Ziroseventytwo
JF-Expert Member
- Mar 27, 2011
- 7,971
- 13,605
Kila kosa au amri lina/ina adhabu yake,kwa mujibu wa sheria. Wakati Mungu akiumba dunia hakukuwa na sheria au amri kwa mujibu wa maandiko(bibilia). Amri ya kwanza kabisa duniani ni USILE TUNDA LA MTI WA KATIKATI, na ukila adhabu yake ilikuwa ni kifo..nanukuu hakika siku mkila tunda la mti ule wa ktkt hakika mtakufa!. Ndivyo alivyowaambia Adam na Hawa. Hawa alikuwa wa kwanza kula tunda, then akampa na Adam, mungu alipowatokea pale bustani, badala ya kuwapa ile adhabu ya kifo papo hapo, akawafukuza bustanini,..adhabu ya kifo ikabaki palepale, akaongeza na nyingi ambaya ni ngumu zaidi "UTAKULA KWA JASHO" ardhi imelaaniwa kwa ajili yetu! Kiukweli adhabu hii ni ngumu sana..bora tungebakiziwa adhabu hii ya kifo kuliko kula kwa jasho, ila pamaja na hayo God is good.