KWELI Inawezekana kushiriki tendo la ndoa na mtu mwenye VVU/UKIMWI bila kinga na usipate Maambukizi hayo

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kuna magonjwa mengi yanayosababisha upungufu wa Kinga mwilini ikiwemo maambukizi ya VVU.

Kumekuwa na mijadala mingi pamoja na tetesi zinazohitaji majibu ya kina kuhusu uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kutoka kwa mtu aliye athirika hasa ikihusisha ushiriki wa tendo la ndoa pasipo kutumia kinga hata kama ni mara moja tu.

08289B1B-AC79-4F6C-975E-77283B90B7FC.jpeg

Ukweli upoje na majibu ya kisayansi yanatoa picha gani? Baadhi hudai hauwezi kupata VVU/UKIMWI kwa kufanya tendo moja tu la ngono na muathirika pasipo kutumia kinga kwa kuwa maambukizi hayaji kirahisi hivyo kama tunavyodhani.
 
Tunachokijua
HIV ama Human Immunodeficiency Virus ni kirusi kinachoshambulia mfumo wa kinga mwili, ambacho baada kuishi mwilini kwa kipindi fulani kinaweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini (UKIMWI).

Virusi hawa wenye sifa ya RNA, hubeba aina 15 za protini pia huzungukwa na kuta mbili za mafuta. Hushambulia seli hai zenye vipokeo vya CD4 pekee, hubadilika mara kwa mara pamoja na kupoteza sifa ya kuishi kikiwa kwenye mazingira yasiyo rafiki.

Ili virusi viweze kuingia mwilini na kusababisha madhara huhitaji mambo matatu ya msingi-
  1. Damu au Majimaji ya mwili
  2. Kitendo hatarishi
  3. Upatikanaji wa moja kwa moja wa mishipa ya damu
Takwimu
Kwa kutumia rejea ya CDC, huu ndiyo wastani wa watu wanaopata maambukizi ya VVU/UKIMWI katika kila kundi la watu 10,000 wanaokuwa kwenye mazingira hatarishi kwa mara ya kwanza.
  • Watu 9250 kwa kupokea damu
  • Watu 63 kwa kushirikiana vitu vyenye ncha kali
  • Watu 138 kwa kushiriki tendo la ndoa kinyume cha maumbile
  • Watu 8 kwa kushiriki tendo la ndoa kwa njia ya kawaida
Kwa kuzingatia takwimu hizi za CDC, JamiiForums inatambua kuwa sio kila anayeshiriki tendo la ndoa na mtu mwenye VVU/UKIMWI pamoja na kujiingiza kwenye mazingira hatarishi kwa mara ya kwanza huambukizwa ugonjwa huu. Hata hivyo, takwimu hizi huongezeka ukubwa wake kadri mtu anavyokuwa anarudia kujiingiza mara kwa mara kwenye mazingira husika.

Uwepo wa maambukizi ya magonjwa ya zinaa, hatua ya maambukizi ya VVU/UKIMWI, idadi ya nakala za virusi (Viral load) pamoja na udhaifu wa kinga ya mwili ya mhusika huongeza uwezekano wa kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI.

Kondomu kama kinga
Kwa mujibu wa USAID, Matumizi ya kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya VVU kwa zaidi ya 90%. Ni muhimu kutumia njia hii ili kujilinda dhidi ya gonjwa hili hatari ambalo kwa mwaka 2021 pekee liliondoa uhai wa takriban watu 650,000 duniani.

Kwa kuwa ni ngumu kujua hali ya afya ya mtu kwa kumtazama hasa kwa kuzingatia idadi ya nakala za VVU pamoja na hatua ya ugonjwa kwa wahusika, pia ili kufuta kabisa nafasi ya kuugua ugonjwa huu, ni muhimu kujilinda kikamilifu pamoja na kuepuka mazingira yote hatarishi yanayoweza kufanya uambukizwe.

Aidha, ili kupunguza nafasi ya kuambukiza wengine, waathirika wa VVU wanapaswa kutumia dawa za kufubaza makali ya maambukizi ili kudhibiti utengenezwaji wa nakala mpya za virusi, pamoja na kuongezeka kwa ukubwa wa maambukizi. Wanaofikia kiwango cha chini kabisa cha nakala za VVU hukosa sifa ya kuambukiza wengine.

Usijaribu kushiriki ngono zembe kwa imani kuwa nafasi ya kuambukizwa VVU/UKIMWI ni ndogo. Tendo la mara moja linaweza kukufanya ukanasa kwenye mtego huo.
MADAI
Kuna magonjwa mengi yanayosababisha upungufu wa Kinga mwilini ikiwemo maambukizi ya VVU.

Kumekuwa na mijadala mingi pamoja na tetesi zinazohitaji majibu ya kina kuhusu uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kutoka kwa mtu aliye athirika hasa ikihusisha ushiriki wa tendo la ndoa pasipo kutumia kinga hata kama ni mara moja tu.

View attachment 2405505

Ukweli upoje na majibu ya kisayansi yanatoa picha gani? Baadhi hudai hauwezi kupata VVU/UKIMWI kwa kufanya tendo moja tu la ngono na muathirika pasipo kutumia kinga kwa kuwa maambukizi hayaji kirahisi hivyo kama tunavyodhani.

Hii inawezekana kabisa: kuna watu wako kwenye ndoa mmoja anao mmoja hana wanaitwa discordant couple.

Hii inawezekana kabisa ila jitahidi kumuandaa mwenzio ili maji ya uke yatoke ukishindwa tumia kilainishi ila pia kuna wadada maumbile yao ni makubwa kwa hivo mjamaa anateleza tu no friction.

Japo usichukulie poa tumia kondom ili uwe salama zaidi. Pia ningekupa ushuhuda ila tuache km unaweza nichek private ntakupa.
 
Kama mwathirika wa virusi vya ukimwi anatumia dawa na viral load iko chini ya 100 mpaka 0 na CD4 ikiwa ipo juu, hapo piga kavu kavu hakuna shida.

Lakini kwa uhakika zaidi vaa kondom kwa usahihi. VVU ni noma
 
Kama mwathirika wa virusi vya ukimwi anatumia dawa na viral load iko chini ya 100 mpaka 0 na CD4 ikiwa ipo juu, hapo piga kavu kavu hakuna shida.

Lakini kwa uhakika zaidi vaa kondom kwa usahihi. VVU ni noma
Condom zinafahamika matumizi yake si za kuhimiza.

Watu hapo wanataka uwaelekeze kupiga kavu kavu hata kwa waathirika wa vvu.

Utamfamu vipi huyo mwathirika kama viral load yake ipo chini ya mia mkiwa tayari mmevuliana nguo 'gest', ni kipimo gani kinatumika?
 
Condom zinafahamika matumizi yake si za kuhimiza.

Watu hapo wanataka uwaelekeze kupiga kavu kavu hata kwa waathirika wa vvu.

Utamfamu vipi huyo mwathirika kama viral load yake ipo chini ya mia mkiwa tayari mmevuliana nguo 'gest', ni kipimo gani kinatumika?
Kula kavu mzee haiwezekani tembea na kipimo ukikuta mzigo upo fresh wewe piga ingawa haina guarantee kwamba upo safe.The best option ni kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu au tumia kondom.Hali ni mbaya mzee
 
Kupata maambukizi ya VVU ni kama mikosi au balaa, Na pengine kuna baadhi ya Familia zimekumbwa na mkosi huu na Cha kushangaza kuna watu wanaweza sex na waathirika na wasiupate na we mwenzangu na Mimi ukaokota hata kijiwembe na ukaunasa kwa kujikata kwa jeraha dogo tu ndio mjue kua kuna Mungu na wanadamu.
 
MADAI
Kuna magonjwa mengi yanayosababisha upungufu wa Kinga mwilini ikiwemo maambukizi ya VVU.

Kumekuwa na mijadala mingi pamoja na tetesi zinazohitaji majibu ya kina kuhusu uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kutoka kwa mtu aliye athirika hasa ikihusisha ushiriki wa tendo la ndoa pasipo kutumia kinga hata kama ni mara moja tu.

View attachment 2405505

Ukweli upoje na majibu ya kisayansi yanatoa picha gani? Baadhi hudai hauwezi kupata VVU/UKIMWI kwa kufanya tendo moja tu la ngono na muathirika pasipo kutumia kinga kwa kuwa maambukizi hayaji kirahisi hivyo kama tunavyodhani.
Hebu tuseme "KUZINI" Au "kufanya uzinzi" na siyo kufanya tendo la ndoa.sababu tendo la ndoa ni kwa wanandoa.

Huko kwingine nawaachia wanasayansi
 
Mimi nahisi Kuna elimu haiko wazi juu ya ugonjwa huu kama Kuna vtu tumefichwa hivi...mbona watu wanaishi na walioathirika ,wanapiga kavu ,wanazaa watoto wenye afya njema na maisha yanaendelea.ila Kuna mwingine akigusa tu kanasa.
Jambo kubwa ni mwenendo wa matibabu kwa huyo unayekutana nae. Akiwa kwenye dawa kwa usahihi kiwango cha virus kinashuka chini sana na hawezi kuambukiza kwa njia ya ngono

Hatarishi kwa maambukizi ni watu waliopata maabukizi chini ya mwezi mmoja, hao wanakua na idadi kubwa sana ya virusi, wengine ni wasio kwenye matibabu na tayari wanaelekea kwenye UKIMWI
 
Kama mwathirika wa virusi vya ukimwi anatumia dawa na viral load iko chini ya 100 mpaka 0 na CD4 ikiwa ipo juu, hapo piga kavu kavu hakuna shida.

Lakini kwa uhakika zaidi vaa kondom kwa usahihi. VVU ni noma
Ikiwa mwathirika anatumia dawa ipasavyo na ukashiriki nae tendo na mpaka mkapata michubuko,je matokeo yake yatakuaje?
Je kwann asikuambukize wakat mmechubuana?
Je toka virusi kuingia mwilini vitatumia mda gan kuanza kuonekana kwenye vipimo
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom