Inasikitisha na kuhuzunisha sana jinsi 'plants' za madini zinavyohatarisha maisha ya watu

Kumbuka pia kwenye hizi plants watu wanauza ramani...mwaka jana niliingiza senga kwenye plant fulani baada tu ya kuondoa carbon,kuna mwamba mmoja aliingiza senga kali sana lkn,dk za mwisho alivamiwa na kuporwa carbon yote,hata aliyefuatia aliporwa carbon tena so,ndani ya mwezi mmoja watu wawili wakaporwa na wengine kuuawa!

Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
Hilo nalo ni tatizo, kuna baadhi ya watu wanafanya biashara ya madini igeuke ya umafia kwa mambo kama haya.
 
Hii nayo ngumu kumeza, pamoja na ugumu wa maisha tulionao watanzania wenzangu bado uhai ni kitu cha thamani sana

Unakubalije kuingia Plant area bila PPE?
Kama wanaweza kula maandazi, chapati , vitumbua vilivyolowana maandishi ya magazeti nini kushika kemikali
 
kama mnajadiri matajiri wakubwa na sie tulio ktk makarasha ya kawaida mnatusaidiaje me niko chunya ila maisha ya kuendesha mitambo mbona poa tu
 
Dunia imeamua hivyo acha tuangamie. Hata maabara za kisasa hatari ipo palepale. Cha msingi mshauri mtoto wako asiende kuganta kazi hayo maeneo basi. Kuwazuia hao wenye migodi ni kupiteza muda.
 
Si kwamba awajui madhara,sisi waswahili ni watu wa kuupuza Sana mambo
 
Dunia imeamua hivyo acha tuangamie. Hata maabara za kisasa hatari ipo palepale. Cha msingi mshauri mtoto wako asiende kuganta kazi hayo maeneo basi. Kuwazuia hao wenye migodi ni kupiteza muda.
Sumu hizo hazitumiki kwetu pekee,sema atupendi kuchukua taadhari.
Mfano watu wanaambiwa mzitumie vyombo vya plastic uleta Kansa,awasikii,magazeti kufungia Vyakula ni sumu, kuweka chai au Vyakula kwenye mifuko ya plastic sumu tupu.
Hapo utamlaumu vipi Mungu sasa
 
Mkuu sidhan Kama umefanya tafiti sahihi kwasbb moyo wa plant wote utegemea mkemia. Mkemia fake si kuleta madhara kwa watu tu, Bali kuleta hasara kubwa kwa kutosababisha dhahabu ikamatwe kwenye cabon.

Kwa mmiliki wa plant au mtu aliyepeleka rundo kuozesha hawez kuwa na mkemia fake maana atajua yuko hatarin kupata hasara.

Jambo lingine zile kemikali ni hatari Sana kwa binadam na wanyana na hata mimea. Mfano sayanaidi ni sum mbaya, sidhan Kama kweli mtu anachezea maisha yake kijinga jinga.

Kama hiyo haitoshi sehem ya kujenga plant serikali kupitia watu wa mazingira NEMK, wako Makin Sana kutoa vibali haswa kwa kuangalia yale maji ya shimo la sumu.

So nakubaliana na wewe kwa kias kidogo, siyo plant zote Zina hatarisha maisha, uenda ni uko Kanda ya ziwa tu. Unaweza kwenda Kanda ya kati mfano pale dodoma kule NHOLI, plant zote ziko na wataalam na Serikali inasimamia usalama wa watu kwa ukaribu sana.
Ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya wakemia wanafanya kazi ktk plant si professional pia NEMC hawajui yanayoendelea uko plant kiufupi plant karibu zote za Kanda ya ziwa ni vyanzo vya uchafuzi wa maji.
 
Kaka kanda ya ziwa kuna shida sana kwenye issue za plant na elution suala la usalama na hata utunzaji wa chemical zinazotumika kuna shida kidgo japo siyo sehemu zote, kweny suala la mkemia hapa tukubaliane kwamba tanzania wakemia wa masuala ya madini wapo ila lazima tupate wakemia bora ili kupata faida nzuri tatzo ni kwamba hao pia wapo ila ni wachache sana, na ni kama serikali haijawekeza sana kwao na kwa watu wenye plant na elution hasa kwenye suala la elimu ya afya za watu, utunzaji wa mazingira na kuwa updated kila mara
Bro wakemia wengine ni wa kufundishwa juu juu na hao wengi n ma cheap labour hawana gharama na wanapendwa na maboss.
Wataalam wa madini (Processing engineers na technicians) wapo wengi ila wengi wao utawakuta kwenye CIP/CIL plants maana nyingi zinakua monitored na NEMC/TUME YA MADINI,ila hizi VAT leachings wengi wanatumia hao wa kemia wa kuunga wasiojua hata namna bora ya kufanya chemical handling na kusimamia afya zao na wafanya kazi wazungukao maeneo yao ya kazi.
 
Kingine cha kuongezea maboss wapunguze ujuaji na kuajiri cheap labours,Tume ya madini,Nemc na GCLA wawe wakali kwenye haya kuepusha athari za kiafya kwa wafanyakazi wa sekta ya uchenjuaji madini
 
Kiukweli nilibahatika kutembelea jumla ya plants za madini 9, tatu kahama Shinyanga na 6 wiliya ya Bukombe Geita. Nilichokiona na kukishuhudia kwenye plants hizo ni cha kuhuzunisha na kusitikisha sana haswa kuhusu afya za watu walioajiriwa kwenye hizo plants na wanaoishi kuzunguka hizo plants.

Plants hizo ambazo zinajihusisha na uchenjuaji wa dhahabu kutoka kwenye mchanga au mawe ni za watu wenye kipato cha kati na cha juu, ili kuendesha plants hizo, wataalamu mbalimbali wa kusimamia na kuendesha shughuli hiyo uhitajika.

Jinsi gani zinahatarisha afya za watu, niligundua baadhi ya mambo kama ifuatavyo

Kwanza
Wataalamu walioajiriwa ni unprofessional, hawana taaluma ya kile wanachokifanyia kazi. Hapa nitatolea mfano wakemia wanaotumika kupima na kuandaa kemikali zinazohitajika Kwa ajili ya uchenjuaji, cha kwanza kabisa katika plants zote hizo ni plant moja tu iliyokuwa na mkemia ambaye ni professional (na huyo anasema ndiye anaye wafundisha vijana), zilizobaki ni vijana wanachukuliwa mtaani na kufundishwa jinsi ya kupima na kuandaa hizo kemikali, vijana hawa kwa sababu hawana ujuzi zaidi kuhusu hiyo taaluma wanajikuta wakifanya kazi katika mazingira magumu sana.

Vijana wanaingia maabara bila vifaa maalumu vya kujikinga na kumwagikiwa au kudondokewa na sumu hizo za kemikali, katika hali ya kustahajabisha vijana hawa ushika kemikali kwa mikono na vifaa vya kemikali bila kujali, hapa ndipo wanajikuta katika matatizo ya kiafya kwani nilishuhudia baadhi yao wakikohoa damu, kucha kuchomoka, nywele kuungua, ngozi kubabuka n.k, baada ya kuwauliza Kwa nini jibu lilikuwa ni sisi "tumeshazoea haya ndiyo maisha yetu, tunajua tutakufa". Hii ni kwa sababu maabara hazikizi viwanga na ukosefu wa maarifa kuhusu good laboratory practices na laboratory safety.

Wakati nikiwa Bukombe, sehemu moja inaitwa namba moja, kuna plant moja kijana alikuwa anachanganya conc. Sulfuric acid kwa bahati mbaya sijuhi alikosea nini, kutokana na kuvuta hewa yake kwa sababu moshi ulitanda chumba kizima, alipiga kelele na kuomba msaada, wakati anatolewa kupelekwa kituo cha afya alisema hivi "siwezi kuona", kituoni aliambiwa sumu aliyovuta hawaiwezi ikabidi apelekwe hospitali ya wilaya Bukombe, kiukweli mpaka natoka kule kijana niliacha hajaweza kuona tena.

Pili
Uchafuzi wa vyanzo vya maji vinavyozunguka plants hizo, hapa ndipo kuna hatari kubwa sana ya watu wa kanda ya ziwa kupata cancer, kwani plants hizo hazina wataalamu wenye utaalamu wowote kuhusu "chemical speciation" na "waste management", hivyo hawajuhi chochote kuhusu bio-concentration, bio-accumulation concepts, hivyo kemikali hizo baada ya kuzifanyia treatment uzitoa kwenye mantenki na kwenda kuzitupa bila utaratibu, kwahiyo kemikali hizo utiririka hadi kwenye vyanzo vya maji kama mito na visima ,hali hii inapelekea maji wanayotumia kutoka kwenye visima na samaki kutoka kwenye mabwawa na hiyo mito kuwa na kiasi kikubwa cha kemikali hizo zenye sumu.

Pamoja na kwamba ni uchimbaji mdogo, lakini unahitaji utaalamu na usimamizi pia, wamiliki wa plants wanapata pesa nyingi, lakini hawajali kabisa kuhusu afya za watu, NEMC pamoja na ofisi ya mkemia mkuu mkuu wa serikali (GCLA) kwa kushirikiana na wizara ya madini chini ya serikali mnao wajibu wa kusimamia hili ili kuwanusuru watu kutokana na hizo sumu za kemikali.

Najua kuna rushwa kubwa sana kule, Ila wekeni nguvu, vijana mikono, miguu inatoboka tu, huku wenye plants wakivuna pesa.
INASIKITISHAA SANAA ANII HADII MOYOO UMEUMIAAA DAAAAAAAAH😭😭😭😭😭😭😭😭😭🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺
 
Asante Artificial Intelligence, Kwa hii
Unaweza saidia inbox migodi ambayo umetembelea bukombe namba moja Geita na ukakutana na kadhia hii ili tuungane kulisemea.
Tukipata muathirika wa haya kwetu wanahabar inakua nzuri Zaid.

Changamoto yetu toka lwa wamiliki wa migodi na.maafisa madini ni kuwa hawako wazi kwetu wakiamini wakisema migodi utafungwa jambo ambalo sio kweli.

Naomba picture na contacts za yule mhanga wa Migodi ya No 1 bukombe aliye haribika macho kwa kemikali.

lubangoseni@gmail.com
 
Naomba jina la mgodi huo wa no1, jina la mhanga na contacts zake
Ili tuone tunamsaodiaje kwa haraka.
Tumeguswa sana sana na hilo.
Asante kutujuza.
Wakati nikiwa Bukombe, sehemu moja inaitwa namba moja, kuna plant moja kijana alikuwa anachanganya conc. Sulfuric acid kwa bahati mbaya sijuhi alikosea nini, kutokana na kuvuta hewa yake kwa sababu moshi ulitanda chumba kizima, alipiga kelele na kuomba msaada, wakati anatolewa kupelekwa kituo cha afya alisema hivi "siwezi kuona", kituoni aliambiwa sumu aliyovuta hawaiwezi ikabidi apelekwe hospitali ya wilaya Bukombe, kiukweli mpaka natoka kule kijana niliacha hajaweza kuona tena.
 
Asante Artificial Intelligence, Kwa hii
Unaweza saidia inbox migodi ambayo umetembelea bukombe namba moja Geita na ukakutana na kadhia hii ili tuungane kulisemea.
Tukipata muathirika wa haya kwetu wanahabar inakua nzuri Zaid.

Changamoto yetu toka lwa wamiliki wa migodi na.maafisa madini ni kuwa hawako wazi kwetu wakiamini wakisema migodi utafungwa jambo ambalo sio kweli.

Naomba picture na contacts za yule mhanga wa Migodi ya No 1 bukombe aliye haribika macho kwa kemikali.

lubangoseni@gmail.com
siku siyo nyingi nimeibiwa simu ambayo ilikuwa na picha, contacts , na vitu vyangu vingine ndiyo maana nina siku nyingi sijaingia JF,hivyo kwa kukuwa umejitokeza kusaidia ngoja nifatilie upya ntaktumia.
 
Back
Top Bottom