the ultimatum
JF-Expert Member
- Dec 16, 2012
- 402
- 114
Na BBC Swahili
MV Nyerere: Familia yangu iliandaa mazishi yangu
Jina la Injinia Augustine Cherehani lilianza kuvuma katika vyombo vya habari vya ndani na nje ya Tanzania siku tatu baada ya kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere kilichokuwa kikifanya safari zake katika ziwa Victoria kati ya kisiwa cha Ukerewe na Ukara.
Injinia Augustine Cherehani katika kile kilichowaacha wengi vinywa wazi aliokolewa wakati tumaini la kupata walio hai likiwa limesha malizika.
'Siku kama siku nyingine'
Siku ya tukio Injinia anasema ilkuwa siku kama siku nyingine lakini kwao kwa misingi ya usafirishaji ilikuwa siku ya kazi kubwa kwani ilikuwa ni siku ya gulio eneo la Bugorora.
Kawaida wakazi wa kisiwa cha Ukara hufurika gulioni kujipatia mahitaji mbalimbali na siku hiyo ilikuwa vivyo hivyo.
Kabla ya safari kama kawaida alikagua chombo (MV Nyerere) zikiwemo Injini zake mbili mpya na kujiridhisha kuwa chombo kilikuwa tayari kwa safari kutoka Bugorora (Ukerewe) kueleka Bwisya (Ukara)
Baada ya kuwasha Injini alimruhusu Nahodha kuianza safari ambayo kwa kawaida huchukua wastani wa dakika arobaini na tano (45) hadi saa moja.
Baada kukamilisha wajibu huu wa muhimu, Injinia huyo mwenye miaka 53 mkaazi wa Magu Masanza jijini Mwanza alirejea katika chumba cha injini na kuketi katika kiti chake kuhakikisha hali ya injini zake ni shwari mpaka Mv Nyerere itakapo kita nanga.
Augustine Cherehani: Injinia aliyenusurika baada ya kuzama MV Nyerere
''Ninacho kumbuka ni kwamba nilijikuta niko chini ni kama mtu kapigwa ngwara''
Maji yaki panda kasi ya wastani tayari yalisha mvuka kiunoni lakini Injini tiifu za Mv Nyerere bado zilikuwa zikifanya kazi kabla ya kumwaga oili na kuzima.
''Injini zile zimezimika, wakati ule zimeshapata moto, na sasa zikaanza kupoozwa na maji kwa kweli ile dakika ya kwanza mpaka ya ishirini ilikuwa ni kazi kubwa sana na nilihisi naweza kufa mapema sana kwa moshi kabla ya maji''.
Image captionInjinia ni Cherehani ni baba wa watoto wanne wasichana wawili na wavulana wawili, ambayo walikuwa moyoni mwake wakati wote wa mkasa huo
Jua linachomoza kwa walio nje ya MV Nyerere, lakini simanzi kwa wakazi wa wilaya ya Ukerewe, Tanzania inashusha bendera yake nusu mlingoti, hili si jambo la kawaida hakika taifa hili kubwa Afrika ya mashariki liko katika maombolezo.
Raisi John Pombe Magufuli anatuma salamu za pole na maombolezo salamu ambazo injinia Cherehani hazipati ila kwa uzoefu na utaalamu wa kibaharia anajua taifa linalia.
Kwake kiza kinaendelea na mara hii maji yanelekea kifuani, usiku wa pili usiku ambao ulikuwa na ndoto nyingi za mauti, anaposikia sauti za waokozi nje yeye anaendela kugonga akiwa na tumaini atasikika.
Mtalamu huyu anagonga kitaalamu , 1 2 3 ishara za kibaharaia na mabaharia wenzake wamsikia na kumgongea 1 2 3 anashusha pumzi na kuamini huenda aka uona tena uso wa Mke wake na watoto wake wapenzi.
Lakini si leo maana punde kimya kinatawala na yeye anajua sasa ni usiku umeingia, siku ya tatu bila maji wala chakula.
''…namshukuru Mungu alinipa uvumilivu nikasema kwamba kama ni kifo na kinikute hapa hapa".
Haki miliki ya pichaSTEVE MSENGI, AFISA HABARI WILAYA YA UKEREWE
Hakika subira huvuta kheri, mzamiaji huyu alikuja mara tatu na safari hii alimgonga begani na kumwambia ''bwana nimekuja kukuchukua lakini kabla ya hapo naomba nikupe darasa, kama utafanya mchezo nitakutoa marehemu"
Baada ya dakika kadhaa za hofu na kukata tamaa ndipo kamera za waandishi wa habari zilipo mmulika, na waandishi hao kuandika: 'Injinia Mkuu wa MV Nyerere aokolewa siku tatu baada kuzama kwake akiwa amejipaka weli chafu'.
Kati ya Mwaka 2009 hadi 2017 Mwezi wa tano Injinia huyu anayeliona jua baada ya siku tau alihudumu kama injinia mkuu katika vivuko vya serikali ya Tanzania kigongo ferry kabla ya kuhamishiwa Ukerewa kukihudumia kivuko cha MV Nyerere mwezi wa tano mwaka 2017 hadi siku ya mkasa huu usio sahaulika.
''Kuna namba yoyote unayo ikumbuka nikamwambia ni ya mke wangu, unaweza kunitajia nimwambie? ndipo nilipo mtajia, akanipa kuongea naye aliposikia sauti yangu akaniambia inabidi umwombe Mungu sana sisi tayari tulishaweka msiba hapa''.
Kwa Picha: Sehemu za ndani za gari lililotumika kumteka Mo Dewji
Wanasiasa wanacheza karata mjadala wa mageuzi ya katiba Kenya
Baada ya kuokolewa, Injinia huyu alipatiwa huduma ya kwanza katika kituo cha afya cha Bwisya na kuchukuliwa kwa helikopta ya polisi kupelekwa hospitali ya rufaa Bugando na kupatiwa matibabu kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.
'Ila mpaka sasa bado na hudhuria kliniki katika hospitali hiyo'.
MV Nyerere: Familia yangu iliandaa mazishi yangu
Jina la Injinia Augustine Cherehani lilianza kuvuma katika vyombo vya habari vya ndani na nje ya Tanzania siku tatu baada ya kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere kilichokuwa kikifanya safari zake katika ziwa Victoria kati ya kisiwa cha Ukerewe na Ukara.
Injinia Augustine Cherehani katika kile kilichowaacha wengi vinywa wazi aliokolewa wakati tumaini la kupata walio hai likiwa limesha malizika.
- Saudia yabanwa mbavu mauaji ya Khashoggi
- Mgahawa ambapo wateja hulipa kwa njia ya Bitcoin Kenya
- Mwanasiasa wa upinzani anayedaiwa kupanga kumuua Rais Pierre Nkurunziza
Siku ya tukio Injinia anasema ilkuwa siku kama siku nyingine lakini kwao kwa misingi ya usafirishaji ilikuwa siku ya kazi kubwa kwani ilikuwa ni siku ya gulio eneo la Bugorora.
Kawaida wakazi wa kisiwa cha Ukara hufurika gulioni kujipatia mahitaji mbalimbali na siku hiyo ilikuwa vivyo hivyo.
Kabla ya safari kama kawaida alikagua chombo (MV Nyerere) zikiwemo Injini zake mbili mpya na kujiridhisha kuwa chombo kilikuwa tayari kwa safari kutoka Bugorora (Ukerewe) kueleka Bwisya (Ukara)
Baada ya kuwasha Injini alimruhusu Nahodha kuianza safari ambayo kwa kawaida huchukua wastani wa dakika arobaini na tano (45) hadi saa moja.
- MV Nyerere: Je kuna mabadiliko yoyote mwezi mmoja baadaye?
- Magufuli avunja bodi ya Sumatra na ile ya ushauri ya Tamesa Tanzania
Baada kukamilisha wajibu huu wa muhimu, Injinia huyo mwenye miaka 53 mkaazi wa Magu Masanza jijini Mwanza alirejea katika chumba cha injini na kuketi katika kiti chake kuhakikisha hali ya injini zake ni shwari mpaka Mv Nyerere itakapo kita nanga.
Augustine Cherehani: Injinia aliyenusurika baada ya kuzama MV Nyerere
''Ninacho kumbuka ni kwamba nilijikuta niko chini ni kama mtu kapigwa ngwara''
''Ninacho kumbuka ni kwamba nilijikuta niko chini ni kama mtu kapigwa ngwara''Augustine Cherehani, Injinia mkuu MV Nyerere
Mara hii MV Nyerere ilisimama bila ya kukita nanga lakini pia injini zake ambazo amekuwa akizikagua mara zote, safari hii zilikuwa juu na yeye chini jambo ambalo si la kawaida, ndipo alipogundua hali si shwari hata kujisema moyoni ''hii ya leo nayo ni kali''.Maji yaki panda kasi ya wastani tayari yalisha mvuka kiunoni lakini Injini tiifu za Mv Nyerere bado zilikuwa zikifanya kazi kabla ya kumwaga oili na kuzima.
''Injini zile zimezimika, wakati ule zimeshapata moto, na sasa zikaanza kupoozwa na maji kwa kweli ile dakika ya kwanza mpaka ya ishirini ilikuwa ni kazi kubwa sana na nilihisi naweza kufa mapema sana kwa moshi kabla ya maji''.
- Mwanafunzi ashtakiwa baada ya kumtishia mwalimu silaha bandia
- Kwa nini Wanaigeria wanailalamikia Tanzania?
Jua linachomoza kwa walio nje ya MV Nyerere, lakini simanzi kwa wakazi wa wilaya ya Ukerewe, Tanzania inashusha bendera yake nusu mlingoti, hili si jambo la kawaida hakika taifa hili kubwa Afrika ya mashariki liko katika maombolezo.
Raisi John Pombe Magufuli anatuma salamu za pole na maombolezo salamu ambazo injinia Cherehani hazipati ila kwa uzoefu na utaalamu wa kibaharia anajua taifa linalia.
Kwake kiza kinaendelea na mara hii maji yanelekea kifuani, usiku wa pili usiku ambao ulikuwa na ndoto nyingi za mauti, anaposikia sauti za waokozi nje yeye anaendela kugonga akiwa na tumaini atasikika.
Mtalamu huyu anagonga kitaalamu , 1 2 3 ishara za kibaharaia na mabaharia wenzake wamsikia na kumgongea 1 2 3 anashusha pumzi na kuamini huenda aka uona tena uso wa Mke wake na watoto wake wapenzi.
Lakini si leo maana punde kimya kinatawala na yeye anajua sasa ni usiku umeingia, siku ya tatu bila maji wala chakula.
- Je upinzani una makali kiasi gani Afrika ?
- Rekodi mpya ya dola bilioni 1.6 bahati nasibu nchini Marekani
''…namshukuru Mungu alinipa uvumilivu nikasema kwamba kama ni kifo na kinikute hapa hapa".
Hakika subira huvuta kheri, mzamiaji huyu alikuja mara tatu na safari hii alimgonga begani na kumwambia ''bwana nimekuja kukuchukua lakini kabla ya hapo naomba nikupe darasa, kama utafanya mchezo nitakutoa marehemu"
Baada ya dakika kadhaa za hofu na kukata tamaa ndipo kamera za waandishi wa habari zilipo mmulika, na waandishi hao kuandika: 'Injinia Mkuu wa MV Nyerere aokolewa siku tatu baada kuzama kwake akiwa amejipaka weli chafu'.
Kati ya Mwaka 2009 hadi 2017 Mwezi wa tano Injinia huyu anayeliona jua baada ya siku tau alihudumu kama injinia mkuu katika vivuko vya serikali ya Tanzania kigongo ferry kabla ya kuhamishiwa Ukerewa kukihudumia kivuko cha MV Nyerere mwezi wa tano mwaka 2017 hadi siku ya mkasa huu usio sahaulika.
''Kuna namba yoyote unayo ikumbuka nikamwambia ni ya mke wangu, unaweza kunitajia nimwambie? ndipo nilipo mtajia, akanipa kuongea naye aliposikia sauti yangu akaniambia inabidi umwombe Mungu sana sisi tayari tulishaweka msiba hapa''.
Kwa Picha: Sehemu za ndani za gari lililotumika kumteka Mo Dewji
Wanasiasa wanacheza karata mjadala wa mageuzi ya katiba Kenya
Baada ya kuokolewa, Injinia huyu alipatiwa huduma ya kwanza katika kituo cha afya cha Bwisya na kuchukuliwa kwa helikopta ya polisi kupelekwa hospitali ya rufaa Bugando na kupatiwa matibabu kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.
'Ila mpaka sasa bado na hudhuria kliniki katika hospitali hiyo'.