Independence without freedom is meaningless.

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Tulipokuwa tunadai uhuru hatukudai uhuru ili tujengewe reli, kama ni reli wajerumani walijenga, hatukudai uhuru ili tujengewe shule kama ni shule wakoloni na wamishonari walijenga, hatukudai uhuru ili tujengewe viwanja vya ndege, hatukudai wakoloni waondoke ili tujenge hospitali.

Tulichokuwa tunadai ni Uhuru wa kujiamulia mambo yetu wenyewe bila kuingilia na mkoloni, uhuru wa kukusanyika, uhuru wa kujieleza bila kupangiwa cha kusema, tulidai uhuru wa kiuchumi kila mtu awe huru kufanya biashara, kulima, kuuza na kununua, uhuru wa kupanga na kuchagua viongozi wetu wenyewe.

Serikali imeshindwa kusimamia uhuru kamili (total independence) tuliokuwa tunadai, uhuru tulioupata tarehe 9 December 1961 umeporwa na dola, serikali imekuwa kama ndiyo mkoloni mpya, inawapangia watu cha kusema, imeua uhuru wa vyombo vya habari, imezuia vyama vya siasa kukutana, inaingilia biashara za wananchi wake, inawapangia wakulima bei na kuwalazimsha wauze wapi, haki za binadamu zinakiukwa na vyombo yenyewe vya dola.

Haya yanayofanywa na dola dhidi ya raia wake yanaharibu kabisa maana halisi ya Uhuru tuliodai na kuupata tarehe 9 December 1961. Kuna wengine wanafikia hatua wanasema 'Heri ya mkoloni mweupe kuliko mkoloni mweusi'.

Nawatakia sikukuu njema tunapoadhimisha Uhuru wa bendera.
 
Tulipokuwa tunadai uhuru hatukudai uhuru ili tujengewe reli, kama ni reli wajerumani walijenga, hatukudai uhuru ili tujengewe shule kama ni shule wakoloni na wamishonari walijenga, hatukudai uhuru ili tujengewe viwanja vya ndege, hatukudai wakoloni waondoke ili tujenge hospitali.

Tulichokuwa tunadai ni Uhuru wa kujiamulia mambo yetu wenyewe bila kuingilia na mkoloni, uhuru wa kukusanyika, uhuru wa kujieleza bila kupangiwa cha kusema, tulidai uhuru wa kiuchumi kila mtu awe huru kufanya biashara, kulima, kuuza na kununua, uhuru wa kupanga na kuchagua viongozi wetu wenyewe.

Serikali imeshindwa kusimamia uhuru kamili (total independence) tuliokuwa tunadai, uhuru tulioupata tarehe 1 December 1961 umeporwa na dola, serikali imekuwa kama ndiyo mkoloni mpya, inawapangia watu cha kusema, imeua uhuru wa vyombo vya habari, imezuia vyama vya siasa kukutana, inaingilia biashara za wananchi wake, inawapangia wakulima bei na kuwalazimsha wauze wapi, haki za binadamu zinakiukwa na vyombo yenyewe vya dola.

Haya yanayofanywa na dola dhidi ya raia wake yanaharibu kabisa maana halisi ya Uhuru tuliodai na kuupata tarehe 1 December 1961. Kuna wengine wanafikia hatua wanasema 'Heri ya mkoloni mweupe kuliko mkoloni mweusi'.

Nawatakia sikukuu njema tunapoadhimisha Uhuru wa bendera.
Cc wazazibari hatujapata uhuru bado
 
Kwahiyo barabara zisijengwe ... ila Kenya na Rwanda wakijenga mnafungua nyuzi na kupanda majukwaani kuwapongeza ila tz ikifanya maendeleo mnapinga ....
 
Hakika bado tuna mtihani kupata uhuru wa kweli , Tunahitaji Katiba bora.Ni aibu leo hii kama taifa huru tumemkasimu Majukumu makubwa sana MTU. Rejea mfano kauli yake karibuni kuhusu hitaji la Katiba,majibu simpo kibabe na Kiburi cha madaraka.
 
Kwahiyo barabara zisijengwe ... ila Kenya na Rwanda wakijenga mnafungua nyuzi na kupanda majukwaani kuwapongeza ila tz ikifanya maendeleo mnapinga ....
Kenya wana Uhuru mpana,kumbuka walipodai katiba mpya ilipatakana kwa njia ile waliyotumia,mikutano ya kisiasa inafanyika. Barbara reli zinajengwa na kodi za wananchi kupitia mamlaka zilizokasimiwa. KWA MAWAZO YAKO,UHURU UNANYIMA MAENDELEO YA NCHI? kama ndiyo basi wazee wetu walikosea kudai Uhuru kwa wakoloni. Daaah kwa mawazo haya tutafika tukiwa hoi.
 
Uhuru wanao wanaccm, wengine ni kupingwa risasi tu tena mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom