Dkt. Harrison Mwakyembe ajilipua suala la Ushoga; Kukabidhi jina la Mwenyekiti wao kitaifa na mikoa kwa Serikali

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,896
22,663
Waziri wa zamani wa wizara mbalimbali amesema kuna chama la mashoga hapa Tanzania na wana uongozi wao wa kitaifa na kimataifa, kimkoa na kiwilaya atawataja na kukabidhi majina yao kwa mamlaka husika ili wachukue hatua.

Amesema anayo majina yao wote namba zao za simu na washirika wao wote

USSR

----
Mashoga wana mkurugenzi mkuu wao kabisa wa kuendeleza masuala ya ushoga Tanzania, jina lake ninalo na hata namba yake pia, nitawasilisha serikalini. Pia kuna wenyeviti wa mikoa na mtandao wa ufuatiliaji hadi vijijini

Kuna wahamasishaji wa masuala ya ushoga ngazi ya kanda, ninayo orodha ya majina yao pamoja na namba zao za simu. Na wahamasishaji hawa wapo kwa miaka mingi tu, naomba mtambue ndugu zangu hali ni mbaya sana

Kuna dodoso maalum la masuala ya ushoga ambalo ukilijaza linapelekwa Marekani, na pia kuna mwongozo maalum wa mafunzo ya mabadiliko ya tabia na mawasiliano ya wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao, mwongozo huo upo

Na tumekaa na vijana ambao ni mashoga, niwaambie tu wanatamani kabisa kurudi katika hali ya zamani, ukimuuliza aliingiaje, mwingine anakwambia nilianza kidogo kidogo darasa la tatu hata sijui niliingiaje, na natamani kurudi. Ukimsikiliza machozi yanataka kutoka

"Sheria yetu ya kudhibiti ushoga inahitaji marekebisho, inapaswa kuwa na meno ya kutosha na kung'ata. Mfano kwa msagaji adhabu yake ni kati ya mwaka mmoja na miaka mitano jela au faini kati ya shilingi laki moja na laki tatu, na sheria hii inaangalia zaidi kufanyika kwa tendo, kuna umuhimu ikaangalia na mazingira ya kupelekea jinai hiyo kufanyika, na mara nyingi anakamatwa shoga lakini baasha hakamatwi

Kwa kufuru,upuuzi, uchafu na uasi na ushetani unaoufanywa na wanadamu hapa duniani, unafanya yaliyofanywa na Sodoma na Gomora kuwa 'cha mtoto

Kule Marekani, watoto wa miaka 5-7 wanafundishwa kwamba, umezaliwa na sehemu za siri za kiume lakini ukijisikia na ukipenda, unaweza ukaamua kuendelea kuwa mwanaume au la, na unaweza ukaoa mwanaume au mwanamke


Mwaka 2016 Serikali yetu ilimfukuza mwakilishi wa Mfuko wa Ukimwi wa Rais wa Marekani alituharibia watoto wetu sana, lakini sasa kuna mwanaume mwingine kutoka Marekani yupo hapa Dar es Salaam anatuharibia watoto wa kiume, na taarifa zake tumeshaziwasilisha polisi

Chanzo: Jambo TV

 
Back
Top Bottom