Inasikitisha: Kama Nondo na mbao (Vitu Tangible) vinachakachuliwa na TBS/TFDA wapo, Nina mashaka sana na usalama wa maji ya chupa!

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,279
21,396
Habari ndugu zangu!

Nimefanya ziara/survey katika hardware mbalimbali jijini Dar es salaam kwa ajili ya maandalizi ya material ya ujenzi naotarajia kuufanya hivi karibuni!
Nilichogundua asilimia 95% bidhaa za nondo na mbao hazina urefu unaotakiwa!
nilikuwa na tape measure pamoja na Vernier caliper nikaamua kutumia akili yangu ndogo niliyopata enzi za secondary!
Kwa mujibu Wa TBS na standard ya nondo kimataifa zimewekwa kwa unene tofauti tofauti kulingana na uhitaji Zikitakiwa kuwa na Futi 40 ( zipo 4mm,6mm,....8mm,10mm,12mm,16mm......nakuendelea)

Lakini cha ajabu nilichogundua kutoka kwenye hardware karibu zote wana nondo zilizochakachuliwa zenye urefu Wa Futi 37 yaani futi tatu zimeibiwa kwenye kila nondo.
  • kwa maana hiyo kama nondo moja inaibiwa futi 3 ina maana ukinunua nondo 13 unakuwa umeibiwa nondo moja nzima kwahiyo utakuwa sawa na nondo 12 TU
  • Nikaamua kwenda kwenye mbao nazo nI yaleyale; mbao zinazouzwa kuwa ni futi 10 nazo zimechakachuliwa Futi moja haipo, nyingi zina futi tisa tisa tu;
  • nikaamua kuangalia unene Wa nondo; kwa mjibu wa vernier caliper yangu nondo za 16mm baadhi hazikutimia zilikuwa pungufu.
  • Flat bar na square pipe zote ziko pungufu!
  • misumari nayo ni milaini yaani inapinda kirahisi sana.
  • Ebu fikilia siku hizi hadi bajaji au vile vigari viyoriyori/kirikuu vinabeba nondo can you imagine urefu wa futi 40, ikikunjwa futi 20 ikabebwe kwenye chombo kama bajaji yenye futi 5? Obviously nondo zimekuwa fupi thus wanabeba!
Nimetafakari sana kama Mimi mwananchi Wa kawaida nisiye na utaalamu nimeyaona haya wazi; Hawa TBS na TFDA wanafanya nini hadi bidhaa inatoka kiwandani hadi kufika madukani?
  • Kama TBS wana kitengo cha Inspection viwandani, Je hizo nondo zilizochakachuliwa wao wanashindwaje kuziona ?
  • Kama bidhaa feki hizi zimetapakaa namna hii kuna umhimu gani wafanyakazi wa TBS kulipwa mshahara wakati hawaoni?
Kutokana na hili la Nondo na mbao zinazoonekana kwa macho ya nyama na mikono kushindwa kung'amuliwa na mamlaka tunazozitegemea,

Basi napata mashaka makubwa sana kama mamlaka hizi kama zinasimamia vyema hata ubora Wa maji ya kunywa tunayouziwa kwenye chupa toka kampuni mbalimbali!

  • Bahati mbaya haya yanatokea Wakurugenzi wapo!
  • Bahati mbaya haya yanatokea waziri yupo.
  • Bahati mbaya haya yanatokea viwanda vipo hapahapa nchini lakini havikaguliwi
  • Bahati mbaya haya yanatokea maduka na hardware zote zipo tena mbao na nondo huwa ziko nje lakini hazikaguliwi.
Kama bidhaa zetu zinachakachuliwa, Tusishangae Wageni na wachina wakijenga bongo kwa kuagiza bidhaa toka nchini kwao!
Screenshot_20190713-203927.png


****karibuni****
 
Sio huko huku uswahilini kuna juice za Ufresh,dawa za mbu za kuchoma ,kuna vipipi vidogo vidogo kama piriton vina sukari nyingi mno sizani kama zinapitia TBS kwani nina wasiwasi na ubora wake.Alafu hizi dawa za kichina wanazotumia dada zetu zimepitia kweli TBS .
 
Sio huko huku uswahilini kuna juice ya ufresh,dawa za mbu za kuchoma ,kuna vipipi vidogo vidogo kama piriton vina sukari nyingi mno sizani kama zinapitia TBS kwani nina wasiwasi na ubora wake.Alafu hizi dawa za kichina wanazotumia dada zetu zimepitia kweli TBS .
Halafu wanaouza wanajitangaza kuongeza shepu lakini hawaonwi, kibaya na kushangaza zaidi hadi wafanyakazi wao TBS baadhi wanapaka mchina
 
Bora umeliona hill Mkuu..mfano wale jamaa wauza mbao buguruni ndio michezo yao..zile tape measure zao zimeungwa..ukienda wanakuangalia kwanza..kuna watu wanaibiwa pale kila siku...
 
Bora umeliona hill Mkuu..mfano wale jamaa wauza mbao buguruni ndio michezo yao..zile tape measure zao zimeungwa..ukienda wanakuangalia kwanza..kuna watu wanaibiwa pale kila siku...
nimepita hadi huko nimejionea
 
Habari ndugu zangu!

Nimefanya ziara/survey katika hardware mbalimbali jijini Dar es salaam kwa ajili ya maandalizi ya material ya ujenzi naotarajia kuufanya hivi karibuni!
Nilichogundua asilimia 95% bidhaa za nondo na mbao hazina urefu unaotakiwa!
nilikuwa na tape measure pamoja na Vernier caliper nikaamua kutumia akili yangu ndogo niliyopata enzi za secondary!
Kwa mujibu Wa TBS na standard ya nondo kimataifa zimewekwa kwa unene tofauti tofauti kulingana na uhitaji Zikitakiwa kuwa na Futi 40 ( zipo 4mm,6mm,....8mm,10mm,12mm,16mm......nakuendelea)

Lakini cha ajabu nilichogundua kutoka kwenye hardware karibu zote wana nondo zenye urefu Wa Futi 37 yaani futi tatu zimeibiwa kwenye kila nondo.
  • kwa maana hiyo kama nondo moja inaibiwa futi 3 ina maana ukinunua nondo 13 unakuwa umeibiwa nondo moja nzima kwahiyo utakuwa sawa na nondo 12 TU
  • Nikaamua kwenda kwenye mbao nazo nI yaleyale; mbao zinazouzwa kuwa ni futi 10 nazo zimechakachuliwa Futi moja haipo, nyingi zina futi tisa tisa tu;
  • nikaamua kuangalia unene Wa nondo; kwa mjibu wa vernier caliper yangu nondo za 16mm baadhi hazikutimia zilikuwa pungufu.
Nimetafakari sana kama Mimi mwananchi Wa kawaida nisiye na utaalamu nimeyaona haya wazi; Hawa TBS na TFDA wanafanya nini hadi bidhaa inatoka kiwandani hadi kufika madukani?
  • Kama TBS wana kitengo cha Inspection viwandani, Je hizo nondo zilizochakachuliwa wao wanashindwaje kuziona ?
  • Kama bidhaa feki hizi zimetapakaa namna hii kuna umhimu gani wafanyakazi wa TBS kulipwa mshahara wakati hawaoni?
Kutokana na hili la Nondo na mbao zinazoonekana kwa macho ya nyama na mikono kushindwa kung'amuliwa na mamlaka tunazozitegemea,

Basi napata mashaka makubwa sana kama mamlaka hizi kama zinasimamia vyema hata ubora Wa maji ya kunywa tunayouziwa kwenye chupa toka kampuni mbalimbali!

  • Bahati mbaya haya yanatokea Wakurugenzi wapo!
  • Bahati mbaya haya yanatokea waziri yupo.
  • Bahati mbaya haya yanatokea viwanda vipo hapahapa nchini lakini havikaguliwi
  • Bahati mbaya haya yanatokea maduka na hardware zote zipo tena mbao na nondo huwa ziko nje lakini hazikaguliwi.
Kama bidhaa zetu zinachakachuliwa, Tusishangae Wageni na wachina wakijenga bongo kwa kuagiza bidhaa toka nchini kwao!

****karibuni****


Mkuu umeeleza vizuri sana, kama ungeweza kufanya hivyo kwa mabati na saruji, waya na gypsum powder ni wizi mtupu.

Chukua mfano mdogo wa bati la geji 28 la mwaka 1990 linganisha na bati la geji hiyohiyo la sasa tenabkutkka kiwanda kilekile cha Galco bati la Simba, fanya hivyo kwa mabati ya geji zote ndipo utaelewa nchi hii iko wapi
 
Nina uzoefu na viwanda vya nondo dar, vinatembelewa na maofisa wa TBS mara kwa mara, cha kusikitisha hua hawaji kukagua ubora/viwango vya nondo bali wao huenda kuchukua pesa na kuondoka.
Aisee! kwahiyo wanachukua pesa hawakaguwi! halafu wapo kazini
 
Thread iliyokwenda sana shule hii.

Mkuu unastahili pongezi za dhati kulifanyia uchunguzi jambo hilo na kubaini uozo uliotamalaki nchini Tz.

Si kwa bidhaa za ujenzi pekee, ni karibia bidhaa zote zinazozalishwa kwenye viwanda vyetu zina figisu mbalimbali!

Ukija kwenye bidhaa za vyakula zinazozalishwa kiwandani ndiyo usiseme!

Mafuta kwenye madumu hupunguzwa ujazo stahiki na sukari kwenye viroba hesabia!

Raia tukipendelea kununua bidhaa import, wanasema hatupendi vya kwetu!

Wakati hayo yakitendeka, waziri pa1 na wasaidizi wake anayeshughulika na viwanda yupo kwenye ofisi za serikali zenye viyoyozi, katinga na miwani mieusi akirotet kwenye viti vya magurudumu, hana mpango!

Jambo hili si geni, linafahamika siku nyingi.

Lakini hakuna hatua yoyote inayochukuliwa, nadhani linaachwa makusudi liendelee kwa ajili ya manufaa binafsi ya wenye viwanda, wafanyabiashara na viongozi ili kunyonya raia.
Zamani hon.
Magufuli alipokuwa akitumbua viongozi 'kabila hiyo' zembe, nilikuwa ninajawa na huruma.

Lakini hivi sasa ninashangilia sana kuona viongozi wa namna hiyo, mumiani wasiojali shida za watu, wakifukuzwa kidhalilishaji hadharani.


.
 
Thread iliyokwenda sana shule hii.

Mkuu unastahili pongezi za dhati kulifanyia uchunguzi jambo hilo na kubaini uozo uliotamalaki nchini Tz.

Si kwa bidhaa za ujenzi pekee, ni karibia bidhaa zote zinazozalishwa kwenye viwanda vyetu zina figisu mbalimbali!

Ukija kwenye bidhaa za vyakula zinazozalishwa kiwandani ndiyo usiseme!

Mafuta kwenye madumu hupunguzwa ujazo stahiki na sukari kwenye viroba hesabia!

Raia tukipendelea kununua bidhaa import, wanasema hatupendi vya kwetu!

Wakati hayo yakitendeka, waziri pa1 na wasaidizi wake anayeshughulika na viwanda yupo kwenye ofisi za serikali zenye viyoyozi, katinga na miwani mieusi akirotet kwenye viti vya magurudumu, hana mpango!

Jambo hili si geni, linafahamika siku nyingi.

Lakini hakuna hatua yoyote inayochukuliwa, nadhani linaachwa makusudi liendelee kwa ajili ya manufaa binafsi ya wenye viwanda, wafanyabiashara na viongozi ili kunyonya raia.
Zamani hon.
Magufuli alipokuwa akitumbua viongozi 'kabila hiyo' zembe, nilikuwa ninajawa na huruma.

Lakini hivi sasa ninashangilia sana kuona viongozi wa namna hiyo, mumiani wasiojali shida za watu, wakifukuzwa kidhalilishaji hadharani.


.
hawaoni haya kwa maslahi ya nani?
 
Back
Top Bottom