Inawezekana Rais Magufuli amesaini ule mkataba wa ushirikiano na mataifa ya Ulaya (EPA)?

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wanajamvi,

Kuna habari zimekuwepo kuhusu nchi za EU kuanza kutoa misaada mara baada ya nchi hizo kusimamisha misaada hiyo kwasababu ya ukosekanaji wa demokrasia nchini. Lakini kuna makala moja nimekutana nayo ambapo inaonyesha Mh. Rais ameshaanza kubadili msimamo kuhusiana na mkataba huo wa ushirikiano wa kibiashara na mataifa ya Ulaya, ama “Economic Partnership Agreement”(EPA). Mkataba ambao mwanzoni rais alisema ni wa kinyonyaji na kikoloni. Na ukapingwa vikali hadi bungeni.

Mkataba huu ulipoletwa mwanzoni, Magufuli aliuita kuwa ni “mkataba wa kikoloni”, kwasababu unaenda tofauti na malengo ya serikali yake ya viwanda. Na bunge lilifuatia kwa kuupigia kura ya “Hapana”. Point yao ikiwa ni kwamba hatuwaweza kufanikisha sera ya viwanda kwasababu hatuwezi kushindana nao, na pia tunategemea kodi za mapato kutokana na bidhaa zinazoingizwa kutoka kwenye mataifa hayo.

Rais Magufuli aliuponda sana mkataba huo mbele ya rais Museveni wa Uganda. Mkataba huo ni wa kuondoa ushuru kwenye bidhaa baina ya mataifa hayo ya Africa na Europe.

Hadi kufikia mwaka jana, Rwanda na Kenya tayari walikwisha usaini mkataba huo. Mkataba huu ulitakiwa usainiwe na mataifa yote ya EAC. Baadhi walisaini na baadhi hawakusaini tukiwemo sisi, Uganda na Burundi.

Kwenye makala hii, mwandishi anaonesha kuwepo na uhusiano kati ya serikali kuonyesha dalili za kubadili msimamo kwenye mkataba be serikali kunyimwa msaada na mataifa hayo kwa kukandamiza demokrasia.

Sasa nilikuwa nikijiuliza ni kipi kimefanyika wakabadili mawazo? Ndipo nikakutana na hii.
The European Commission is close to invoking Article 96 of the Cotonou Agreement and cutting off all financial support and political relations with the Tanzania government, EURACTIV understands. The EU’s ambassador Roeland Van de Geer was expelled from Tanzania in November after raising concerns about democratic freedoms and human rights.

‘He (Magufuli) has managed to completely destroy relations between the EU and Tanzania. The mood upstairs [in the Commission] is very ugly,’ one Brussels official told EURACTIV.

Several EU countries, including Denmark, Sweden and Belgium, have already cancelled bilateral aid programmes worth around €50 million, but invoking Article 96 would strike down the €100 million the Commission gives Tanzania in budgetary support each year.

In signs of a new rapprochement in recent weeks, Magufuli’s office released photographs in early February of the Tanzanian president meeting with Van de Geer’s successor, Charles Stuart.

But Brussels is still waiting for substantive negotiations on the EPA to re-start. There are also few signs that Tanzania is opening up its trade policy. At the Trade Policy Review of the East African Community on 20 March, the EU noted that Tanzania and Burundi had failed to ratify the WTO Agreement on Trade Facilitation.

Kwa kifupi, mwandishi anaonyesha uwezekano wa “quid pro quo”, yani mkataba unasainiwa na vikwazo vinaondolewa bila kujali kama sababu zilizofanya vikwazo hivyo vikawekwa zimekwisha kufanyiwa kazi!

Je, hapa tunajifunza nini? Je, kuna kingine ambacho Magufuli akiwapa basi watafumbia macho yote waliyokuwa wakiyakodolea mimacho hapo mwanzoni? Mfano uminywaji wa demokrasia?
 
Mwandishi anadai maofisa wa EU walishtushwa na uamuzi wa Maghufuli kubadili mawazo na kutaka kuusaini huo mkataba. Mwanzoni nilijiuliza nini kimebadilika kwenye mkataba huo? Kwasababu Maghufuli aliwahi kuuita ni “mkataba wa kikoloni”

An Economic Partnership Agreement (EPA) between the EU and six East African countries has been stuck for several years. When President John Magufuli’s Tanzanian government suddenly announced it was reviewing its position on the EPA with a view to endorsing it, EU officials were taken aback.
 
Gazeti la Business Daily nalo linasema kuwa serikali inachukuwa hatua za kutaka kusaini mkataba huu a kikoloni ili kujaribu kukarabati mahusiano yaliyokuwa yameharibiwa na matendo yasiyo ya kidemokrasia. Serikali ilikuwa imeharibu mahusiano na EU hadi balozi wao kurudishwa kwasababu ya ukosekanaji wa demokrasia Tanzania.

Fresh review
According to sources, the government may have relaxed its earlier stance on EPA as a means to repair its soured diplomatic relations with the EU, which saw the Brussels-based body announce a fresh review of its diplomatic and economic engagement with Tanzania.
 
Yaan wewe jibu ushatoa kuwa sababu ni kuondelewa vikwazo

Alafu hapo hapo bado tena unatuuliza tena sisi sababu
Hakuna mbabe mbele ya mbeberu hayo majamaa yana uwezo wa kukushushia wahyi ukabaki unashangaa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapa umemix madesa. Nitasema sababu ni kuondolewa vikwazo kama atakuwa ameshaini huo mkataba.

Sababu zilizotolewa na waandishi hao zinahusishwa na serikali kuonyesha nia ya kutaka kusaini mkataba huo.

Nimeuliza tu kama umeshasainiwa maana kina MsemajiUkweli, Pascal Mayalla na YEHODAYA walileta habari za misaada kutolewa. Unachokiwa ni maoni mkuu na si maneno ya kwenye kanga!
 
Maana naona hata beberu la Economist inasemekana linaisifia ccm na serikali yake!😂 Kabendera naye ni a victim of circumstances.
 
Mwandishi anadai maofisa wa EU walishtushwa na uamuzi wa Maghufuli kubadili mawazo na kutaka kuusaini huo mkataba. Mwanzoni nilijiuliza nini kimebadilika kwenye mkataba huo? Kwasababu Maghufuli aliwahi kuuita ni “mkataba wa kikoloni”
Hizo setenso za kiingereza zinamaanisha ulivyoandika kiswahili?
 
Mkuu elewa kuwa tajiri hadhihakiwi na hakuna siku mkate utakuwa mgumu mbele ya chai jmushi1,

In God we Trust
 
Hakuna mwenye njaa anayeweza kushindana na mwenye shibe
Mwandishi anadai maofisa wa EU walishtushwa na uamuzi wa Maghufuli kubadili mawazo na kutaka kuusaini huo mkataba. Mwanzoni nilijiuliza nini kimebadilika kwenye mkataba huo? Kwasababu Maghufuli aliwahi kuuita ni “mkataba wa kikoloni”


In God we Trust
 
Kwanza habari quoted ni ya march mwaka jana.

So the hypothesis enumerated above could safely be nullified. In relation to EPA agreement, will surely be signed be it sooner or later.

Swala la EU ku-release mshiko, nafikiri EU wako kwenye competition na UK/US.
 
Hizo setenso za kiingereza zinamaanisha ulivyoandika kiswahili?
Ndiyo, zinamaanisha hivyo.

“Taken aback” ni kushtushwa na kushangazwa.

“to be taken aback. phrase. If you are taken aback by something, you are surprised or shocked by it and you cannot respond at once. Roland was taken aback by our strength of feeling.”-Collins Dictionary
 
Kwanza habari quoted ni ya march mwaka jana.

So the hypothesis enumerated above could safely be nullified. In relation to EPA agreement, will surely be signed be it sooner or later.

Swala la EU ku-release mshiko, nafikiri EU wako kwenye competition na UK/US.
Sasa ndo umeandika kitu gani?
 
Kwa hiyo akisaini mkataba wa EPA hata hoja za demokrasia zitaisha!

Maelezo yako yanaonyesha kumbe tatizo halikuwa suala la demokrasia bali Mkataba wa EPA!

Tukisema hizi kelele za EU na USA kudai demokrasia ni kibwagizo tu kwa sababu maslahi yao yamezibwa tutakuwa tunakosea!


Sent from my iPhone
 
Mkuu hapa umemix madesa. Nitasema sababu ni kuondolewa vikwazo kama atakuwa ameshaini huo mkataba.

Sababu zilizotolewa na waandishi hao zinahusishwa na serikali kuonyesha nia ya kutaka kusaini mkataba huo.

Nimeuliza tu kama umeshasainiwa maana kina MsemajiUkweli, Pascal Mayalla na YEHODAYA walileta habari za misaada kutolewa. Unachokiwa ni maoni mkuu na si maneno ya kwenye kanga!
Dah! Ndugu kumbe nilikukwaza tena?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo akisaini mkataba wa EPA hata hoja za demokrasia zitaisha!

Maelezo yako yanaonyesha kumbe tatizo halikuwa suala la demokrasia bali Mkataba wa EPA!

Tukisema hizi kelele za EU na USA kudai demokrasia ni kibwagizo tu kwa sababu maslahi yao yamezibwa tutakuwa tunakosea!


Sent from my iPhone
Sawa mkuu. Maslahi ya Taifa yamezingatiwa? Au unazungumzia kukaa madarakani kwa gharama yoyote? Vipi kuhusu viwanda?
 
Kwa hiyo akisaini mkataba wa EPA hata hoja za demokrasia zitaisha!

Maelezo yako yanaonyesha kumbe tatizo halikuwa suala la demokrasia bali Mkataba wa EPA!

Tukisema hizi kelele za EU na USA kudai demokrasia ni kibwagizo tu kwa sababu maslahi yao yamezibwa tutakuwa tunakosea!


Sent from my iPhone
Na aliyeita mkataba wa kikoloni kisha akaja kuusaini tusemeje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom