Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 4,952
- 4,326
Ingalikuwa rahisi, gonjwa hili la corona tungaliweza kulitokomeza (cut the transmission chain) kwa kupima watu wote nchini na duniani kwa siku moja kwa mtindo wa nyumba hadi nyumba. Na nyumba zitakazopatikana zina mtu positive zikawekwa lockdown au self isolation papo hapo kwa siku 14, tungalifanikiwa sana kulitokomeza gonjwa hili ndani ya siku 14 tu kwa kukata mnyororo wake wa usambazaji.
Jambo kama hilo si rahisi na haliwezekani. Kwa mfano gharama tu ya kipimo kimoja ni Tsh 120,000/. Watanzania tuko millioni 60. Hivyo gharama ya kipimo ni:
Shs 60,000,000 × 120,000 = Tsh 7,200,000,000,000/ = Trillion 7.2 Shs.
Hapo hujaweka gharama za logistics zingine za kufanya zoezi hilo nchi nzima ndani ya siku moja na mambo mengine mengi. Hizi ukizijumlisha ni zaidi ya bajeti yetu ya mwaka mmoja. Hata hizo nchi zilizoendelea haziwezi kumudu kitu kama hicho.
Hivyo mbinu hiyo haiwezekani. Mbinu nyingine effective ni ku lockdown watu wote kwa siku 14 kwa mara moja duniani kote. Yaani watu wote duniani kwa muda mmoja wakaji lockdown kwa siku 14. Watu wote hakuna cha exemption: uwe mtumishi wa afya, askari wa jeshi lo lote na kadhalika wote lockdown.
Kifedha mbinu hii inaweza kuwa rahisi ukilinganisha na mbinu ya kwanza lakini matokeo yake ni janga (disaster) kubwa zaidi kuliko hiyo ya corona. Watu wengi watakufa kwa magonjwa mengine na njaa, mifugo yote itakufa kwani wachungaji wake watakuwa lockdown, mazao yote ya kilimo yatakufa kwani wakulima wake watakuwa lockdown na kadhalika. Itakuwa balaa lisilokipimo.
Hivyo mbinu hizo zote ambazo ndizo madhubuti kuvunja mnyororo wa usambazaji wa mdudu huyu haziwezekani. Ndiyo maana kinachofanyika ni part messures tu ambazo zinawezekana kwenye nchi husika bila kusababisha madhara zaidi kwa binadamu na viumbe vingine. Tufuate wanachotushauri wataalamu wa nchi yetu na tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu!
Jambo kama hilo si rahisi na haliwezekani. Kwa mfano gharama tu ya kipimo kimoja ni Tsh 120,000/. Watanzania tuko millioni 60. Hivyo gharama ya kipimo ni:
Shs 60,000,000 × 120,000 = Tsh 7,200,000,000,000/ = Trillion 7.2 Shs.
Hapo hujaweka gharama za logistics zingine za kufanya zoezi hilo nchi nzima ndani ya siku moja na mambo mengine mengi. Hizi ukizijumlisha ni zaidi ya bajeti yetu ya mwaka mmoja. Hata hizo nchi zilizoendelea haziwezi kumudu kitu kama hicho.
Hivyo mbinu hiyo haiwezekani. Mbinu nyingine effective ni ku lockdown watu wote kwa siku 14 kwa mara moja duniani kote. Yaani watu wote duniani kwa muda mmoja wakaji lockdown kwa siku 14. Watu wote hakuna cha exemption: uwe mtumishi wa afya, askari wa jeshi lo lote na kadhalika wote lockdown.
Kifedha mbinu hii inaweza kuwa rahisi ukilinganisha na mbinu ya kwanza lakini matokeo yake ni janga (disaster) kubwa zaidi kuliko hiyo ya corona. Watu wengi watakufa kwa magonjwa mengine na njaa, mifugo yote itakufa kwani wachungaji wake watakuwa lockdown, mazao yote ya kilimo yatakufa kwani wakulima wake watakuwa lockdown na kadhalika. Itakuwa balaa lisilokipimo.
Hivyo mbinu hizo zote ambazo ndizo madhubuti kuvunja mnyororo wa usambazaji wa mdudu huyu haziwezekani. Ndiyo maana kinachofanyika ni part messures tu ambazo zinawezekana kwenye nchi husika bila kusababisha madhara zaidi kwa binadamu na viumbe vingine. Tufuate wanachotushauri wataalamu wa nchi yetu na tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu!