Inatosha - Lowassa Jiuzulu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995

56906.jpg
Pichani Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa (Monduli - CCM) akiapa kuilinda Katiba alipoapishwa kuwa Waziri Mkkuu

Hatimaye mchawi wa Richmond ni yule ambaye watu walimhisi kwa muda mrefu. Na sasa tumegundua hakuwa peke yake. Taarifa ya leo ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa mwishoni mwa mwaka jana kuchunguza mkataba wa Richmond imeonesha kuwa siyo tu taratibu zilikiukwa bali pia kuna ushahidi mkubwa wa rushwa.

Ripoti hiyo ambayo unaweza kuipata kwenye tovuti ya http://www.klhnews.com inaonesha wazi kuwa mhusika mkubwa wa sakata hili zima ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa vile bwana Lowassa aliapa kuilinda na kuitetea Katiba yetu na kwa vitendo vyake ameshindwa kufanya hivyo hana budi kuwa wa kwanza kuwajibika yeye mwenyewe bila ya kungojea kuwajibishwa. Mhe. Lowassa kwa hili umekosea na liwe somo kwa viongozi wengine wote kuwa Tanzania inabadilika na viongozi wasioongoza hawana budi kuwekwa pembeni. Mhe. Lowassa tunataka ujiuzulu wadhifa wako mara moja.

Pamoja na wewe wahusika wengine wote ambao wanatajwa katika ripoti hiyo akiwemo Waziri Msabaha, Karamagi, Rostam Aziz na Mwanyika nao pia wajiuzulu mara moja kwa kutumia madaraka yao vibaya, kulidanganya Taifa, kufanya kazi kinyume na maadili, na kwa kuliletea Taifa letu hasara.

Watanzania wana mambo mengine ya msingi ya kufuatilia (kama BoT na mengine) na wakati umefika suala la Richmond lifikie kikomo kwa viongozi na wahusika wote kujiuzulu. Tulishasema toka awali kuwa Baraza hili la mawaziri ni la kishikaji na ambalo limemwangusha sana Rais na kwa hakika ni kujiangusha alikojitakia kwani alishaonywa, halina budi kuvunjwa ili Baraza jipya litakalokidhi hamu na matamanio ya Watanzania na ambalo wajumbe wake watatoka hata nje ya CCM liundwe ili tuendelee na jitihada za kulijenga Taifa letu

Watanzania naomba kutoa hoja!
 
Hivi hoja hii inaweza kufikishwa Chamwino kwa Muungwana?

Dotori kila unacho kiandika hapa kuanzia Rais wa Nchi hadi mamvi wote wanapewa taarifa kila siku na kusoma pia .Wana watu na mtu kama JK anamuda wake wa kuja JF na kusoma mwenyewe .Kwa taarifa tu ni kwamba JF inamsaidia sana JK kujua mambo kulio magazeti mengi ya hapa nyumbani .
 
Dotori kila unacho kiandika hapa kuanzia Rais wa Nchi hadi mamvi wote wanapewa taarifa kila siku na kusoma pia .Wana watu na mtu kama JK anamuda wake wa kuja JF na kusoma mwenyewe .Kwa taarifa tu ni kwamba JF inamsaidia sana JK kujua mambo kulio magazeti mengi ya hapa nyumbani .

Lunyungu
Nakubaliana na wewe, nami naitumia forum hii kupata in depth analysis ya yale yanayoandikwa katika magazeti yetu.
Kama Muungwana anayapata yale yanayojiri hapa, basi akate kiu cha watanzania katika sakata hili.
 
Hii imeniacha hoi!...

"Lakini Mhe. Dk. Msabaha (Mb), baada ya mahojiano chini ya kiapo, akaiuma sikio Kamati Teule kuwa katika suala hilo yeye atakuwa kondoo wa kafara tu au, kwa maneno yake mwenyewe, "Bangusilo" kwa lugha ya Kizaramo. Maelezo hayo ya ziada nje ya kiapo ya Mheshimiwa Waziri yaliyotoa ujumbe kuwa "si yeye ila mkuu wake wa kazi", yalioana na maelezo aliyoyatoa Balozi Kazaura nje ya kiapo tarehe 30 Novemba, 2007. Mara baada ya kumaliza mahojiano kwa kiapo na Kamati Teule, Balozi akatoa maelezo ya ziada kuwa Richmond ilikuwa mradi wa "Bwana Mkubwa" na "mshiriki wake mkubwa kibiashara", akimaanisha Mhe. Waziri Mkuu na Mhe. Rostam Aziz (Mb)."...
 
Mimi nafikiri rais inabidi avunje baraza lote la mawaziri na aunde baraza jipya.

Pia taasisi ya kuchunguza na kuzuia rushwa inabidi iundwe upya ikiwa inajitegemea na mkurugenzi wake awe anapitishwa na bunge.


Kama nilivowahi kusema katika baadhi ya hoja zangu zingine ni kwamba kwa kuwa Tanzania ina viongozi ambao huutaka ubunge kwa minajili ya kujitosheleza kimaslahi, kwa kujilimbikizia mali na kufanya biashara badala ya kushughulikia wananchi na kuleta maendeleo.

Wananchi ndio wa kulaumiwa kwa kushindwa (kwa makusudi) kuchanganua yale yanayosemwa katika kampeni za wagombea ubunge na kufikia uamuzi wa kuchagua mbunge bora.



Hongera Dr. Mwakyembe.
 
Naona tunapotezeana muda na Taifa letu haliwezi kujifunga katika nyuzi za kashfa miezi nenda miezi rudi. Haiwezekani watu wale wale waendelee kutuumiza vichwa kana kwamba katika Jamhuri mzima wenye akili timamu ni wao tu!

Binafsi siyo tu nimechoka na kuandika kuhusu kashfa lakini nimechoka na majina yale yale hadi inakuwa kama uchuro!

Mgonja
Chenge
Rostam
Lowassa

Wanatoka sayari gani hawa kiasi kwamba kuwaondoa hadi tuliite Bunge la Mbinguni? Wana maslahi gani kwenye ofisi za serikali kiasi kwamba wanaweza kuendelea kuendeshwa katika magari ya serikali kama vile malaika wa kheri?

Mhe. Rais, sijakuomba vitu vingi muda mrefu ila sasa naomba nilete ombi rasmi, vunja baraza unda jipya. Jipya siyo kwa sababu ya uundwaji wake bali jipya kwa watu watakaokuwemo, majukumu yatakayosimamiwa nayo, na uwazi na uwajibikaji wa wananchi hao.

Kwa miaka nenda rudi tumekuwa na wanaume kama mawaziri wakuu, inatosha majaribio hayo, naamini Taifa letu liko tayari kuwa na mama ambaye anaweza kusimama na kufanya kweli maana inawezekana kwa kuwaangalia kina baba zaidi tumefunga macho kuona vipaji vingine!

Tengeza Baraza ambalo siyo tu litakuwa ni msaada kwako, bali litakuwa na lengo moja kubwa nalo ni kupiga vita ufisadi katika kila nyanja na sekta. Kupiga vita upotevu (isomeke ukwapuaji) wa fedha za serikali na matumizi mabaya ya ofisi na madaraka.

Mhe. Rais unasimama katika wakati wa pekee wa historia yetu, Watanzania hata wasiokubaliana na wewe au wasiokipenda chama chako kilichogubikwa na kashfa hizi nyingi ndani ya serikali yake, bado wanakuangalia wewe kama kiongozi wa Taifa lao.

Wakati huu wa pekee na ambao bila ya shaka ni wa tunu, unakutaka wewe kusimama hata ikibidi peke yako kufanya maamuzi machungu kama vile Rambo alivyojishona kidonde chake baada ya kuanguka toka kwenye genge (Kwenye First Blood - I hope you saw the movie.. )na wewe ushone kidonda cha kujitakia na ambacho kinazidi kujeruhiwa kwa mlundikano wa kashfa!

Bado ninaamini kuwa ukitaka kusafisha serikali yetu unaweza. Hauhitaji kibali cha kiumbe mwingine yoyote yule duniani, na hauhitaji kusikiliza ushauri wa mizimu na mapepo!

Katika hili lazima ujisikie mpweke na peke. Ujisikie kama mtu aliyeachwa nyikani na rafiki zake, wakati huu ni lazima ubakiwe na machozi ya uchungu kwani uliyekula naye chakula, ndiye amekuinulia kisigino!!

Mhe. Rais ongoza Taifa katika vita vya ufisadi, vita ambavyo maadui wako ndani ya serikali yako! Ni wewe uliye Amiri wa majeshi yetu yote! Pigana mwana wa Tanzania, na ufanya kama alivyofanya Wallace kwenye "Braveheart"! Pambana usirudi nyuma.

Vinginevyo, nafasi hii ikipotea, siyo tu wataanguka wasaidizi wako, bali na wewe mwenyewe utaanguka kama gunia la lumbesa kwenye kona za Tandale! Utabwaga chini kama manyanga ya wazaramo!

Jifunge kibwewe Kikwete, uliomba kazi, ifanye!
 
Grey Mgonja anakuwa "featuring" kwenye kila ripoti ya ubadhirifu, hivi ni kitu gani kinamfanya asiwajibishwe mpaka sasa? Hivi hili la BOT yeye limempitia kando kweli?
Naomba kueleweshwa, kwa nini ako kazini hadi leo wakati madudu waliyofanya na Balali yanatosha kabisa kumnyang'anya kazi?
 
Mgonja sii ndo ana nyumba ya zaidi ya 1 million USD Califonia US?

Hivi kweli hizi peza kama sii wizi na kupora huwa wanapata wapi?
 
bunge lipige vote of no confidence.. Kama kuna watu wako katika nafasi nzuri ya kupeleka petition basi tunaweza tukafanya hata onlibe petition alafu iwasilishwe kwa wabunge. This is inacceptable. Na JK akimuachia huyu jamaa apete then amuachie na Ballali. Lazma Lowassa aondoke.
 
Hii imeniacha hoi!...

"Lakini Mhe. Dk. Msabaha (Mb), baada ya mahojiano chini ya kiapo, akaiuma sikio Kamati Teule kuwa katika suala hilo yeye atakuwa kondoo wa kafara tu au, kwa maneno yake mwenyewe, “Bangusilo” kwa lugha ya Kizaramo. Maelezo hayo ya ziada nje ya kiapo ya Mheshimiwa Waziri yaliyotoa ujumbe kuwa “si yeye ila mkuu wake wa kazi”, yalioana na maelezo aliyoyatoa Balozi Kazaura nje ya kiapo tarehe 30 Novemba, 2007. Mara baada ya kumaliza mahojiano kwa kiapo na Kamati Teule, Balozi akatoa maelezo ya ziada kuwa Richmond ilikuwa mradi wa “Bwana Mkubwa” na “mshiriki wake mkubwa kibiashara”, akimaanisha Mhe. Waziri Mkuu na Mhe. Rostam Aziz (Mb)."...

...hii ni kali ya mwaka,maana mzee mzima analia kaa mtoto jamani huu ni wa bwana mkubwa mimi bangusilo tuu
 
Watu kutoka Sayari ya Dunia ni Wadunia.

Watu kutoka Sayari ya Zebaki( Mercury) ni Wazebaki.

Wazebaki wamevamia dunia na kuitawala kwa fimbo ya chuma kwa muda mrefu sasa.

Wazebaki kwa kawaida haogopi moto wala joto la namna yeyote ile.

Kwao Uzebakini Joto la kawaida latosha kuyeyusha chuma kikamiminika kama maji kwa sababu Sayari yao iko karibu sana na Jua.

Kwa muda mrefu tumejaribu kupambana na wazebaki hawa kwa kuwawashia moto mkali kabisa ili wazebaki hawa waachie ngazi lakini moto wetu umeshindwa kabisa kutimiza lengo letu.
Wote tumechoka na tunaelekea kukata tamaa na kudhani makucha yao watayasimika milele.

Kwa vile tunajua hakuna mzebaki hata mmoja anaweza kutezwa nguvu zake kwa moto au kwa joto kali la aina ya kidunia, tumeamua kutumia nguvu iliyo kinyume chake, yaani Baridi.

Moto huunguza lakini tunajua pia kwamba baridi nayo huunguza tena huunguza vibaya vizuri tu.

Tumeamua kwa pamoja kuwaunguza wazebaki kwa Baridi kali kama lile la Antactica.
Janja yetu inaelekea kufanya kazi vizuri sana inaelekea tayari wameanza kuungua vidole vya mikononi na miguuni,ncha za pua masikia na midomo yao pia imeanza kuungua.
Ili kuzidisha ukali wa baridi hili la kusini mwa dunia tumeamua kuanzisha upepo aina ya Kimbunga ili kuhakikisha kwamba baridi letu linazidi mara dufu.

Ninyi wazebaki mkiongozwa na MH sana Mamvi(Lowassa) muda wenu kwenye dunia yetu umekwisha, saa yenu ya kuelekea kwenu Uzebakini kula moto imefika.

Kama mlivyo kuja mikono mitupu kutoka kwenu uzebakini mtaipiga kwa heri dunia yetu mkiwa mikono mitupu vilevile.
Hatimaye Wa TZ tutapata fursa ya kuwatakia kila la kheri katika safari yenu ndefu na ya majuto ya kujitakia kurudi kwenu Uzebakini.

Tunamwomba huyo Mnaye mwamini na kumwabudu na aliye asili ya nguvu yenu ya kunyanyasa na kuwadhurumu watu awape maumivu makali na uchungu mwingi katika safari yenu ngumu na iliyo haki yenu kuelekea kwenu.

Mamvi na Troupe yako kikombe mlichotupia katika kututia Maumivu na machungu yetu nasi tutawapimia mara tatu na kuwaamuru mnywe mpaka tone la mwisho, na adhabu yenu itadumu mpaka siku ya kurudisha namba.
 
Nadhani hii skendo inavunja rekodi ya skendo zote nilizowahi kuzisikia japo kwa tetesi. Sasa hii si tetesi, ni ukweli wenyewe! Aibu kubwa mno. Na kama kweli Waziri Mkuu, Mawaziri wengine 2, AG, Katibu Mkuu, DG wa TAKUKURU wote watajiuzulu au kufukuzwa kwa mpigo, nadhani hii pia itakuwa "record"! Namsikitikia Donald Chidowu ni mshkaji wangu tulishawahi sota wote sehemu (kipindi nabangaiza ajira kwenye shule za private za Dar tulikula wote chipsi dume wakati anauza makala za habari za sheria kwenye "Mfanyakazi" na "Watu"), pole mtu wangu katika maisha kuna kujifunza, ndio kama hivi, nakuombea heri yaishe salama.

Pongezi kwa Dr Mwakyembe na kamati yake, wamefanya kazi kwa umakini. Sasa mkuu JK tunamwomba asisubiri nini wala nini, awapige chini tu waliotajwa, itatupoza kidogo kisha awakabidhi kwa IGP! (Duh noma ingine, ile kamati ya kumshughulikia Balali nayo imeingia kwenye msala! Si ndo hawa kina AG na TAKUKURU? I can feel the shock waves, I'm confused!)
 
Madela nimekusikia!! Ila ujumbe unaopenyezwa toka kwenye mkutano (bado unaendelea) ni kuwa EL amewagomea kujiuzulu kwani "hana sababu ya kujiuzulu" na kama nilivyosema jana, jiandaeni kwa hotuba ya kuomba radhi na defiance!

Hata hivyo, tetesi ambazo zinaingia taratibu kama mnyoo ardhini zinaonesha kuwa Mawaziri wawili tayari wameandika barua za kujiuzulu... na mida yoyote kuanzia sasa tutajua who is out first..
 
Au JK alikuwa anasubiri ngoma ikolee ndipo aghani wimbo wake? Tumeisubiri sana "single" ya baraza jipya, labda alikuwa anasubiri "producer" amkamilishie "beats"!
 
Grey Mgonja anakuwa "featuring" kwenye kila ripoti ya ubadhirifu, hivi ni kitu gani kinamfanya asiwajibishwe mpaka sasa? Hivi hili la BOT yeye limempitia kando kweli?
Naomba kueleweshwa, kwa nini ako kazini hadi leo wakati madudu waliyofanya na Balali yanatosha kabisa kumnyang'anya kazi?

Yaani hata mimi nashangaa kuwa bado anaamka asubuhi na kwenda Hazina kama kawaida. Yaani viongozi wetu hawana sense of responsibility hata kidogo. Kwenye ripoti hii yeye alikuwa kama star witness, akichangia jinsi MoF ilivyopinga deal la Msabaha. Lakini hii haifuti madhambi yake makubwa zaidi mengi.

Kati ya mapendekezo ya ripoti hii, ni kusitisha uteuaji wa wawakilishi wa wizara kwenye bodi za wakurugenzi kwenye mashirika husika. Hili ni la kulipa heko (ripoti yote ni ya kuipa heko)kwani mfano mzuri ni huyo huyo Mgonja. Yeye ndio katibu wa Hazina na mjumbe wa bodi BoT. Sasa akifanya maamuzi na gavana na kuafikiana naye (gavana ndio mwenyekiti wa bodi hii), akirudi wizarani na kupata instructions tofauti kutoka kwa waziri, huku si kumtia majaribuni na kutoa kauli zenye kukinzana?

Mzee Mwanakijiji, tafsiri yako ya Lowassa ni sahihi kabisa. Kamati Teule imemwambia kiutu uzima/kidiplomasia kuwa ajiuzulu. Kama ana macho ataona pale ripoti iliposisitiza "Maelekezo ya Waziri Mkuu" kwa kutumia bold font!! Watanzania wengi walifikiri kuwa hatimaye Sokoine amerudi pale Lowassa alipochaguliwa kuwa WM...tukasahau laana aliyoitoa Baba wa Taifa na kumfanya Lowassa atoe mshozi mnamo mwaka 1995.

Sasa tusubiri wengine ambao walikuwa kwenye timu ya BWM. Huu ndo utamu wa kukeep mawaziri wa awamu iliyopita kwani wizi wao ulianza zamani na sasa wameshikwa na itabidi wajieleze tangu wakati walivyoanza na kwa mtaji huo, BWM naye atakumbwa tu. Yaani Mgonja, Rostam, Yona, Lowassa na BWM wote wako kundi moja; ulizia wizi wowote wenye fedha za kitanzania zisiopungua tarakimu kumi (1 Billion Tshs), huwezi kukosa mikono ya hawa mabwana.
 
Mkjj:
Huenda umewasahau wengine mashuhuri wanaoweza ku-fit vizuri sana katika orodha hiyo hapo chini.

Lakini sidhani kuwa mtu kama Pesambili anaweza kusahaulika kamwe!
 
Kujiuzulu kwa Karamagi na Msabaha (ndicho ninachotegemea kusikia) ni long overdue. Watu tumelalamika hapa siku kibao posts zimejaza mamia ya kurasa! Dr Msabaha kwa kweli namsikitikia, lakini najiuliza nini kilimkosesha uzalendo wa kutamka ule ukweli wa lile neno lake la kizaramo (nikumbusheni!) ili Lowassa ahojiwe na Kamati? Kweli ni mbuzi wa kafara, lakini kafara haramu! Yaani anaona bora atemeshwe mzigo kuliko kumtaja mwizi? Hii tabia wanayo vibaka wazoefu, ukiwaona vibaka watatu wanaiba ukafanikiwa kukamata wawili, kamwe hawamtaji mwenzao hata wakiambiwa wanachinjwa! Sasa huu si ushujaa, ni ukibaka tu! Nitamsifu Msabaha kama atamwaga ukweli wote kwenye hiyo barua yake ya kujiuzulu, better late than never!
 
Back
Top Bottom