Inasemekana Young D karudia kubwia unga

Soso J

JF-Expert Member
Aug 17, 2011
1,976
1,220
Kheri ya mwaka mpya wana JF wote! Hii ndio habari ya kusikitisha baada ya msanii Young D kusemekana kurudia kubwia unga! Hii ni baada ya meneja wake Max kuonekana akichat na dada fulani kuhusu ishu hiyo kwenye mtandao wa Instagram.

e2bbe7223df1a870cb4453314be77f95.jpg
 
Makaburi hayajajaa. Atakayewahi kati yetu na yeye hima afukiwe.
 
Acha afanye kile roho yake inapenda.

Maisha yenyewe yako wapi, tunaiahi mara moja hivyo fanya kadri uwezavyo kufurahia maisha kadri moyo wako utakavyo.

Waacheni wafu wazikane.
 
Kwa mujibu wa meneja wa Young Dee, Maximillian Rioba, rapper huyo amerejea tena kwenye matumizi ya dawa za kulevya.

Max anadai amejaribu kila awezalo, lakini sasa ameamua kunawa mikono Amezitoa taarifa hizo Instagram alipokuwa akichat na msichana aitwaye Wendy Eliah.

tatu.png
moja.png
mbili.png
 
acha afe nao waache kiherehere cha kujidai wana wasaidia kabla hawajawa tayari kusaidiwa.....mchuma janga hula na wakwao.
 
Nasikia ni kiki ya nyimbo mpya sijui...idk...inaweza kua kweli though...

Maneno bila picha ni blah blah...tuone picha za youn D akiwa kwenye hiyo hali...
 
Kila kifo kinapangwa na Mungu ila hivi vya madawa ya kulevya vinapangwa na shetani, acha wafe tu ili wengine wajifunze, wasiokufa hakuna mtu atakayejifunza kuwa madawa ya kulevya ni hatari.
 
Namhurumia maana kujitoa mule kwenye janga sio rahisi kwa mwezi mmoja au miwili kama wafanyavyo wasanii wetu.
 
Hii staili ya kuacha unga ya wasanii ndio uwa inanishangaza.. Unaachaje unga kirahisi hivyo!

Wasanii wetu wakae wakijua unga hauna mjanja.. Unga ata uufiche vipi kuna siku utakuumbua tu... Tunasubiri wajanja kina Mr blue, TID, Babuu, Mox, Majani, Bushoke ,Q chilla nk tuuone mwisho wao .

Btw hivi Tippo wa Zizu yupo wapi? Ana dhambi nyingi sana huyu jamaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom