Jehanamu Hii
Member
- Dec 16, 2016
- 41
- 31
Raia anatakiwa kuwa msingi wa mawazo. Yeye ndiyo wa kusikilizwa kwanza. Bila raia hao viongozi wangekuwa madarakani? Si sisi ndiyo tunaowalipa kwa kutumia kodi zetu na kuwapa uhalali wa kutawala mali asili za nchi kama zive machimbo ya madini, mbuga za wanyama, ardhi inayotoa gesi n.k ili zitutuletee faida sisi? Cha kushangaza naona viongozi ndiyo msingi wa mawazo--kwenye nchi yetu, na nchi nyingine za kimaskini nikimaanisha nchi nyingi za Kiafrika ukiachilia mbali Tanzania! Wao ndiyo wamegeuka kutoa amri ya nini tufanye badala ya kujaribu kutusikiliza tunahitaji nini. Mbaya zaidi, elimu yetu na maisha yetu kwa ujumla, hayamjengi mwananchi au mtu kudai haki yake. Inamjenga kufuata amri tu. Dhana ya kufuata amri tu bila kuulizia, inaanzia toka ngazi ya familia nikimaanisha mtoto na mzazi. Mtoto=fuata amri za mzazi bila kuuliza swali, mwanafunzi=fuata amri za mwalimu bila kuuliza swali, raia=fuata amri za viongozi bila kuuliza swali!!! Inasikitisha sana. Kwa mtindo huu tunakosa 'changamoto' ambayo ndiyo kichocheo cha mabadiliko. Hakuna mabadiliko pasipo changamoto! Nchi inayoogopa changamoto kama vile viongozi kukosolewa, haiwezi kuendelea.