Michael Scofield
JF-Expert Member
- Jul 30, 2011
- 1,225
- 471
Hii kusema kweli sijaelewa serikali ya mkoa wa Dar es salaam, ilichokifanya kuwabomolea watu makazi yao huko Mabwepande. Hili sijajua tafsiri yake kama waliyajalii maisha ya wakazi wa jangwani, inakuwaje wakazi wa mabwepande hawawajali? wako katika nchi gani? chini ya serikali gani?
Nadhani swala lilikuwa ni busara tu ya kuwatambua, na kisha kuwawekea taratibu ili wazifuate, kama vile wawapimie viwanja kisha wavilipie, kuliko kuingiza greda na kuwavunjia makazi yao. na kuwaacha wakitaabika na watoto wadogo, wazee, wagonjwa.
Nadhani serikali ya mkoa wa Dar es salaam kuna haja ya kuwafikiria wananchi hawa walio ktika wakati mgumu.
Nadhani swala lilikuwa ni busara tu ya kuwatambua, na kisha kuwawekea taratibu ili wazifuate, kama vile wawapimie viwanja kisha wavilipie, kuliko kuingiza greda na kuwavunjia makazi yao. na kuwaacha wakitaabika na watoto wadogo, wazee, wagonjwa.
Nadhani serikali ya mkoa wa Dar es salaam kuna haja ya kuwafikiria wananchi hawa walio ktika wakati mgumu.