Inasikitisha sana kama Serikali imeamua kuminya utumiaji wa Mitandao kwa njia hii

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Nimefuatilia trend ya huduma za internet kwa mitandao kadhaa na kusema kweli hali ni mbaya na ya kusikitisha sana.

Kwa miaka kadhaa sasa, Serikali imejaribu mbinu mbalimbali za kubana uhuru wa watu kuongea. Siku za nyuma watu walikuwa wananyakuliwa kutokana na post zao. Lakini mbinu hiyo imeonekana kutofanya kazi sana.

Ambacho naona kinafanyika sasa ni kufanya gharama za vifurushi kuwa aghali mno. Nia ni kupunguza muda ambao watu watakaa kwenye mitandao, na mategemeo yao ni kuwa itasaidia watu wasifuatilie au kuchangia mijadala ya kisiasa inayoendelea.

Bei za vifurushi zimekuwa kubwa mno. Na si kubwa kwa sababu ya bei tu ya vifurushi lakini kiasi cha data ambazo unapewa kwa kila kifurushi kimepungua mno kiasi kwamba kwa vifurushi vingi, ndani ya siku moja mtu unalazimika kununua zaidi ya mara moja hata kama una matumizi ya kawaida tu.

Huu ni ushetani na sidhani kama utaleta faida wanazozifikiria. Sana sana inapunguza fursa za watu kupata elimu na kujifunza mambo ya msingi mitandaoni, kufanya biashara mtandao na hata kubadilishana mawazo na watu mbalimbali duniani ambayo mwisho wa siku yatasaidia kujenga nchi.

Wakiona wameshindwa huko kote watasema mtu haruhusiwi kununua zaidi ya kiwango fulani cha data kwa siku bila kibali maalumu! Tunapokwenda, ukiwa mnunuaji mkubwa wa bundle za internet unaweza kuwa suspect wa ugaidi!
 
Nimefuatilia trend ya huduma za internet kwa mitandao kadhaa na kusema kweli hali ni mbaya na ya kusikitisha sana.

Kwa miaka kadhaa sasa, Serikali imejaribu mbinu mbalimbali za kubana uhuru wa watu kuongea. Siku za nyuma watu walikuwa wananyakuliwa kutokana na post zao. Lakini mbinu hiyo imeonekana kutofanya kazi sana.

Ambacho naona kinafanyika sasa ni kufanya gharama za vifurushi kuwa aghali mno. Nia ni kupunguza muda ambao watu watakaa kwenye mitandao, na mategemeo yao ni kuwa itasaidia watu wasifuatilie au kuchangia mijadala ya kisiasa inayoendelea.

Bei za vifurushi zimekuwa kubwa mno. Na si kubwa kwa sababu ya bei tu ya vifurushi lakini kiasi cha data ambazo unapewa kwa kila kifurushi kimepungua mno kiasi kwamba kwa vifurushi vingi, ndani ya siku moja mtu unalazimika kununua zaidi ya mara moja hata kama una matumizi ya kawaida tu.

Huu ni ushetani na sidhani kama utaleta faida wanazozifikiria. Sana sana inapunguza fursa za watu kupata elimu na kujifunza mambo ya msingi mitandaoni, kufanya biashara mtandao na hata kubadilishana mawazo na watu mbalimbali duniani ambayo mwisho wa siku yatasaidia kujenga nchi.

Wakiona wameshindwa huko kote watasema mtu haruhusiwi kununua zaidi ya kiwango fulani cha data kwa siku bila kibali maalumu! Tunapokwenda, ukiwa mnunuaji mkubwa wa bundle za internet unaweza kuwa suspect wa ugaidi!
Ni jambo jema watu wafanye Kazi,tena bei zinatakiwa kulingana na nchi jirani..

Bei zetu ziko chini Sana matokeo yake watu hawafanyi Kazi Wanaishia kulaumu na kutukana .
 
Nimefuatilia trend ya huduma za internet kwa mitandao kadhaa na kusema kweli hali ni mbaya na ya kusikitisha sana.

Kwa miaka kadhaa sasa, Serikali imejaribu mbinu mbalimbali za kubana uhuru wa watu kuongea. Siku za nyuma watu walikuwa wananyakuliwa kutokana na post zao. Lakini mbinu hiyo imeonekana kutofanya kazi sana.

Ambacho naona kinafanyika sasa ni kufanya gharama za vifurushi kuwa aghali mno. Nia ni kupunguza muda ambao watu watakaa kwenye mitandao, na mategemeo yao ni kuwa itasaidia watu wasifuatilie au kuchangia mijadala ya kisiasa inayoendelea.

Bei za vifurushi zimekuwa kubwa mno. Na si kubwa kwa sababu ya bei tu ya vifurushi lakini kiasi cha data ambazo unapewa kwa kila kifurushi kimepungua mno kiasi kwamba kwa vifurushi vingi, ndani ya siku moja mtu unalazimika kununua zaidi ya mara moja hata kama una matumizi ya kawaida tu.

Huu ni ushetani na sidhani kama utaleta faida wanazozifikiria. Sana sana inapunguza fursa za watu kupata elimu na kujifunza mambo ya msingi mitandaoni, kufanya biashara mtandao na hata kubadilishana mawazo na watu mbalimbali duniani ambayo mwisho wa siku yatasaidia kujenga nchi.

Wakiona wameshindwa huko kote watasema mtu haruhusiwi kununua zaidi ya kiwango fulani cha data kwa siku bila kibali maalumu! Tunapokwenda, ukiwa mnunuaji mkubwa wa bundle za internet unaweza kuwa suspect wa ugaidi!
ndo muachage mambo ya kuangalia pono x videos na ni vzr ili watu wasipoteze mida yao kwenye mitandao.
 
😁😁😁

1630324497_1630324497-picsay.jpg
 
Ni jambo jema watu wafanye Kazi,tena bei zinatakiwa kulingana na nchi jirani..

Bei zetu ziko chini Sana matokeo yake watu hawafanyi Kazi Wanaishia kulaumu na kutukana .
Wajinga kama wewe hawaishi. Internet ni hitaji muhimu katika kukuza uchumi, hata kutengeneza ajira nyingi hivi leo.
 
Wajinga kama wewe hawaishi. Internet ni hitaji muhimu katika kukuza uchumi, hata kutengeneza ajira nyingi hivi leo.
Anadhani internet ni ngono tu maujinga kama haya ndio ccm wanataka ili waendelee kustawi.
 
Karibu Tanzania katika Taifa linaloelekea kufa kisa WALANCHI hawataki kuwaona raia wao wakiwa na HAKI, UHURU, USAWA na Demokrasia ya kweli.

Nimefuatilia trend ya huduma za internet kwa mitandao kadhaa na kusema kweli hali ni mbaya na ya kusikitisha sana.

Kwa miaka kadhaa sasa, Serikali imejaribu mbinu mbalimbali za kubana uhuru wa watu kuongea. Siku za nyuma watu walikuwa wananyakuliwa kutokana na post zao. Lakini mbinu hiyo imeonekana kutofanya kazi sana.

Ambacho naona kinafanyika sasa ni kufanya gharama za vifurushi kuwa aghali mno. Nia ni kupunguza muda ambao watu watakaa kwenye mitandao, na mategemeo yao ni kuwa itasaidia watu wasifuatilie au kuchangia mijadala ya kisiasa inayoendelea.

Bei za vifurushi zimekuwa kubwa mno. Na si kubwa kwa sababu ya bei tu ya vifurushi lakini kiasi cha data ambazo unapewa kwa kila kifurushi kimepungua mno kiasi kwamba kwa vifurushi vingi, ndani ya siku moja mtu unalazimika kununua zaidi ya mara moja hata kama una matumizi ya kawaida tu.

Huu ni ushetani na sidhani kama utaleta faida wanazozifikiria. Sana sana inapunguza fursa za watu kupata elimu na kujifunza mambo ya msingi mitandaoni, kufanya biashara mtandao na hata kubadilishana mawazo na watu mbalimbali duniani ambayo mwisho wa siku yatasaidia kujenga nchi.

Wakiona wameshindwa huko kote watasema mtu haruhusiwi kununua zaidi ya kiwango fulani cha data kwa siku bila kibali maalumu! Tunapokwenda, ukiwa mnunuaji mkubwa wa bundle za internet unaweza kuwa suspect wa ugaidi!
 
Wewe badala uchape kazi unataka kushinda mitandaoni ufuatilie umbea wa akina Wema Sepetu na Bugati, tena serikali inakosea sana, kifurushi cha chini kabisa ilibidi kiwe 10k na unapewa MB 200 tu! Wanaotumia mitandao kufanya biashara pekee ndiyo wangesajiliwa na kupewa vifurushi vyao maalum vya bei nafuu
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom