Baada ya utafiti nilioufanya,kwa kweli tunahitaji wapinzani tubadilike kumg'oa huyu jini CCM,tunahitaji kuunganisha nguvu za ziada, nimeangalia hivi vyama vyetu vya upinzani kwa kweli vimegawana maeneo,kwa mfano Cuf wanakubalika saana baadhi ya mikoa,na Chadema nao wanakubalika saana baadhi ya mikoa mengine,na kuna sababu nyingi zinazofanya hivi vyama kugawana maeneo,kwa mfano,moja ya sababu ni propaganda ya ccm inayofanywa kusingizia Cuf ni ya pemba na Uislam,na Chadema ni uchaga na Ukristo,kwa kweli ccm wamefanikiwa kwa hili,na wananchi wengi wamelipokea hili bila kujua athari zake,Hili lina Athari kubwa kwetu na ni faida kwa ccm ambapo wamefanikiwa kwa kitumia kitengo cha usalama kueneza hali hii,wamezigawa kura za wapinzani,Jamani tuamkeni,kwa nini isiwezekane kuunganisha nguvu ili hili dudu lipotee kabisa duniani? Bila ya kuwa kitu kimoja ni ngumu Kuing'oa ccm,kwani wanatumia pesa nyingi saana,askari woote wao,jeshi lipo nyuma yao,wana Usalama wa hali ya juu,hata wanafikia kushirikiana na baadhi ya mataifa makubwa kuhakikisha CCM inaendelea kubaki madarakani. Je itawezekana kuing'oa ccm bila kuwa kuunganisha nguvu zetu?