Inakuwaje Rostam aliyekataliwa leo ndo anapiga kampeni kupata mrithi wake mwenyewe?

luckman

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,211
371
Miaka 50 ya uhuru inanionesha mengi sana chini ya jua! ndani ya nchi yenye asali na maziwa vilivyogeuzwa kuwa shubiri kwa watanzania walio wengi, Unapokuwa unafanya jambo fanya ukiangalia na kupima impact zake baada ya mda fulani! Nadhani wote tulishuhudia kampeni ya wenzetu walafi na wasio na uhuru na wanachi, walivyo anzisha vua magamba theory ingawa kada mmoja alijitoa mwenyewe kutokana na shinikizo la magambazi senior!leo mtu huyohuyo, wa eneo hilihilo anatumika kupigia chama kilikile, kilichomfukuza kwenye kiti kilekile kumpigia kampeni mtu achukue nafasi ileile, na yeye huyohuyo anakubali kupigia chama kilekile alichosema kina siasa uchwara, napata wasiwasi juu ya hili ila maswali kadhaa yanakuja akilini na kujiuliza inakuwaje hii?1.Alishinikizwa kupiga kampeni na chama chake?2.Je mbona kati ya watuumiwa wote kwa nini yeye ndo kabaki, ni sababu ya uraia wake na rangi?3.Wanajikomba kwake ili zile outlets zisifungwe?4.Hajiamini na biashara zake kutokuwa na uhalali wowote5.Alikuwa anakubalika au alikuwa ananunua ushindi?6.Je ni kipi anakisema anaposimama ulingoni??Sielewi kabisa katika hili,JAMAA WAMEENDA MBALI SANA HADI WAKAMUITA MANGULA, KONDOO ALIYEKATALIWA TANGU MWANZO WA PHASE YA KWANZA LEO AMEKUWA LULU? na yeye kakubali vp? napata shida sana juu ya hili!!!!!!!!!!wanajamvi mi nawasilisha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom