Blackafrica
Senior Member
- Jun 26, 2021
- 141
- 401
Hii nchi ina kila kitu cha kuifanya iwe nchi Tajiri, lakini bado ni nchi maskini inayotegemea misaada kutoka kwa walipa kodi wa nchi nyingine, kila mradi unaofanyika Tz karibu yote inafadhiriwa na wahisani yaani ni aibu sana.
Nchi ambayo tunajivuna ina amani na rasilimali za kutosha, ilipaswa iwe nchi yenye maendeleo ya kujivuna, lakini ukweli ni kwamba ni nchi ya ajabu sana, idara zake nyingi zinanuka rushwa yaani kufanya biashara Tanzania inakubidi uwe na moyo kweli kweli, coz hakuna haki katika biashara, pia watu sio waamininfu na vile vile vyombo vingi vinavyohusika na mambo ya biashara havitekelezi wajibu wake vizuri.
Tunashindwa na nchi kama Rwanda kanchi kadogo, hata kenya yenyewe sio wa kutushinda sisi ambao tupo zaidi ya watu milioni 60, nchi haina dira, kila kiongozi anapangua na kupanga anavyotaka yeye, wananchi wengi ni wa hovyo, yaani kutokana na nchi kuwa ya hovyo hovyo hata wananchi tumekuwa wa hovyo hovyo, ni suala la muda tu, ila tunakoelekea wananchi wengi watanzania tutakuwa na sifa ya kuwa matapeli kama wanaigeria.
Tulipofika hapa tunahitaji mabadiliko kwa kweli, inawezekana CCM ikawa ni tatizo, hofu ya wengi yupi atakuwa mbadala wa CCM, nadhani waliopo ndani ya CCM waone hii fursa, wananchi wanataka mabadiliko sio vibaya tupate mabadiliko kwa kuwa na chama imara mbadala wa CCM, hicho chama kitokane na wanaccm waliochoshwa na wanaotaka mabadiliko, lakini vile vile kiwe na muunganiko na watanzania wazalendo wanaohitaji mabadiliko ya kweli katika nchi yao.
Tukubaliane hapa mda tuliowapa hawa jamaa CCM wa kuwa madarakani umetosha, sasa iwe zamu ya wengine nao pia tuwajaribu, labda wanaweza kutuvusha katika mabadiliko tunayoyataka, tuanze kujianda sasa kuhakikisha Tanzania tunayoitaka tunaifikia kwa kuhakikisha tunawaondoa madarakani hawa walioshindwa kazi miaka yote hiyo tuliyowapa kazi, 2025 ipo karibu tutumie fursa ya uchaguzi na fursa nyingine zozote kuwaondoa hawa jamaa ni tatizo katika nchi hii.
Nchi ambayo tunajivuna ina amani na rasilimali za kutosha, ilipaswa iwe nchi yenye maendeleo ya kujivuna, lakini ukweli ni kwamba ni nchi ya ajabu sana, idara zake nyingi zinanuka rushwa yaani kufanya biashara Tanzania inakubidi uwe na moyo kweli kweli, coz hakuna haki katika biashara, pia watu sio waamininfu na vile vile vyombo vingi vinavyohusika na mambo ya biashara havitekelezi wajibu wake vizuri.
Tunashindwa na nchi kama Rwanda kanchi kadogo, hata kenya yenyewe sio wa kutushinda sisi ambao tupo zaidi ya watu milioni 60, nchi haina dira, kila kiongozi anapangua na kupanga anavyotaka yeye, wananchi wengi ni wa hovyo, yaani kutokana na nchi kuwa ya hovyo hovyo hata wananchi tumekuwa wa hovyo hovyo, ni suala la muda tu, ila tunakoelekea wananchi wengi watanzania tutakuwa na sifa ya kuwa matapeli kama wanaigeria.
Tulipofika hapa tunahitaji mabadiliko kwa kweli, inawezekana CCM ikawa ni tatizo, hofu ya wengi yupi atakuwa mbadala wa CCM, nadhani waliopo ndani ya CCM waone hii fursa, wananchi wanataka mabadiliko sio vibaya tupate mabadiliko kwa kuwa na chama imara mbadala wa CCM, hicho chama kitokane na wanaccm waliochoshwa na wanaotaka mabadiliko, lakini vile vile kiwe na muunganiko na watanzania wazalendo wanaohitaji mabadiliko ya kweli katika nchi yao.
Tukubaliane hapa mda tuliowapa hawa jamaa CCM wa kuwa madarakani umetosha, sasa iwe zamu ya wengine nao pia tuwajaribu, labda wanaweza kutuvusha katika mabadiliko tunayoyataka, tuanze kujianda sasa kuhakikisha Tanzania tunayoitaka tunaifikia kwa kuhakikisha tunawaondoa madarakani hawa walioshindwa kazi miaka yote hiyo tuliyowapa kazi, 2025 ipo karibu tutumie fursa ya uchaguzi na fursa nyingine zozote kuwaondoa hawa jamaa ni tatizo katika nchi hii.