Inaonesha hila alizofanyiwa mfanyabiashara Ramadhani Ntunzwe zilikuwa na baraka za Serikali ya awamu ya tano

James Martin

JF-Expert Member
Apr 2, 2016
1,206
1,509
Tangu mwaka jana nimekuwa nikimsikiliza mfanyabiashara Ramadhani Ntunzwe anavyosumbuliwa bila kupata ufumbuzi.

Nina imani kabisa rais wa wakati huo kama kweli alikuwa na nia ya kumaliza jambo hilo lisingechukua muda mrefu kiasi hiki.

Pia nadiriki kusema mateso aliyoyapata huyu mfanyabiashara yalikuwa na baraka zote za mkuu wa nchi wa wakati huo. Mteule wake Sabaya alikuwa akitaka pesa kwa nguvu kutoka kwa wafanyabiashara, siamini kama Rais alikuwa hajui.

Kwa uchambuzi wangu nafikiri aliyekuwa rais wakati huo alitoa "maagizo" huyu bwana atatuliwe matatizo yake kama geresha.

Hao watu wa wizara ya fedha kufanya naye kikao kama kumzuga tu na Rais lazima alikuwa sehemu ya mkakati huo.

Kama bwana Ramadhani atakuwa anausoma uzi huu, watu wa wizara ya fedha hawakukuita kutatua tatizo bali ni kukulagai tu.

Sababu ya kwanza Rais kutoa "maagizo" ni kwamba huyu mfanyabiashara alipaza sauti kubwa kupitia vyombo vya habari. Ilibidi Rais ajifanye anamsaidia ili kujitoa lawama.

Sababu ya pili ambayo ni kubwa ni uchaguzi ulikuwa umekaribia. Kujifanya wanamsaidia huyu bwana ilikuwa ni njia ya kumnyamazisha kwenye kipindi cha uchaguzi. Wapinzani wangeweza kuitumia kesi ya huyu bwana kuipaka matope serikali ya awamu ta tano.

Kama kweli Wizara ya Fedha ilikuwa inataka kumsaidia bwana Ramadhan Ntunzwe ilikuwa na uwezo wa kufanya uchunguzi wake wa haraka kama wao wenyewe kuwasiliana na mahakama kujua kama kesi ilifunguliwa, kuhakiki stakabadhi za TRA, kuwasiliana na polisi n.k. Nchi za dunia ya kwanza wanaita multi agency cooperation.

Hivi vyombo vyote vingeweza kufanya kazi kwa pamoja kutatua hili tatizo kwa haraka bila kumlaghai huyu bwana kwa kumsumbua aende kwenye "mikutano"
 
Ukifuatilia maongezi yake utangua tofauti ya awamu ya tano na hii ya sita katika kushughulikia matatizo ya wananchi. Halafu TRA(RUSHWA) na JESHI la polisi(KUPIGA MADILI)
 
Inasikitisha sana kwa manyanyaso anayopewa na anayoendelea kupewa mhusika. Ni vema Mhe. Rais aliye madarakani kwa sasa alimalize suala hili haraka iwezekanavyo. Kwani madai kama Ths. billioni moja kama fidia kwa mhusika mbona ni fedha kidogo sana kwa Serikali?.

Suala hili ni la muda mrefu na Mhe. Rais wa awamu ya tano kama angekuwa bado hai tayari mhusika angekwishalipwa fidia yake.

Baada ya Mhe. Rais kufariki mambo yamerudi kama yalivyoanza ya danadana. Kwa nini Wizara ya Fedha mnashindwa kulitatua tatizo hili?

Kumbe mlikuwa mnamuogopa Hayati Mhe. Magufuli lakini ikumbukwe Rais ni taasisi na huyu aliyepo madarakani bado ile amri ya Mhe. Magufuli bado ni amri yake.

Sasa suala hili lifikie mwisho.
 
Kwa kilio chake alichotoa na sehemu anayotokea huyu....
Lazima alimwachia mungu

waliyomfanyia huyu mfanyabiashara mpaka sasa sijuwi watakuwa kwenye hali gani????

Ova
 
1642477659658.png

Una kula kwa urefu wa kamba yako.
 
Ukifuatilia maongezi yake utangua tofauti ya awamu ya tano na hii ya sita katika kushughulikia matatizo ya wananchi.....Halafu TRA(RUSHWA) na JESHI la polisi(KUPIGA MADILI)
Hakuna utofauti wa tawala wote Bado wanamtesa tu huyu Jamaa
 
Kwa kilio chake alichotoa na sehemu anayotokea huyu....
Lazima alimwachia mungu

waliyomfanyia huyu mfanyabiashara mpaka sasa sijuwi watakuwa kwenye hali gani????

Ova
... kwanza pole nyingi san kwake; inakera mno pale ambapo mamlaka zilizotegemea zimsadie mwananchi zinamnyanyasa bila sababu. Anatokea sehemu gani ambako ni watu wa mungu kwa kiwango kilichotukuka namna hiyo?
 
... kwanza pole nyingi san kwake; inakera mno pale ambapo mamlaka zilizotegemea zimsadie mwananchi zinamnyanyasa bila sababu. Anatokea sehemu gani ambako ni watu wa mungu kwa kiwango kilichotukuka namna hiyo?
Kigoma mojaaa ile

Ova
 
Ondoa kinyongo zungumza ukweli unaposikiliza maelezo ya huyu mfanyabiashara.Kwanini utekelezaji wa maamuzi ya vikao umesimama tu baada ya kifo cha rais aliyepita?Maanuzi yalishafanyika kwanini hawa viongozi waliopo hawatekelezi?
 
Back
Top Bottom