Inawezekana matatizo ya nchi ni makubwa kuliko tunavyodhani: Immanuel Didas, apasuliwa kichwa badala ya mguu MOI

..taratiibu ukweli utafahamika!kwamba routine haikufuatwa ipasavyo,kwa uzembe tu!au kwa hujuma?

..hii itafanya taratibu zote za kuhudumia wagonjwa,hasa huduma wanazotoa ma-nurse kuwa reviewed!na hapa tuombee zitakosolewa na kusahihishwa!

..ilikuwa inangojwa ajali ili MOI irekebishwe!sasa ndio hiyoooo!
 
Hivi huyu aliyekosewa operation ndio mahakama kuu juzi imeamuru alipwe milioni 100 Kama fidia?!
 
Hii ni another issue of medical negligence na waathirika wa hii mix-up wana chance nzuri ya kuagana na umasikini kama watapata solicitor mzuri na kufile claim. Si mtaalamu sana kwenye mambo ya sheria lakini ni wazi kwamba these guys are entitled to compesation kwa maumivu waliyoyapata, gharama za matibabu (if any), loss of income kwa muda wote ambao wameshindwa au watashindwa kujiingizia kipato cha kujikimu wao pamoja na familia zao.
Kwa upande wa madaktari waliohusika na uzembe huu,sina hakika kama kuna chombo ambacho kina monitor standards za utendaji wao hapo nyumbani. Normally kwenye nchi za wenzetu zilizoendelea wangeitwa mbele ya chombo hicho for a discpilinary hearing, depending on jinsi watakavyojitetea mbele ya chombo hicho na uzito wa kosa lenyewe- outcome inaweza kuwa warning, suspension au kuwa struck off kama ni gross misconduct.
Sidhani kama its the right decision kaka Kitila kuanzisha petition hapa ili kuwafukuza hawa madaktari. Kwanza this is a very unsual scenario, something that doesnt happen everyday na naona ni vizuri wakapewa nafasi wajieleze, they didnt do this on purpose I believe and these things happen all over the world (soma hizo story mbili hapo chini ujionee mwenyewe).


GMC CLEARS GYNAECOLOGIST WHO MISTREATED WOMAN WITH STOMACH PAINS


Dr May Mammo was working as a consultant obstetrician and gynaecologist at Bassetlaw Hospital in Worksop when a woman in his care died following a hysterectomy operation.

He denied misconduct. At a GMC fitness to practice hearing this week he was cleared of the charge.

The hearing had heard that Mammo should not have carried out the inappropriate treatment
and should have considered alternative treatments.

The woman had the surgery after suffering from stomach pains.

She died following surgery at Bassetlaw Hospital in 2001.

In actual fact the stomach pains had probably been caused by fibroids and HRT.

Mammo's failure to diagnose accurately the cause of the patient's stomach pains led to him inappropriately treating her by operating unnecessarily.

The misdiagnosis led to a decision to perform a hysterectomy which was the cause of her death.

It is thought that the operation posed a risk to the patient because she suffered from angina and the operation would have put her at risk of heart attack.

The patient died the day after the operation from a suspected heart attack.


Mums Swap Back Babies That Were Mixed Up
Oct 10 2007 By Mark Ellis

Couples Raise Each Others' Kids As Theirs After Blunder Parents Were Handed Wrong Tots In Hospital

TWO mums given the wrong babies in a hospital mix-up are saying painful goodbyes to the little girls they have loved for 10 months.

Babies Nikola and Veronika will be reunited full-time with their biological mums just before Christmas.

Mums Jaroslava Trojanova and Jaroslava Cermakova, who gave birth just 18 minutes apart, met last week to plan the swap.

And they agreed to gradually spend more and more time together before the final handover.

The blunder only came to light when Miss Trojanova's partner Libor Broza was stung by workmates' jibes that blonde baby Nikola looked nothing like the couple, who are both dark.

To their shock, DNA tests revealed that Libor, 29, was not the father - and his 25-year-old partner was not her mother.

A fortnight later, they discovered their real daughter, Veronika, was living with Mrs Cermakova and her husband Jan in a village 20 miles away.

Both couples now plan to sue Trebic Hospital in Brno in the Czech Republic for &[HASHTAG]#163[/HASHTAG];250,000.

Lorry driver Libor said yesterday: "It was a total shock. I just cried for two hours solid and Jaroslava was inconsolable.

"We have raised Nikola for the past 10 months. She's a beautiful little girl who's always smiling and it's impossible to imagine her now living apart from us.

"But at the same time just 20 miles away lives our real daughter."

He added: "We have missed so many milestones in Veronika's life - her first teeth and her first steps.

"Now we are determined not to miss her first birthday and her first Christmas."

The girls were born on December 9 last year and both sets of parents were puzzled when they were weighed the following day.

Nikola weighed less than 6lb, compared with a birth weight of more than 7lb, and Veronika appeared to have put on 1.65lb overnight.

But staff reassured the parents the birth weights must have been recorded wrongly.

The Cermakovas say photos show Veronika was tagged with just a number.

Miss Trojanova, who is still breast-feeding Nikola, said: "Nikola is my little angel and so far I don't have any feelings for Veronika. I wish I could live with both of them."

Libor explained he secretly had a DNA test which revealed he was not Nikola's father.

When he confronted his partner, she insisted he must be the father and had a DNA test herself, which revealed the shocking truth.

The hospital has declined to comment publicly but its director Petr Mayer this week delivered a written apology to the couples.
I like ur Thread Mkuu umeongea nondo za maaana!!
 
Mkuu unaikumbuka hii
tapatalk_1559191531971.jpeg
 
Mimi nafikiri matatizo ya nchi yetu ni makubwa kuliko tunavyofikiria. Yapo kila kona, si tu katika siasa. Kama daktari anaweza akamfanyia mtu upasuaji wa kichwa badala ya mguu, hivi jamani utasema hapo ni siasa tena? Very confusing! Hii dhana ya uwajiikaji itafika siku tutaielewa kweli katika nchi yetu? Yaani watu wamefanya kosa kama hili lakini bado Mkurugenzi yupo, wale madaktari wanaendelea na udaktari wao hivyohivyo!


Naomba wale wenye utaalamu wa mambo ya petition tuanzishe petition ya kutaka uongozi wa MOI na hawa madaktari waondoke haraka sana. Yes, this is more than ile issue ya Ukraine! Hebu na nyie someni hii habari, tafakari, usilie bali pendekeza hatua za kuchukua!

Aliyeumia mguu apasuliwa kichwa, wa kichwa apasuliwa mguu.
Na Jackson Odoyo


WAGONJWA wawili waliokuwa wamelazwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) Muhimbili wamefanyiwa upasuaji tofauti na matatizo yaliyokuwa yakiwasumbua.


Wagonjwa hao walifanyiwa upasuaji Novemba Mosi, mwaka huu kwa nyakati tofauti katika taasisi hiyo, ambapo aliyekuwa na matatizo ya mguu alipasuliwa kichwa na wa kichwa akapasuliwa mguu.


Mmoja wa wagonjwa hao Immanuel Didas, aliyeumia goti baada ya kupata ajali ya pikipiki hivi karibuni na kulazwa katika taasisi hiyo, alifanyiwa uchunguzi na madaktari kushauri kwamba afanyiwe upasuaji wa goti hilo.


Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakati wa kumpatia huduma hiyo, madaktari waliohusika walimfanyia upasuaji wa kichwa badala ya goti.


Katika kile kinachoonekana kuchanganyikiwa kwa madaktari hao, mgonjwa mwingine, Immanuel Mgaya ambaye pia alilazwa MOI kwa matatizo ya kichwa na uchunguzi kubaini kuwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa, badala yake alifanyiwa upasuaji wa mguu.


Mwandishi wa Mwananchi alizungumza na ndugu wa wagonjwa hao kuhusiana na matatizo yaliyowafika ndugu zao wakati wanapatiwa huduma ya matibabu katika taasisi ambayo waliweka bayana magonywa yaliyokuwa yanawasumbua, lakini wakapata mshangao baada ya kutibiwa tofauti na matatizo yao.


Kaka wa Immanuel Didas, Sisti Marishay alisema mgonjwa wake alikwenda hospitalini hapo kwa matatizo ya goti baada ya kupata ajali ya pikipiki, lakini alipopigwa picha za x-ray hakuwa na matatizo katika mfupa ila kulikuwa na uvimbe kwa ndani ndipo madaktari wakashauri afanyiwe upasuaji ili kuuondoa.


Alisema katika hali ya kusikitisha madaktari hao walimfanyia upasuaji kichwani wakati alikuwa haumwi kichwa.


"Kilicho fanyika ni uzembe wa hali ya juu, kwa sababu mdogo wangu alikuwa anaumwa mguu na sio kichwa, wao wakamfanyia upasuaji wa kichwa na baada ya kutokea tatizo hilo, nilizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Profesa Laurent Museru ambaye alikiri kwamba kuna makosa yametokea hivyo wameamua kukaa na kuunda tume ya kuchunguza uzembe huo kisha watatoa taarifa baada ya wiki moja," alisema Marishay.


Marishay alisema kwa sasa hawawezi kuchukua hatua yoyote mpaka watakapo pata majibu ya tume iliyoundwa na taasisi hiyo kuchunguza suala hilo.


Ndugu mwingine wa Didas, Ludani Didas naye alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia uzembe huo uliofanywa na madaktari hao kwa sababu mpaka sasa mdogo wake amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).


"Mpaka dakika hii mdogo wangu hajitambui, hawezi kuzungumza chochote na yuko ICU, sasa mimi nitazungumza kitu gani, tusubiri nione hatima ya afya yake ndipo nitazungumzia uzembe huu wa wazi kabisa tena kwa wanyonge," alilalamika.


Naye mama mzazi wa Immanuel Mgaya aliyefanyiwa upasuaji wa mguu badala ya kichwa, Mary Mgina akiwa kwenye Wodi na 17, Sewahaji alimolazwa kijana wake, alisema alifika hospitalini hapo akitokea Njombe, mkoani Iringa wiki iliyopita.


"Tulikuja wiki iliyopita tukitokea Njombe katika Hospitali ya Kibena ambapo walituandikia barua kuja hapa kwa matibabu zaidi ya kichwa kilichoanza kumuuma ghafla siku chache baada ya kuanza mitihani ya kidato cha nne akiwa kwenye chumba cha mtihani," alisema Magina.


Alisema kutokana na tatizo hilo alishindwa kuendelea na mitihani kutokana na kuendelea kuumwa kichwa huku akianguka na kupoteza fahamu, ndipo akahamishiwa MOI ambako baada ya kumchunguza waliamua apasuliwe kichwa ila hawakumweleza ugonjwa unaomsumbua," alisema mama huyo.


Mjomba wa Mgaya, Dick Magina alisema baada ya kufanyiwa upasuaji huo walikabidhiwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa, lakini hakuwa ndugu yao na walipomkataa walianza kumtafuta na walipompata wakakuta amefanyiwa upasuaji wa mguu na si kichwa.


"Walinikabidhi mgonjwa mwingine tofauti na ndugu yangu nikawakatalia ndipo wakaanza kumtafuta na kumpata akiwa amepasuliwa mguu. Kilicho nishangaza zaidi ni kwamba tangu walipogundua kwamba wamefanya makosa hayo hawajafika kumuona mgonjwa ili wajue anaendeleaje," alisema Mgina na kuongeza;


"Kutokana na uzembe huo uliofanyika tunahitaji matibabu kwa mgonjwa wetu tena kwa gharama zao, pia nimehuzunishwa sana kutokana na makosa yaliyofanyika na hasa kwa wenzetu ambao mgonjwa wao amefanyiwa upasuaji wa kichwa badala ya mguu na hali yake ni mbaya," alisema.


Baadhi ya madaktari na wauguzi wa Muhimbili waliozungumza na mwandishi wa Mwananchi kwa njia ya simu kwa nyakati tofauti jana kwa masharti ya kutoandikwa majina yao gazetini, walidai kuwa uzembe kama huo ni wa kawaida hospitalini hapo.


Walidai kuwa madaktari wengine baada ya upasuaji wanaacha vipande vya pamba, nyembe na hata mikasi ndani ya mwili wa mgonjwa, lakini hufanywa kwa siri na mgonjwa anapofanyiwa upasuaji upya huwa haambiwi sababu ya kumpasua tena.


Baadhi ya wogonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo walidai kuwa uzembe kama huo ni wa kawaida kufanyika hospitalini hapo na kudokeza kwamba, hata akina mama wanaojifungua wengine hupewa watoto ambao si wao na wengine huambiwa uwongo kwamba mtoto amefariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.


Naye Profesa Museru alikiri kuwepo kwa madai hayo na kusema kwamba, amesikitishwa na tukio hilo na kwamba aliamua kufikisha taarifa hizo wizarani.


Profesa Museru alisema pia wameunda tume ya kuchunguza madai hayo ambayo itaanza kazi leo na kutoa majibu kesho kutwa.


"Ni kweli kuna tukio la aina hiyo hapa hospitalini, lakini kuna taratibu nimeanza kuzichukuwa na sasa hivi ninapozungumza nawe nipo kwenye kikao cha kuunda tume ya kufuatilia na siwezi kukiri au kukataa kuwa ni uzembe, ndiyo maana tunaunda tume ya kuchunguza suala hilo na pia nimeishapeleka taarifa wizarani," alisema Profesa Museru.
Nakusalimu mleta uzi Profesa wangu.
 
Mimi nafikiri matatizo ya nchi yetu ni makubwa kuliko tunavyofikiria. Yapo kila kona, si tu katika siasa. Kama daktari anaweza akamfanyia mtu upasuaji wa kichwa badala ya mguu, hivi jamani utasema hapo ni siasa tena? Very confusing! Hii dhana ya uwajiikaji itafika siku tutaielewa kweli katika nchi yetu? Yaani watu wamefanya kosa kama hili lakini bado Mkurugenzi yupo, wale madaktari wanaendelea na udaktari wao hivyohivyo!


Naomba wale wenye utaalamu wa mambo ya petition tuanzishe petition ya kutaka uongozi wa MOI na hawa madaktari waondoke haraka sana. Yes, this is more than ile issue ya Ukraine! Hebu na nyie someni hii habari, tafakari, usilie bali pendekeza hatua za kuchukua!

Aliyeumia mguu apasuliwa kichwa, wa kichwa apasuliwa mguu.
Na Jackson Odoyo


WAGONJWA wawili waliokuwa wamelazwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) Muhimbili wamefanyiwa upasuaji tofauti na matatizo yaliyokuwa yakiwasumbua.


Wagonjwa hao walifanyiwa upasuaji Novemba Mosi, mwaka huu kwa nyakati tofauti katika taasisi hiyo, ambapo aliyekuwa na matatizo ya mguu alipasuliwa kichwa na wa kichwa akapasuliwa mguu.


Mmoja wa wagonjwa hao Immanuel Didas, aliyeumia goti baada ya kupata ajali ya pikipiki hivi karibuni na kulazwa katika taasisi hiyo, alifanyiwa uchunguzi na madaktari kushauri kwamba afanyiwe upasuaji wa goti hilo.


Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakati wa kumpatia huduma hiyo, madaktari waliohusika walimfanyia upasuaji wa kichwa badala ya goti.


Katika kile kinachoonekana kuchanganyikiwa kwa madaktari hao, mgonjwa mwingine, Immanuel Mgaya ambaye pia alilazwa MOI kwa matatizo ya kichwa na uchunguzi kubaini kuwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa, badala yake alifanyiwa upasuaji wa mguu.


Mwandishi wa Mwananchi alizungumza na ndugu wa wagonjwa hao kuhusiana na matatizo yaliyowafika ndugu zao wakati wanapatiwa huduma ya matibabu katika taasisi ambayo waliweka bayana magonywa yaliyokuwa yanawasumbua, lakini wakapata mshangao baada ya kutibiwa tofauti na matatizo yao.


Kaka wa Immanuel Didas, Sisti Marishay alisema mgonjwa wake alikwenda hospitalini hapo kwa matatizo ya goti baada ya kupata ajali ya pikipiki, lakini alipopigwa picha za x-ray hakuwa na matatizo katika mfupa ila kulikuwa na uvimbe kwa ndani ndipo madaktari wakashauri afanyiwe upasuaji ili kuuondoa.


Alisema katika hali ya kusikitisha madaktari hao walimfanyia upasuaji kichwani wakati alikuwa haumwi kichwa.


"Kilicho fanyika ni uzembe wa hali ya juu, kwa sababu mdogo wangu alikuwa anaumwa mguu na sio kichwa, wao wakamfanyia upasuaji wa kichwa na baada ya kutokea tatizo hilo, nilizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Profesa Laurent Museru ambaye alikiri kwamba kuna makosa yametokea hivyo wameamua kukaa na kuunda tume ya kuchunguza uzembe huo kisha watatoa taarifa baada ya wiki moja," alisema Marishay.


Marishay alisema kwa sasa hawawezi kuchukua hatua yoyote mpaka watakapo pata majibu ya tume iliyoundwa na taasisi hiyo kuchunguza suala hilo.


Ndugu mwingine wa Didas, Ludani Didas naye alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia uzembe huo uliofanywa na madaktari hao kwa sababu mpaka sasa mdogo wake amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).


"Mpaka dakika hii mdogo wangu hajitambui, hawezi kuzungumza chochote na yuko ICU, sasa mimi nitazungumza kitu gani, tusubiri nione hatima ya afya yake ndipo nitazungumzia uzembe huu wa wazi kabisa tena kwa wanyonge," alilalamika.


Naye mama mzazi wa Immanuel Mgaya aliyefanyiwa upasuaji wa mguu badala ya kichwa, Mary Mgina akiwa kwenye Wodi na 17, Sewahaji alimolazwa kijana wake, alisema alifika hospitalini hapo akitokea Njombe, mkoani Iringa wiki iliyopita.


"Tulikuja wiki iliyopita tukitokea Njombe katika Hospitali ya Kibena ambapo walituandikia barua kuja hapa kwa matibabu zaidi ya kichwa kilichoanza kumuuma ghafla siku chache baada ya kuanza mitihani ya kidato cha nne akiwa kwenye chumba cha mtihani," alisema Magina.


Alisema kutokana na tatizo hilo alishindwa kuendelea na mitihani kutokana na kuendelea kuumwa kichwa huku akianguka na kupoteza fahamu, ndipo akahamishiwa MOI ambako baada ya kumchunguza waliamua apasuliwe kichwa ila hawakumweleza ugonjwa unaomsumbua," alisema mama huyo.


Mjomba wa Mgaya, Dick Magina alisema baada ya kufanyiwa upasuaji huo walikabidhiwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa, lakini hakuwa ndugu yao na walipomkataa walianza kumtafuta na walipompata wakakuta amefanyiwa upasuaji wa mguu na si kichwa.


"Walinikabidhi mgonjwa mwingine tofauti na ndugu yangu nikawakatalia ndipo wakaanza kumtafuta na kumpata akiwa amepasuliwa mguu. Kilicho nishangaza zaidi ni kwamba tangu walipogundua kwamba wamefanya makosa hayo hawajafika kumuona mgonjwa ili wajue anaendeleaje," alisema Mgina na kuongeza;


"Kutokana na uzembe huo uliofanyika tunahitaji matibabu kwa mgonjwa wetu tena kwa gharama zao, pia nimehuzunishwa sana kutokana na makosa yaliyofanyika na hasa kwa wenzetu ambao mgonjwa wao amefanyiwa upasuaji wa kichwa badala ya mguu na hali yake ni mbaya," alisema.


Baadhi ya madaktari na wauguzi wa Muhimbili waliozungumza na mwandishi wa Mwananchi kwa njia ya simu kwa nyakati tofauti jana kwa masharti ya kutoandikwa majina yao gazetini, walidai kuwa uzembe kama huo ni wa kawaida hospitalini hapo.


Walidai kuwa madaktari wengine baada ya upasuaji wanaacha vipande vya pamba, nyembe na hata mikasi ndani ya mwili wa mgonjwa, lakini hufanywa kwa siri na mgonjwa anapofanyiwa upasuaji upya huwa haambiwi sababu ya kumpasua tena.


Baadhi ya wogonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo walidai kuwa uzembe kama huo ni wa kawaida kufanyika hospitalini hapo na kudokeza kwamba, hata akina mama wanaojifungua wengine hupewa watoto ambao si wao na wengine huambiwa uwongo kwamba mtoto amefariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.


Naye Profesa Museru alikiri kuwepo kwa madai hayo na kusema kwamba, amesikitishwa na tukio hilo na kwamba aliamua kufikisha taarifa hizo wizarani.


Profesa Museru alisema pia wameunda tume ya kuchunguza madai hayo ambayo itaanza kazi leo na kutoa majibu kesho kutwa.


"Ni kweli kuna tukio la aina hiyo hapa hospitalini, lakini kuna taratibu nimeanza kuzichukuwa na sasa hivi ninapozungumza nawe nipo kwenye kikao cha kuunda tume ya kufuatilia na siwezi kukiri au kukataa kuwa ni uzembe, ndiyo maana tunaunda tume ya kuchunguza suala hilo na pia nimeishapeleka taarifa wizarani," alisema Profesa Museru.
Only dictatorship regime can save this country.

The rise of dictatorship in the world after the first world world especially in Europe, was becaause the democratic rule failed to solve the problems facing the people.

And that's why people in those days saw the only way was to support the charismatic men like HITLER & Mussolini to solve their problems.
 
Back
Top Bottom