Inawezekana hofu ya Serikali kupunguza kodi ya uingizaji wa magari inatokana na hofu ya ukosefu barabara za kutosha kwa jiji la Dar-es-Salaam

Mkuu hakuna gari jipya (miaka ya karibuni) lenye kodi nafuu kuliko gari la zamani (miaka ya nyuma) la aina hiyohiyo. Angalia na kucompare kwenye kalkuleta ya TRA na angalia mitaani gari nyingi ni zipi, mpya au za zamani.

Serikali haidiscourage watu kununua magari ya zamani bali kupitia ushuru inadiscourage watu kununua magari tu kwa ujumla (yawe mapya au ya zamani) bila sababu ya msingi.

Ndio sababu inayofanya watu waone kuwa serikali bado ina mawazo ya zamani, kuona gari kama anasa na kuwabania tu raia wake.
Anyway, kwanza usafiri binafsi ni gharama na ni mzigo.

Muhimu serikali iboreshe usafiri wa umma.

Hata nchi zilizoendelea usafiri wa umma unaboreshwa ili watu wautumie kurpusha mifoleni isiyokuwa na sababu.

Unakuta msululu wa FOLENI ya magari 100 halafu yote ukichungulia ndani yana mtu MMOJA MMOJA tu. Upuuzi tu.

Nchi zetu masikini tunachukulia kuwa na gari ndio mafanikio kitu ambacho ni mindset ya kijinga tu.
 
Lengo la kuweka kodi kubwa kwenye magari ( used ) ni kupunguza import kubwa ya magari used nchini. Ndio maana magari mapya kodi zake ni nafuu kuliko used.

Vinginevyo nchi itageuka jalala.
Used ya ulaya kwa bongo ni mpya kabisa.
 
Sio tu ununuzi wa mafuta utaongezeka, bai hata ununuzi wa vipuri vya magari utaongezeka sambamba na watu kuuziana magari humu nchini ili wenye fedha zao waagize magari ya kisasa zaidi(watauza na kununua) na hapo serikali itapata mapato zaidi.

Na scrapers (chuma chakavu pia itaongezeka) kwa watu kuchinja yaliyochoka na kugeuzwa kuwa bidhaa nyingine kv. nondo, safuria nk nk..
 
Anyway, kwanza usafiri binafsi ni gharama na ni mzigo.

Muhimu serikali iboreshe usafiri wa umma.

Hata nchi zilizoendelea usafiri wa umma unaboreshwa ili watu wautumie kurpusha mifoleni isiyokuwa na sababu.

Unakuta msululu wa FOLENI ya magari 100 halafu yote ukichungulia ndani yana mtu MMOJA MMOJA tu. Upuuzi tu.

Nchi zetu masikini tunachukulia kuwa na gari ndio mafanikio kitu ambacho ni mindset ya kijinga tu.
Sasa huu ndio mtazamo wa serikali yetu, inayotokana na maoni ya wataalamu wa serikali yetu ambao fikra zao ni kama zako. Hiyo kauli ya mwisho ya kuchukulia gari kuwa mafanikio ingawa umeisema kwa mtazamo wa raia (wananchi) inakata vilevile kwa serikali, kuona gari kama ni mafanikio sana kiasi cha kuweka kodi kubwa kumtoza mwananchi kwa gari analoagiza, BADILIKENI, mnatucheleweshea maendeleo kwa kutokusanya kodi ambayo ingeletwa na uagizaji wa magari
 
Binafsi siamini kuwa serikali hii ya sasa, kama ilivyokuwa kwa serikali zilizopita, hawaelewi kuwa ukipinguza kodi ya kuingiza magari nchini, watu wengi zaidi wataagiza magari na hivyo kuiongezea zaidi serikali mapato, bali naamini wanahofia miundombinu ya jjji kuzidiwa na wingi wa magari ila hii imekuwa ni siri yao.

Hali hii ni kutokana na ukweli kuwa asilimia kubwa ya magari hubaki jijini Dar-es-Salaam (Jiji la Ilala) na asilimia ndogo tu ndi huenda mikoani.

Hivyo, ukishusha kodi, kuna uwezekano baada ya muda uingizaji wa magari kuongezeka kwa kasi na kufanya baadhi ya barabara za jiji kuwa na foleni kubwa zaidi na hiki ndio serikali huenda wanakihofia kwani mpaka sasa tatizo la foleni katika huu mji teyari ni tatizo na kero kubwa kwa wakati wa huu mji.

Kama kodi ya kuingiza magari nchini ni karibu bei ya kununulia gari huko nje, ni wazi ukipinguza kodi ya kuingiz magari kwa asilimia kubwa mfano kwa asilimia 25 a tu, watu wengi zaidi watamudu kuingiza magari na kuongeza mapato ya serikali lakini kuna hatari ya miundombinu kushindwa kuhimili ongezeko hilo hasa nyakati za asubuhi na jioni kwani private car zinaweza kuongezeka kwa kiwango kikubwa.

Wenye fedha zao watauza magari yao kwa wingi humu nchini ili waagize mengine ya kisasa na bora zaidi (new model, n.k), na hivyo kuongeza magari used ya kibongo na wakati huo huo kupelekea ongezeko la magari used kutoka nje.

Pia, tutarajie ongezeko la magari ya mikopo kutoka kwa wafanyakazi wa serikali na wa sekta binafsi na kwa maana hiyo kutakuwa na ongezeko kubwa la magari hasa Dar-es-Salaam na ongezeko kubwa la mapato ya serikali kupitia kodi ya uingizaji wa magari lakini barabara za jiji zikizidiwa.

Kwa Dar-es-Salaam magari mengi yanaonekaba kuwa na plate number mpya na hiki kinaweza kuwa ni kiashira tosha kuwa sehemu kubwa ya magari (hasa ya kutembelea) hubaki Dar-es-Salaam na asilimia ndogo ndio huenda mikoani na hivyo kuchangia kukua kwa tatizo la foleni jijini Dar-es-Salaam (Ilala)

Hivyo, kwa mtazamo wangu, ugumu wa serikali kupunguza kodi ya kuingiza magari inawezekana inatokana zaidi na hofu ya kuongeza kwa foleni za magari jijini Dar-es-Salaam pamoja na siku moja tukafikia hatua ya magari kushindwa kutembea kabisa hasa nyakati za asubuhi na jioni.

Kwa maneno mengine,serikali kutoza Kodi kubwa za uingizaji wa magari lengo sio serikali kukusanya mapato mengi, bali yawezekana lengo hasa ni kudhibiti uingizaji wa magari nchini wakilenga jiji la Dar-es-Salaam.

Kama hii ndio hasa concern yao, basi wapunguze kodi ya magari yasiyo ya kutembelea (malori,mabasi,n.k) na ikiwezekana kwa magar yanayoingizwa nchini na kisha kupelekwa mikoani ingawa hii inaweza kuwa ni uchochoro wa watu kukwepa kodi kwa kuingiza magari wakida yanakwenda mikoani halafu baadae wakayarudisha jijini unless uwekwe utaratibu maalumu wa kudhibiti unadanganyifu huo unaoweza kujitokeza.

Ni mtazamo wangu pia hata uamuzi wa serikali ya Magufuli kuharakisha kuhamia Dodoma, umesukumwa pia na dhamira ya kupunguza foleni katika jiji la Dar-es-Salaam ingawa serikali haiwezi kukiri hadharani.

No wonder pia serikali imekuwa tayari kutumia mabilioni kujenga daraja la kupita juu ya bahari lengo likiwa ni lile lile la kupunguza foleni na kuwaondolea adha ya kukaa foleni wakubwa wanaoingia na kutoka katikati ya jiji.

Ukisikia siri za serikali au za usalama wa nchi, basi inaweza kuhusu mambo kama haya, mambo ambayo watu wengi wala hawawezi kuyafikiria wala kuyawaza, ila wao kama serikali kwa kutumia data walizonazo, wanakuwa wameshaona hatari ya nini kinaweza kutokea.

Wengi hamtanielewa ila huu unaweza kuwa ndio ukweli wenyewe kwa wanaotazama mambo kwa umbali.
Kuna sababu nyingi zinazowafanya serekali wasipunguze important duty (40%) kwa magari plus vat 18%.
1. hatuna njia ya kuyatoa hayo magari yakichakaa, yani dumping strategy yetu ni ipi. Wenzetu wanadumpia Afrika sisi tunadump wapi.
2. Magari mabovu na used chakaa yatajaa tanzania na hilo lina madhara mengi kimazingira nk.
3. Foleni itakuwa kubwa sana kwani magari yatakithiri. Ni heri kuiomba serekali kuondoa import duty na VAT na kuweka 0% kwa magari mapya na huo ndo utaratibu ulokuwepo kwa authorized dealer wa magari na sio kwa mtu mmoja mmoja. Hii itafanya watu wanunue magari mapya ambayo ni mazuri kwa afya ya nchi yetu.

Serekali za wenzetu wanashajihisha watu kununua electric cars sasahiv na wana incentive nyingi.

Mawazo yako ni ya kimasikini na kinyonge. Badili mtazamo ndogo mana kodi ya magari used tena ikipungua italeta maafa makubwa nchini.

Ni heri upiganie kodi ya necessities kama nguo, chakula na raw material muhimu kwa uzalishaji.
 
Lengo la kuweka kodi kubwa kwenye magari (used) ni kupunguza import kubwa ya magari used nchini. Ndio maana magari mapya kodi zake ni nafuu kuliko used.

Vinginevyo nchi itageuka jalala.
Una uhakika gari jipya kodi yake ni nafuu kuliko lililotumika?
 
Ila mwaka huu,miezi michache iliopita kodi ya magari imeshuka kwa mujibu wa kikokotoo cha TRA. Mama amesikia kilio chenu.
 
Lengo la kuweka kodi kubwa kwenye magari (used) ni kupunguza import kubwa ya magari used nchini. Ndio maana magari mapya kodi zake ni nafuu kuliko used.

Vinginevyo nchi itageuka jalala.
Umefeli bongo gari la 2017 kodi yake kubwa kuliko la 2005 ndio mana unaona harrier ya 2007 na subaru za 2007 zinaitwa new model wakati zipo harrier za 2019 watu hawaziwez sababu ya kodi....
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Mama kashusha sana kodi ya magari used. Kuna gari za 2013/14 ushuru ulikuwa 18m sasa hivi ni 8m
 
Back
Top Bottom