Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,129
- 18,741
Katika maongezi yangu na watu na usomaji wangu juu ya kifo cha RPC Mwanza, nimeshituka kugundua kwamba Watanzania wengi hatuguswi sana na kifo cha huyu RPC, na wengine hata kudai ingekuwa ni RPC wa Iringa ndio ameuwawa wangekunywa champaigne!
Hii ni dalili kwamba uhusiano wa jeshi la Polisi na Wananchi umeharibika sana! Polisi wanapaswa kujitahidi sana kurekebisha hili. Sijawahi kuona jeshi la Polisi linalofanikiwa kupambana na uhalifu bila ushirikiano na raia, na kwa Tanzania inaonekana wazi kwamba Polisi wamezorotesha sana uhusiano wao na raia wa Tanzania.
Hii ni dalili kwamba uhusiano wa jeshi la Polisi na Wananchi umeharibika sana! Polisi wanapaswa kujitahidi sana kurekebisha hili. Sijawahi kuona jeshi la Polisi linalofanikiwa kupambana na uhalifu bila ushirikiano na raia, na kwa Tanzania inaonekana wazi kwamba Polisi wamezorotesha sana uhusiano wao na raia wa Tanzania.