILI TOKA JANA NA ZIKASOMWA NA WATU WENGI WAKIWAMO WAGONJWA WENYEWE LEO HAZIPO! Nani kuziondoa? Ni Njelekela? Ni wagonjwa? Ni usalama wa taifa? au ni upepo ulioambatana na mvua kali? Na kama serikali itaendelea kutumia hizi mbinu za kitoto na za zamani kuzima na kuzuia taarifa kuwafikia wananchi mfano kubandua matangazo yaliyobandikwa na MAT, je tutafika? Na kama hali yenyewe ya utatuzi wa matatizo ni kuondoa matangazo yanayopasha wananchi ukweli wa kwa nini madaktari wanagoma, je? serikali ina nia ya dhati kusuluhisha mgogoro huu au ndiyo inachochea?
WAKUU NAOMBA TUJADILI HAYA MAMBO KWA KINA BILA KUELEMEA UPANDE WOWOTE ILI UKWELI UJULIKANE.
Leo ndiyo ile siku ambayo madaktari waliweka wazi kuwa watagoma endapo serekali itashindwa kuwasimamisha kazi mawaziri wa afya. Napost uzi huu ili kujua hali ikoje kwa wale walio karibu na hospitali zetu hususan MUHIMBILI, KCMC, BUGANDO, DODOMA, MBEYA n.k,Je? Kuna madaktari kazini?
Na vipi wananchi wa kawaida wanasemaje kuhusu mvutano huu kati ya serikali na madaktari?
Lakini pia ikumbukwe kuwa waziri mkuu Pinda alipokuwa anaongea na madaktari tar 9/02/2012 pale CPL MNH aliwaahidi wananchi kuwa serikali ina nia ya dhati kutatua mgogoro kwenye sekta ya afya na kwa kuanza akawasimamisha Blandina Nyoni( aliyeteuliwa na kuapishwa na rais) na Deo Mtasiwa( sina uhakika aliteuliwa na nani labda mnisaidie).
Sasa kama pinda alimsimamisha kazi mteule wa rais ambaye ndiye mtendaji mkuu wa wizara na kusema kuwa atamshauri rais awafukuze mawaziri je?
1. kwa nini asiwe na mamlaka ya kuwasimamisha wateuele wengine wa rais ambao wako ofisi moja na katibu mkuu?
2. au hakushuri rais kama alivyo ahidi kufanya? Na kama ni hivyo ina maana aliudanganya umma hivyo anapaswa kujiuzulu mara moja kulinda heshima yake.
3. kama alimshauri rais halafu huyu bwana mkubwa akapuuzia pia anapaswa kuonesha nia yake ya dhati ya kuwatetea wanyonge kwa kujiuzulu maana amedharauliwa kupita kiasi.
4. kama madaktari wataendelea na msimamo wao wa kugoma hadi serikali iwafukuze mawaziri na serikali ikakataa kwa madai kuwa rais hafanyi kazi kwa shinikizo, je? serikali itaweza kuwafukuza madaktari wote na kuajiri wengine au itaendelea kuatimua wanajeshi kutibu raia?
5. Na vipi kwa upande wa madaktari, je? wapo tayari kushikilia msimamo wao hadi mwisho bila kusalitiana endapo wataambiwa warudi kazini mmoja mmoja kwa kusaini makubaliano maalumu?
KITU KINGINE KILICHONISHANGAZA NI KWAMBA YALE MATANGAZO YALIYOKUWA YAMEBANDIKWA KWENYE NGUZO NA KUTA ZA HOSPITALI YA MUHIMBILI TOKA JANA NA ZIKASOMWA NA WATU WENGI WAKIWAMO WAGONJWA WENYEWE LEO HAZIPO! Nani kuziondoa? Ni Njelekela? Ni wagonjwa? Ni usalama wa taifa? au ni upepo ulioambatana na mvua kali? Na kama serikali itaendelea kutumia hizi mbinu za kitoto na za zamani kuzima na kuzuia taarifa kuwafikia wananchi mfano kubandua matangazo yaliyobandikwa na MAT, je tutafika? Na kama hali yenyewe ya utatuzi wa matatizo ni kuondoa matangazo yanayopasha wananchi ukweli wa kwa nini madaktari wanagoma, je? serikali ina nia ya dhati kusuluhisha mgogoro huu au ndiyo inachochea?
WAKUU NAOMBA TUJADILI HAYA MAMBO KWA KINA BILA KUELEMEA UPANDE WOWOTE ILI UKWELI UJULIKANE.