Uchaguzi 2020 Ingekuwa katika Nchi za wenzetu, Nyalandu na wenzake wangejitoa na kumuachia Lissu

Anaweza kupata kura za aibu hiyo Jumanne.

Nikuambie Waziri wa Vitalu vya maliasili alishaumaliza huu Mchezo zamani?Fedha fedha mikoani?
ingawa hana uwezo kwa Lisssu lakini ndo hivyo kuna Mjumbe hapendi nyumba au piki piki?
 
Lissu angekubalika angekuwa Mwenyekiti
Mpaka muda huu, nashindwa kuwaelewa Nyalandu na wenzake kwani nyakati zinambeba Lissu kwa asilimia 100.

Kwa hali ilivyo, ingekuwa ni katika nchi za wenzetu,mfano US, mtu kama Nyalandu naamini angetangaza kujitoa na kumuunga mkono Lissu bila kusubiri kupigwa kura na wajumbe.

Anyway, wacha tusubiri lakini huku ni kushindwa tu kusoma alama za nyakati kwa kisingizio cha demokrasia, demokrasia ambayo haimpi nafasi yeye na wenzake.

Hata hivyo,hii itakuwa ni fursa ya Lissu kuonyesha kukubalika kwake ndani ya chama kulinganisha na wagombea wenzake.

Wacha tusubiri labda kuna wanaopanga kujitoa siku ya kupiga kura kupitisha mgombea na kumuunga mkono Lissu maana siasa ndio zilivyo.
 
Acha demokrasia ifanye kazi yake.

Mbona CCM alipochukua fomu mmoja tu tumepiga kelele sana?

What if waliona anafaa wakamwachia?

Tuache double standard
Hapa ndipo utaona mapungufu yao.

Sasa nyalandu ajitoaje wakati ni haki yake?
Mimi naangalia hili picha linavyoenda na usikute Nyalandu atashinda kura za maoni ila watamkata jina lake.

Wanajua kutoa kibanzi kwa CCM tu ila maboroti yao hawayaoni .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi zingine hununua wagombea pinzani wajitoe mfano Ni hapo Kenya unaletewa mabox ya pesa na mgombea uraisi au mgombea ubunge anasema hi nafasi naitaka chukua haya mabilioni jitoe niachie

Nyalandu Ni mkristo mshika dini hanunuliki .Hizo nchi unazosema za nje ndicho hufanya Watu hawajitoi bila kulamba pesa ya uhakika

Hata ku form alliance Kama ile ya UKAWA pesa ya Lowasa ilibidi imwagwe Hadi kwa akina Lisu Baada ya kuipata wakampisha na kuimba Lowasa mabadiliko , mabadiliko Lowasa!!! Nyalandu hahongeki ana pesa za kufa mtu hizo porojo zako za nchi zingine
Kwanza kwanini ajitoe?
Hana Haki ya kugombea?
Wakimtoa watakuwa watu wa hovyo Sana kuwahi kutokea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi zingine hununua wagombea pinzani wajitoe mfano Ni hapo Kenya unaletewa mabox ya pesa na mgombea uraisi au mgombea ubunge anasema hi nafasi naitaka chukua haya mabilioni jitoe niachie

Nyalandu Ni mkristo mshika dini hanunuliki .Hizo nchi unazosema za nje ndicho hufanya Watu hawajitoi bila kulamba pesa ya uhakika

Hata ku form alliance Kama ile ya UKAWA pesa ya Lowasa ilibidi imwagwe Hadi kwa akina Lisu Baada ya kuipata wakampisha na kuimba Lowasa mabadiliko , mabadiliko Lowasa!!! Nyalandu hahongeki ana pesa za kufa mtu hizo porojo zako za nchi zingine
I can see the logic ni kama unatuambia Magufuli alihonga ili achukue fomu peke yake.
 
Hapa sikubaliani na wewe mkuu!
Ikiwa mnalalamikia m/kiti wa ccm kujiandalia fomu 1 tu kwa kuogopa kushindanishwa na wenzake ndani ya chama na hivyo kukanyaga demokrasia ndani ya chama chake + udikteta. Vipi na ninyi mnatamani kufanya yale yale?
Mnaogopa nini?
Mnahubiri demokrasia gani?

Kama unasema ni nyakati za Lissu, why uogope?
Binafsi najua pia kwamba Lissu ni mtu sahihi kabisa kumkabili JPM na anakubalika na watu wengi si tu Chadema, bali hata huko ccm pia.
Nstumaini atashinda, ila napendekeza ashinde kwa kupigiwa kura. Amini tu kwamba Nyaradu hatotoboa mbele ya Lissu, usitishwe na ushindi wake wa awali mkuu.
Hivi unaelewa maana ya kujitoa?Kujitoa unajitoa law hiari yako na ni kawaida kabisa na.sio kwa kushinikizwa.

Watu wagumu kue!ewa!
 
Kwenye msafara wa mamba,hata kenge wamo!
Hivi nyie Nyalandu mnadhani ni mwenzenu? Nyalandu atarudi CCM muda muafaka ukifika. Mimi naweza nina uwezo mkubwa wa kujua watu wenye dhamira ya nia ya kuwa upinzani na watu walioko huko kimkakakati. Wapinzani kama wanajua kusoma alama za nyakati, mtu sahihi wa kusimamisha kwa sasa ni Membe. Lissu ni mzuri sana, na namkubali sana ila tu kwa kipindi hiki Membe ndiye aliye kwenye nafasi nzuri zaidi ya kukubalika na watu wa aina mbalimbali. Lissu anaweza kupata support kubwa lakini watu potential wa kumpigia kura ni vijana na wapinzani wakereketwa. Membe akiungwa mkono na Lissu atavutia wale mashabiki wa Lissu na wengine kutoka CCM na watu wasio na hisia kali za upinzani.
 
Hivi nyie Nyalandu mnadhani ni mwenzenu? Nyalandu atarudi CCM muda muafaka ukifika. Mimi naweza nina uwezo mkubwa wa kujua watu wenye dhamira ya nia ya kuwa upinzani na watu walioko huko kimkakakati. Wapinzani kama wanajua kusoma alama za nyakati, mtu sahihi wa kusimamisha kwa sasa ni Membe. Lissu ni mzuri sana, na namkubali sana ila tu kwa kipindi hiki Membe ndiye aliye kwenye nafasi nzuri zaidi ya kukubalika na watu wa aina mbalimbali. Lissu anaweza kupata support kubwa lakini watu potential wa kumpigia kura ni vijana na wapinzani wakereketwa. Membe akiungwa mkono na Lissu atavutia wale mashabiki wa Lissu na wengine kutoka CCM na watu wasio na hisia kali za upinzani.

'Mimi naweza nina uwezo mkubwa wa kujua watu wenye dhamira ya nia ya kuwa upinzani na watu walioko huko kimkakakati.'

Na hapo hapo unasema tena:

'Wapinzani kama wanajua kusoma alama za nyakati, mtu sahihi wa kusimamisha kwa sasa ni Membe.'

Hakika dunia ina maajabu yake.
 
'Mimi naweza nina uwezo mkubwa wa kujua watu wenye dhamira ya nia ya kuwa upinzani na watu walioko huko kimkakakati.'

Na hapo hapo unasema tena:

'Wapinzani kama wanajua kusoma alama za nyakati, mtu sahihi wa kusimamisha kwa sasa ni Membe.'

Hakika dunia ina maajabu yake.
Of Course wewe utaona ni maajabu kwa sababu unadhani Membe amekuja upinzani kimkakati. Ni kweli asingekuja upinzani kama CCM mambo yangekuwa mazuri lakini hii haimaanishi kaenda huko kufanya hujuma. Najua watanzania ni wagumu sana na wengi hawana uwezo wa kutafakari na kupima mambo kwa kina bali kukariri na ndiyo maana baada ya Lowassa kurudi CCM wameshakaririshwa kuwa alienda huko kuhujumu. Ukweli ni kwamba Lowassa alikwenda upinzani akidhamiria na alikuwa tishio kubwa kwa walifanikiwa ku-kushinda na asingerudi huko kama siyo afya yake kuwa mbaya.
 
Sielewi unayaonaje ni mawazo ya hovyo kama wanachama, wapenzi na washabiki wengi wa Chadema wanataka Lissu ndiyo abebe bendera ya Chadema kugombea nafasi ya Urais.
Ni mawazo ya hovyo kutaka Nyalandu ajitoe.
Kwani Hana Haki ya kugombea??
Mbona mnataka atoke hata kabla ya kura ya maoni...hii ndiyo demokrasia mnayoipiga kelele kila siku??

Kwa staili hii upinzani hamji kushika dola .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nyie Nyalandu mnadhani ni mwenzenu? Nyalandu atarudi CCM muda muafaka ukifika. Mimi naweza nina uwezo mkubwa wa kujua watu wenye dhamira ya nia ya kuwa upinzani na watu walioko huko kimkakakati. Wapinzani kama wanajua kusoma alama za nyakati, mtu sahihi wa kusimamisha kwa sasa ni Membe. Lissu ni mzuri sana, na namkubali sana ila tu kwa kipindi hiki Membe ndiye aliye kwenye nafasi nzuri zaidi ya kukubalika na watu wa aina mbalimbali. Lissu anaweza kupata support kubwa lakini watu potential wa kumpigia kura ni vijana na wapinzani wakereketwa. Membe akiungwa mkono na Lissu atavutia wale mashabiki wa Lissu na wengine kutoka CCM na watu wasio na hisia kali za upinzani.

BAK njoo ujionee miujiza mzee baba.
 
Of Course wewe utaona ni maajabu kwa sababu unadhani Membe amekuja upinzani kimkakati. Ni kweli asingekuja upinzani kama CCM mambo yangekuwa mazuri lakini hii haimaanishi kaenda huko kufanya hujuma. Najua watanzania ni wagumu sana na wengi hawana uwezo wa kutafakari na kupima mambo kwa kina bali kukariri na ndiyo maana baada ya Lowassa kurudi CCM wameshakaririshwa kuwa alienda huko kuhujumu. Ukweli ni kwamba Lowassa alikwenda upinzani akidhamiria na alikuwa tishio kubwa kwa walifanikiwa ku-kushinda na asingerudi huko kama siyo afya yake kuwa mbaya.
'Ni kweli asingekuja upinzani kama CCM mambo yangekuwa mazuri'.

Roger that.
 
Back
Top Bottom