Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,527
- 46,053
1.Kwa nini serikali inamiliki ndege?
Ndege zilinunuliwa kama hitaji muhimu kwa wananchi au fahari ya taifa?
2. Serikali kuhamia Dodoma.
Serikali ilihamia Dodoma ili kumuenzi Nyerere kama baba wa Taifa au lilikuwa ni hitaji muhimu la lazima la Taifa?
3.Kujenga miradi mikubwa kwa pesa zetu wenyewe za ndani ni akili kubwa au ndogo?
Sio kwamba hiyo ni kuongeza maumivu kupitia kukusanya kodi kwa nguvu zaidi badala akili? Tunazo pesa nyingi kiasi hicho?
4.Gesi ya Kusini bado ina mchango katika umeme wa nchi yetu? Mabeberu wamepewa au bado ni yetu?
5.Bandari ya Bagamoyo. Nani alisema au anasema kweli hasa?
6.Katiba mpya. Je tunahitaji au bado haina umuhimu kwa sasa?
7. Kila zama inaruhusiwa kuandika kitabu chake? Hii ni zama ya nani? Mwenye zama hii na yeye anaruhusiwa kuandika kitabu chake au lazima aendelee na kitabu alichokikuta?
Hizi nazo ni baadhi ya "Legacies" ambazo wafahidhina na wataka mabadiliko wanazozana!
Faida gani zilipatikana au zitapatikana kwa wananchi wanyonge na wasio wanyonge kwa maamuzi haya?
Tukiweza kupata majibu ya pamoja ya mambo hayo na mengine machache makubwa tutafunga kabisa huu mjadala wa "Legacy".
Ndege zilinunuliwa kama hitaji muhimu kwa wananchi au fahari ya taifa?
2. Serikali kuhamia Dodoma.
Serikali ilihamia Dodoma ili kumuenzi Nyerere kama baba wa Taifa au lilikuwa ni hitaji muhimu la lazima la Taifa?
3.Kujenga miradi mikubwa kwa pesa zetu wenyewe za ndani ni akili kubwa au ndogo?
Sio kwamba hiyo ni kuongeza maumivu kupitia kukusanya kodi kwa nguvu zaidi badala akili? Tunazo pesa nyingi kiasi hicho?
4.Gesi ya Kusini bado ina mchango katika umeme wa nchi yetu? Mabeberu wamepewa au bado ni yetu?
5.Bandari ya Bagamoyo. Nani alisema au anasema kweli hasa?
6.Katiba mpya. Je tunahitaji au bado haina umuhimu kwa sasa?
7. Kila zama inaruhusiwa kuandika kitabu chake? Hii ni zama ya nani? Mwenye zama hii na yeye anaruhusiwa kuandika kitabu chake au lazima aendelee na kitabu alichokikuta?
Hizi nazo ni baadhi ya "Legacies" ambazo wafahidhina na wataka mabadiliko wanazozana!
Faida gani zilipatikana au zitapatikana kwa wananchi wanyonge na wasio wanyonge kwa maamuzi haya?
Tukiweza kupata majibu ya pamoja ya mambo hayo na mengine machache makubwa tutafunga kabisa huu mjadala wa "Legacy".