Inauma sana

CYPRIAN MKALI

Senior Member
Nov 12, 2010
176
65
Kuna jamaa yangu kanifuata kuomba ushauri juu ya tabia ya mke wake, naomba busara zenu wadau.
ishu ni kwamba toka mke wake apate ujauzito, nyumba imewaka moto!
shem amekuwa anamgomea mara nyingine hata kuchomeka neti na kutandika kitanda akidai ajisikii kutandika km hataki walale ivyo ivyo.
amekuwa mara nyingi anamajibu ya mkato na dharau ktk mazungumzo yao ya kila siku. kubwa kuliko hataki kabisa kushiriki tendo akidai hajisikii kufanya ivyo na ukizingatia ujauzito ndo kwanza una mwezi 1 [SUP]1[/SUP]/[SUB]2[/SUB].
mimi wakwangu hakuwa ivyo ati, so nashindwa amini sana ila sina uhakika labda kuna wengne wanakuwa ivyo au ni usanii tu?
jamaa amechanganyikiwa na ndoa ndo bado changa. nilipo muuliza unafikiria kufanya nini ju ya hili, akaniambia anataka atafute mwingne wa pemben hapo ndo nilizidi changanyikiwa nikahisi lipo juu ya uwezo wangu.
 
mambo ya kawaida sana haya,mwambie atulize ball hali itabadilika.Kila mimba huwa ina mambo yake,tena jamaa yako cha mtoto kuna ambao huwa wanawachukia waume zao hadi hawataki kuwaona kabisa mpaka mtu anahama chumba sembuse hii.Mwambie aachane na mawazo ya mahawara miezi tisa ni nini bana?
 
Mimba kuna kipindi inakuwa kama inaleta ukichaa fulani hivi, lakini kwa huyo mwanamke amezidi! Mimba ya mwezi mmoja na nusu ndiyo inampeleka kihivyo! Halafu lipo swala lingine la kisaikolojia kwa wanawake wakipata mimba huona wameshamaliza kila kitu katika ndoa hivyo kujifanyia anavyotaka. Mshauri jamaa yako amuelimishe mkewe athari za tabia yake hususani ya kumnyima unyumba maana vingine mume anaweza kujitahidi kuvifanya kama kazi ndogo ndogo kama ulizosema kutandika net na hata kuosha vyombo, kufua kama jamaa hayupo busy sana lakini la unyumba halina substitute kama kweli amelishika agano la Mungu. Sasa kwa nini iwe hivyo, ndoa imewekwa ili kutupa wanadamu urahisi ikiwemo kupoza mioyo yetu, sasa ikigeuka vita kunakuwa na walakini.
 
.......Mwambie aachane na mawazo ya mahawara miezi tisa ni nini bana?
Mwambie kabisa mahawara ni gharama kuwahandle asije kufikiria watu wanauza maneno nje, kama huna pesa utakuwa unajitafutia balaa bure ila ukiwa nazo huwezi kunote maana kila mara utakuwa unaambiwa honey I love and others mpaka uone mapenzi si ndiyo haja kumbe umeingia chaka!
 
Wanaume wenye ndoa changa mnahitaji shule kuhusu "Women Psychology". Mke anapokuwa mjamzito kuna mabadiliko hutokea ambayo zaidi ni sababu za kisaikolojia na mabadiliko ya homoni katika mwili. Sababu hizi hazifanani na hutofautiana kutoka mwananamke mmoja na mwingine. Moja ya mabadiliko ni pamoja na kutopendelea aina fulani ya vyakula ambavyo kabla ya ujauzito haukuwa tatizo, baadhi kuwachukiwa waume zao, kukosa hamu ya tendo n.k. na mengine mengi. Kiukweli kuna ambao huwachukia sana waume zao, lakini pia kuna ambao huwapenda sana waume zao kiasi cha kutaka awe naye wakati wote (hii nayo inweza kuwa kero kwa baadhi ya wanaume), kuna wengine wanakuwa neutral zaidi na kukubaliana na hali halisi ya ujauzito.

Haijalishi mimba ni muda gani kwa sababu mabadiliko huja kutokana na hali halisi ya wakati huo. Hapo ni ujauzito, baada ya kujifungua pia kuna mabadiliko, kwa kuwa wakati huu mke huweka attention yake yote kwa mtoto, so mume unakuwa second priority. Hii ni akina mama wote, exceptions chache zipo. So, mwanaume unatakiwa uishi na mke kwa akili. Jifunze yale ambayo ukuyafahamu kabla ya ndoa.

Mabadiliko ambayo hayatokani na ujauzito hicho ni kitu kingine. So, mwambie avumilie na afahamu kuwa hiyo ni hali ya kawaida na anatakiwa kuwa more supportive than before.
 
Kuna jamaa yangu kanifuata kuomba ushauri juu ya tabia ya mke wake, naomba busara zenu wadau.
ishu ni kwamba toka mke wake apate ujauzito, nyumba imewaka moto!
shem amekuwa anamgomea mara nyingine hata kuchomeka neti na kutandika kitanda akidai ajisikii kutandika km hataki walale ivyo ivyo.
amekuwa mara nyingi anamajibu ya mkato na dharau ktk mazungumzo yao ya kila siku. kubwa kuliko hataki kabisa kushiriki tendo akidai hajisikii kufanya ivyo na ukizingatia ujauzito ndo kwanza una mwezi 1 [SUP]1[/SUP]/[SUB]2[/SUB].
mimi wakwangu hakuwa ivyo ati, so nashindwa amini sana ila sina uhakika labda kuna wengne wanakuwa ivyo au ni usanii tu?
jamaa amechanganyikiwa na ndoa ndo bado changa. nilipo muuliza unafikiria kufanya nini ju ya hili, akaniambia anataka atafute mwingne wa pemben hapo ndo nilizidi changanyikiwa nikahisi lipo juu ya uwezo wangu.
Wewe unakuwa kama mgeni bana, mke wako ni mke wako na hawezi kufanana na mke wa rafiki yako. Na hustoe ushauri kwa kum-refer mke wako utavunja ndoa ya mwenzio. Ndoa hazifanani hata siku moja ndugu yangu,
 
NDOA; Nyumbani Daima Omba Amani
Wakati wakuapa anakumbuka alisema nini?anakumbuka nyakati zote alizoahidi kua atakua na mkewe?
Wanaume jamani kutandika au kuweka net kuna ishu gani??
Nijuavyo wanaume ni watu wasiopenda malumbano sasa mbona huyu anakua tofauti?ushajua mkeo mjamzito,awe anavunga au ni kweli usjali,wewe fanya pale alipogoma wala asibishane nae hata dk moja,kama huyo mwanamke yuko sawa atajirudi tena kabla hajazaa,ajifunze kuwa mkimya na kufanya anachogoma bila majibizano mana hayo ndio yanampa mkewe power yakuongea kwa kufanya hivyo lazima atanyooka na tendo la ndoa kama kawaida ajaribu wiki tu aone,naamini mwanaume alieoa anaweza.
Kutafuta wa pembeni simshauri coz pesa nayopoteza kwa malaya huyo ni bora akazitumia kuandaa vitu vya mtoto na maandaizi ya mkewe kujifungua kwenye hospital nzuri na kuhakikisha anapata lishe bora ili azae mtoto mwenye afya
Sijui mwenzangu ni mkristo au mwislam ila biblia yangu inasema kwenye Mithali 6:32-33 aziniye na mwanamke ni mpumbavu na ukiendelea mbele utapata maneno mazuri tuuu,pia kumbuka huyo ni mkeo na bado mtazaaa na kuzaa na pia mtakua pamoja hadi kifo kiwatenganishe sasa utabadili wangapi? na Mungu anakuangalia tu au?


"Usifanye kosa kwakua mwenzio amekosa"
 
NDOA; Nyumbani Daima Omba Amani
Wakati wakuapa anakumbuka alisema nini?anakumbuka nyakati zote alizoahidi kua atakua na mkewe?
Wanaume jamani kutandika au kuweka net kuna ishu gani??
Nijuavyo wanaume ni watu wasiopenda malumbano sasa mbona huyu anakua tofauti?ushajua mkeo mjamzito,awe anavunga au ni kweli usjali,wewe fanya pale alipogoma wala asibishane nae hata dk moja,kama huyo mwanamke yuko sawa atajirudi tena kabla hajazaa,ajifunze kuwa mkimya na kufanya anachogoma bila majibizano mana hayo ndio yanampa mkewe power yakuongea kwa kufanya hivyo lazima atanyooka na tendo la ndoa kama kawaida ajaribu wiki tu aone,naamini mwanaume alieoa anaweza.
Kutafuta wa pembeni simshauri coz pesa nayopoteza kwa malaya huyo ni bora akazitumia kuandaa vitu vya mtoto na maandaizi ya mkewe kujifungua kwenye hospital nzuri na kuhakikisha anapata lishe bora ili azae mtoto mwenye afya
Sijui mwenzangu ni mkristo au mwislam ila biblia yangu inasema kwenye Mithali 6:32-33 aziniye na mwanamke ni mpumbavu na ukiendelea mbele utapata maneno mazuri tuuu,pia kumbuka huyo ni mkeo na bado mtazaaa na kuzaa na pia mtakua pamoja hadi kifo kiwatenganishe sasa utabadili wangapi? na Mungu anakuangalia tu au?


"Usifanye kosa kwakua mwenzio amekosa"
Sasa waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani ameshajifunza jambo kwa leo hapa JF. Duh, sikujua hii maana
 
Wewe unakuwa kama mgeni bana, mke wako ni mke wako na hawezi kufanana na mke wa rafiki yako. Na hustoe ushauri kwa kum-refer mke wako utavunja ndoa ya mwenzio. Ndoa hazifanani hata siku moja ndugu yangu,

Labda hukunielewa mkuu, ndo maana nikaendelea zaidi kuwa sina hakika juu ya hilo na hivyo nikahitaji busara zenu. vinginevyo ningemjibu kwa kumuangalia wangu, just read between the lines.
 
wow! nashukuru wote kwa busara zenu, mmekuwa mchango mzuri sana kwa rafiki yangu. nimekuja tambua kuwa yeye alijua anajifanyisha kwani mimi alikuwa ananikuta tunaenjoy so kaniahidi kuwa mpole na kumpa ushikiano zaidi huyo mke wake na suala la hawala kaniahidi atatumia uwezo wake kumvumilia ingawa alikuwa akifikiria huo muda(miezi km 10 mbele) alionekana kuto kuwa na amani, ASANTENTI SANA.
 
hizo kazi ndogo ndogo kama zinamshinda mkeo,weka housegirl ila mie ningekushauri utafute nyumba ndogo ila ucheze safe huko nje kuna magonjwa mengi,mkeo akijirudi uibwage nyumba ndogo asipojirudi baki nayo kuna wanawake wanahitaji wasaidizi mkeo ni mmojawapo.........sijui anafanya makusudi au la ila unahitaji mtu wa kusuplement kinachokosekana ndani ya ndoa yako period.
 
hizo kazi ndogo ndogo kama zinamshinda mkeo,weka housegirl ila mie ningekushauri utafute nyumba ndogo ila ucheze safe huko nje kuna magonjwa mengi,mkeo akijirudi uibwage nyumba ndogo asipojirudi baki nayo kuna wanawake wanahitaji wasaidizi mkeo ni mmojawapo.........sijui anafanya makusudi au la ila unahitaji mtu wa kusuplement kinachokosekana ndani ya ndoa yako period.
wewe ni mwanamke kweli nina mashaka na wewe
 
hizo kazi ndogo ndogo kama zinamshinda mkeo,weka housegirl ila mie ningekushauri utafute nyumba ndogo ila ucheze safe huko nje kuna magonjwa mengi,mkeo akijirudi uibwage nyumba ndogo asipojirudi baki nayo kuna wanawake wanahitaji wasaidizi mkeo ni mmojawapo.........sijui anafanya makusudi au la ila unahitaji mtu wa kusuplement kinachokosekana ndani ya ndoa yako period.

This is the worst scenario one may consider. If it is implemented, its impact will be likened to a tsunami.
 
mwambie asijali mara nyingi wanawake wanapokuwa ktk hali hii huwa navisilani vya ajabu mpe hongera kwa kummezesha mkewe mtoto asijute
 
sina cha kukupunguzia labda cha kukuongezea mwe

N akama ni mwanamke basi hajaolewa na kama kaolewa hajawahi kubeba mbimba na kama bado yupo ndoani hiyo ndoa aijuae ni mola. Au ameshatendwa hadi kaamua kuwa kama alivyo na above inawezekana yeye ni nyumba ndogo ya mtu.
Samahani kwakuharibu thread ya mtu ila nimejiskia kuongea kuhusu Jestina
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom