Inawezekana Kupunguza URASIMU Maofsini na Tukawajali Wateja?

Teamo

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
12,272
1,034
Nilichokuwa nakiamini mimi ni kwamba UTANDAWAZI,na exposure tuseme INGETUOKOA!lakini hamna kitu.

Nilichokuwa nakiamini pia ni kwamba jambo moja linapolalamikiwa sana LABDA WALALAMIKIWA WANGESTUKA NA KUBADILIKA,hilo bado halipo kabisa.

URASIMU umezidi kipimo kwenye maofisi mengi hapa tz HASA HASA MAOFISI YA SERIKALI,HUSUSANI MAWIZARANI,na ofisi mbali mbali za wilaya na manispaa.

Inasikitisha sana mteja anasubiri mtu ofisini ZAIDI YA MASAA SITA!mhusika mwenyewe yumo mule mule ndani ANAZUNGUKA ZUNGUKA TU!anataka nini huyu jaman?

Inasikitisha zaidi unapoifuatillia saini moja tu kwenye document yako FOR TWO MONTHS,with no reason.utaambiwa mara kuna kikao,mara muhusika yupo likizo,mara amerud,mara hajaingia ofisin.

Inauma sana mteja anafuatilia TRANSCRIPT OF RECORDS ili aaply kazi ANASUBIRI MIEZI MINNE,as if kazi inamsubiri yeye.(hili lilinigusa zaiidi,maanake nilikosa sponsorship ya masters kwa HILI TU)

sasa mi najiuliza:

ELIMU TUNAYOIPATA INATUSAIDIA?

UTANDAWAZI UNATUSAIDIA?

EXPOSURE INATUSAIDIA?

KUNA UMUHIMU WA WATUMISHI WA SERIKALI WA SASA KUENDELEA NA KAZI?

KIZAZI HICHI PIA BAADA YA MIAKA KUMI WATAKUWA KWENYE SYSTEM,JE WATAISHI HIVI HIVI?

..............AU NDO MIAFRIKA NDIVYO ILIVYO?

kwani?hivi tunahitaji sana URASIMU?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom